Jumbe Tambaza: Alimsomea Nyerere dua nyota yake ikang'ara

ACHA NA MIMI NIFUTE WATU TONGOTONGO KIDOGO KISHA MWISHONI NITAZUNGUMZA KUHUSU HIZO DUA AZLIOFANYIWA HAYATI MWL J.K NYERERE

Maisha yamegawanyika katika sehemu kuu mbili:-
1. Ulimwengu wa roho
apa namaanisha ulimwengu usionekana kwa macho ya kawaida, hapa ndipo tuaminipo ktk Mungu na Ibilisi.
2. Ulimwengu wa nyama
ulimwengu ni katika vitu vyote ambavyo tunaviona kwa macho yetu ya kawaida.
Nianze kusema kuwa, Taifa la Tanzania limefika hapa lilipo kutokana na makosa yaliyofanywa na waasisi wa hili Taifa na wale ambao wapo pia madarakani ila sana sana ni waasisi, kwanini? kwasababu muasisi wa taifa ama waasisi wa taifa ni LANGO la taifa.

Lango ni nini? Katika tafsiri ya kawaida lango ama mlango ni sehemu inayopitisha kitu ili kuingia ndani, kama tunaona katika ulimwengu wa nyama kuwa ipo mipaka ya nchi ambayo mtu, wanyama n.k huingia ndani ya nchi husika, vivyo hivyo ipo milango ama lango katika ulimwengu wa roho ambao unapitisha mambo ya rohoni ndani ya nchi.

NOTE: Chochote ukionacho katika ulimwengu wa macho ya nyama, tambua kimeanzia rohoni. Hata katika uumbaji Mungu alianza kumuumba mwanamke na mwanaume ktk ulimwengu wa roho kisha ikaja kudhihirika ktk ulimwengu wa nyama.

Mnamo mwaka 1961, baada ya Waingereza kuiachia Tanganyika, waasisi wa hili Taifa wakiongozwa na Nyerere walitegemea saana ama niseme ni waamini wa ulimwengu wa roho ktk ufalme wa giza, hivyo walienda kwa wachawi wa nchi ama waganga ili kupata maarifa na akili ya kuiongoza nchi.

Moja ya vitu ambavyo vilitokea kwao ni kutopata tu maarifa na akili bali pia walitakiwa wakubali wachawi mazindiko ndani ya nchi, chama cha siasa TANU ambacho sasa hivi ni CCM kuzindikwa ama kuongozwa na serikali ama tawala za kuzimu Tanzania.

Nisizungumze mengi, nikatishe kwa kusema kuwa Mwl Nyerere kama kiongozi wa nchi ama muasisi wa Taifa hili, ndie alikuwa lango la kupitisha falme za giza ndani ya nchi ya Tanzania ambapo hata yeye mwenyewe hakujua kama haya anapitisha haya mambo ambayo yaliicost Tanzania kipindi kile na hata sasa. Hayati Baba wa Taifa angejua kama kupitia yeye anapitisha haya mambo wala asingekubali na kama angekuwa na nguvu ya kujinasua angefanya hivyo ila kwa bahati mbaya hakuwa nayo.


TURUDI KWEYE MADA
Dua alizosomewa Hayati JK Nyerere ndizo tunazoita ushirikina sana sana katika kusafisha Nyota, kwanini?
Mungu anapomuumba mwanadamu huwa anamuumba kwa jinsi yake nikimaanisha vinasaba, mtazamo, akili, nyota, hekima, maarifa n.k ila viongozi wengi wa nchi huwa wanapewa akili ya ziada na kupandikiziwa nyota ambazo sio za kwao. Wachawi/Waganga wana uwezo wa kutambua nyota ya mtu tangu akiwa mtoto na wana uwezo wa kutoa nyota yako na kumhamishia mtu mwingine, sio nyota tu bali hata nafsi na mengineyo.

Hayati Baba wa Taifa ni moja ya viongozi waliveshwa nyota ambazo hazikuwa ni za kwao, hizo nyota wachawi/waganga wanazimiliki sana huko kuzimu.

Embu jaribu kutafakari, endapo kweli Mwalimu Nyerere alikuwa na vinasaba vya uongozi, je katika watoto wote aliokuwa nao hakuna hata mmoja ambae ana vinasaba vya baba yake? HAKUNA, endapo uongozi wake ile hekima na maarifa na nyota yake alipewa na Mungu katika uongozi basi kati ya watoto wake wote alokuwa nao yupo mmoja walau angekuwa na characters kutoka kwa baba yake.

Watanzania tusiwasifu sana hawa wasomaji dua hususani wanaojiita wazee wa Dar es Salaam, ni washirikina wakubwa mno, maisha tunayoishi leo Watanzania ni matokeo ya maagano ya kuzimu na watawala wetu ndio maana leo hii akili za watanzania zimefungwa kutokana na yale mazindiko. Mtawala anaweza akafanya chochote na watanzania wasichukue hatua, UFISADI, WANYAMAPORI, DEMOKRASIA N.K watanzania tunalalamika kwa muda ila watawala kupitia wachawi wa nchi wanazima akili za watanzania na hawahoji tena wala hawakumbuki.

kwa leo nitaishia hapa ila ipo siku nitaandika kwa mapana mno kuhusu haya mambo, kwa wale msionielewa mnisamehe, sina kipawa cha kufindisha na haya nimeyaandika ghafla ila ipo siku nitayaandika kwa mpangilio mzuri kabisa.
 
nakubaliana na wewe mkuu kwa fact kwamba Waislamu/Wakristo walei wanaweza kujichanganya bila kuulizwa maswali lakini si viongozi (sheikhs, wachungaji, etc). huu ndiyo muktadha wa swali langu kwa sheikh Mo Said.
Ndugu zangu,
Katika hizi dua na matambiko kwanza napenda nikufahamisheni kuwa
Nyerere si wa kwanza kufanyiwa hizi dua.

Wakati nafanya utafiti katika kuandika kitabu cha Abdul Sykes kwa
mara ya kwanza nilikutana na dua katika kisa cha ugomvi baina ya
Abdul Sykes na Mzungu aliyekuwa ''boss,'' wake aliyevamia ofisi yake
ya Market Master Kariakoo Market akamkuta Abdul anauza kadi za
TANU na nyingine anazo katika mtoto wa meza.

Wafanya biashara pale sokoni kwa kuhofia kuwa Abdul atafukuzwa
kazi waliamua kufanya dua.

Nimeelezwa kila kitu nini kilifanyika katika dua na katika makubwa
zaidi na nini yalikuwa matokeo yake.

Inatisha.
Hii ilikuwa 1955.

Sikuweza kukiandika kisa kile katika kitabu na siwezi leo kukihadithia
hapa.

Abdul hakufukuzwa kazi ila aliyepata shida ni Mzungu na TANU ikazidi
kuimarika na Abdul kaendelea kuuza kadi zake za TANU sokoni Kariakoo.

Dua nyingine ilikuwa ya Rashid Ali Meli aliyetoa fedha katika sefu yake
kazini akiwa Mtunza Fedha wa Dar es Salaam Municipal Council akampa
Idd Faiz Mafungo itiwe kwenye mfuko wa safari ya Nyerere UNO 1955.

Wakaguzi walifika siku ya pili kufanya ukaguzi na ikawa hatari Rashid Ali
Meli
atafungwa kwa ''wizi.''

Walipofungua sefu fedha walizikuta zote kamili hakuna hata senti moja
iliyopotea.

Special Branch walikuwa wametoa taarifa zisizo shaka walizopewa na mtu
wao ndani ya TANU tena kiongozi wa juu kabisa.

Dua nyingine 1956 iliyofanywa Lindi na Sheikh Yusuf Badi Nyerere
akiwapo.

Tabu kuamini yaliyotokea usiku ule.
Sijaweza pia kuandika katika kitabu cha Abdul Sykes.

Dua ilifanyika nyumbani kwa Suleiman Masoud Mnonji Mtaa wa Makonde.
Hii ilikuwa 1956

Dua nyingine ni ya Mnyanjani kuhusu Kura Tatu mwaka wa 1958.
Sishangai kuwa leo watu wanatatazika na historia hii.
 
Mohamed Said,
shukurani sheikh Said kwa kutushirikisha historia hii iliyotukuka.

katika ufafanuzi, umeegemea zaidi upande wa dua - upande huu sina matatizo nao kwani siku zote ninaamini kuwa Mungu (Allah) ndiye muweza katika yote.

tatizo langu lipo kwa viongozi wa dini kuchanganya dua kwa Allah na matambiko kwa miungu wakati wakimuombea Mwalimu JKN.
hili bado hujalijibu sheikh.

wasi wasi wangu, genuinely speaking, ni nini?

kwa miaka nenda rudi nchi yetu iliyosheheni neema kubwa ya mali asili imekuwa ikipiga mark time kiuchumi. wasi wasi ni kuwa isijekuwa Mungu (Allah) labda alituachia laana kupitia Mwalimu baada ya viongozi wetu wa dini ku blend ibada za Mwenyezi Mungu na yale matambiko ya miungu.
 
M-mbabe,
M Mbabe,
Wa kujibu hayo si mimi kwani mimi si niliyefanya hayo.

Mimi kama mwanahistoria nimeeleza yale niliyoyakuta
katika historia ya TANU.

Hayo niliyoweka katika kitabu cha Abdul Sykes ni madogo
sana.

Kipande hiki kinatisha na ndiyo sikuweza kuwa na ujasiri
wa kuyaandika yote niliyoelezwa.

Lakini nitakufahamisha kitu hawa wote waliofanya haya
wakiamini kuwa walikuwa sawa.
 
sawa. nimekusoma sheikh.

nirudi kwako wewe binafsi....

ninaamini wewe ni muumini mzuri wa Uislamu.
swali langu kwako - jee, unaona walichofanya ma sheikh wetu kuchanganya ibada (Mungu vs miungu) ni sawa au si sawa from Islam doctrine perspective?
 
Historia nzuri sana, inatufundisha kukaa na wazee tupate hekima zao. Je viongozi wa sasa wanaweza kujishusha hivyo na kupata baraka na ushauri wa wazee?
 
Mzee Mohamed Said, umeongelea kuhusu shule ya Azania kujengwa na wahindi, ila nafikiri umetatanisha kidogo, navyofahamu, Tambaza ndiyo ilikuwa Aga Khan Boys na zanaki, Aga Khan girls huku muhimbili primary ikiwa Aga Khan Primary.

Azania ilijengwa na serikali baada ya uhuru (ikiwa ni shule pekee ya sekondari ya kiume jijini huku Jangwani iliyojengwa na wajerumani ikibaki kuwa ya wasichana) kabla ya shule za Agha Khan kutaifishwa. Ndipo waismailia walipojenga shule yao mpya ya Aga Khan Mzizima sec school 1967.
 
Chamoto,
Muandishi wa makala hiyo ni Abdallah Tambaza si mimi.
Mimi nimeleta hapa.
 
sawa. nimekusoma sheikh.

nirudi kwako wewe binafsi....

ninaamini wewe ni muumini mzuri wa Uislamu.
swali langu kwako - jee, unaona walichofanya ma sheikh wetu kuchanganya ibada (Mungu vs miungu) ni sawa au si sawa from Islam doctrine perspective?

M-mbabe,
Mimi si mtaalamu wa dini kuweza kujibu swali hilo.
Mimi ni mwanahistoria.

Shabaha yangu wakati naandika kitabu cha Abdul Sykes ilikuwa
kuwaeleza watu nini Abdul kaifanyia Tanganyika na kumfanyia
Nyerere na TANU.

Hivi ndivyo nilivyokutana na haya yote ya dua za usiku, Dar es Salaam,
Tanga na Lindi na kuwaleta katika historia ya TANU wazalendo hakuna
mtu alipatapo kuwasikia hata kwa mbali.

Niulize maswali katika historia hii.
 
Chamoto,
Muandishi wa makala hiyo ni Abdallah Tambaza si mimi.
Mimi nimeleta hapa.
Halafu wewe unataka sisi tuamini kila kitu wazee wako wa Gerezani walikueleza wakati mmoja kishashikwa ni mwongo na umeshindwa kumtetea na kutuambia wewe si mwandishi.
 
Mbase...
Jitulize na soma upya mjadala wangu na Chamoto na zingatia
nini ameniuliza na mimi nimemjibu nini.

Hapajakuwa na suala kuwa yaliyoandikwa si kweli.

Usiandike kwa ghadhabu ingawa historia hii kawaida yake toka
ilipoanza kuandikwa takriban sasa miaka 20 imekuwa ikichoma
nyoyo za wengi kwa bahati mbaya wewe ni mmoja wa hao.

Lakini muhimu ni kuwa mtu hana lazima ya kuamini hii historia
na wala sijakutaka wewe uamini ninayoandika na una uhuru na
haki ya kuona historia hii wala haikuwapo ni utunzi wa hadithi.

Historia ya Mzee Jumbe Tambaza sikuandika mimi kaandika
mjukuu wake Abdallah Tambaza.
 
Dah aisee historia kama hizi bora mmezidocument mapema kabla jua lenu kuzama

Mimi naifahamu upanga vizuri sana ule mskiti maamur umepakana na mgahawa mmoja zamani duka linaitwa *chetu wote*
Mle ndani kwa nyuma kuna mzambarau kweli kwenye zile flat za wahindi zamani usalama wa taifa na sasa kuna ofisi za mama Anna mkapa fursa sawa kwa wote

Swali langu ni je hayo makaburi ya wazee wako yako ndani mskitini au kwenye mgahawa wa chetu wote yule mangi kwa nyuma?
 
Ni kweli pia upanga kuna mi zambarau mingi sana kuanzia muhimbili kushuka mpk mitaa ya tunakopesha makao makuu aisee nimependa sana hili bandiko

Pia ilipo baa ya tairo nasikia palikuwa na machine ya kusaga ya kina mama Sophia simba hili nalo ni kweli?
 
Dah...Sijaelewa...nimekusamehe...ila nawe naomba uniwie radhi[emoji13]
 
Ukipata jibu nitag please



 
Huu ni ushirikina.
 
Hapa cha uongo ilikuwa lazima uruke kiunzi ukikamatwa km kawaida yako.
 
Uliyejinasibu kuwa upanga unaifshamu vizuri sana unaliuliza tena.wabongo ni nani aliyewaroga?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…