Juninho Pernambucano: Mpiga freekick bora kuwahi kumtizama

Juninho ata alipokua england epl pale middoz, ilikua hatari kila akienda kupiga faulo, asee maishani mwangu sijawaona kuona mpiga set pieces kama huyu.
mkuu umechanganya kidogo
juninho anayeongelewa hapa ni wa lyon sio wa middlesbrough
 
Sio lazima kila mchezaji nyota acheze hizo timu! Unamkumbuka All time goal scorer wa EPL? Unajua aliwika wapi na alistaafia wapi? Unamfahamu mtu alieitwa DEVOR SUKER? Hao waliwika pasi na kuchezea hizo timu ulizotaja!
DAVOR SUKER alicheza Arsenal
 
Juninho alikuwa ni mpiga faulo bora lakin haimaanishi hakuwa mchezaji mzuri, alikuwa mchezaji mzuri sana na ndio maana aliitwa national team mara kwa mara na katika mashindano makubwa, tatizo angecheza kwa nani, laiti kama angekuwa taifa kama uingereza basi 1st eleven ilikuwa inamuhusu kwa %98
 
Juninho ata alipokua england epl pale middoz, ilikua hatari kila akienda kupiga faulo, asee maishani mwangu sijawaona kuona mpiga set pieces kama huyu.
Juninho wa middoz si juninho huyu..
Pernambucano hakuwahi kukipiga uingereza.
 
Huyu jamaa kapata heshima kubwa pale Vasco da Gama,pale anafahamika kama Reizinho de Sao Januario Giant of the Hill or Reizinho da Colina The little King of the Hill. Pia jamaa ameimbwa kwenye chorus ya wimbo wa fans wa Vasco hii ni baada ya kuifungia Vasco goal la free kick dhidi ya River Plate ya Argentina huku River akiwa nyumbani kwake ikapelekea Vasco kutinga final ya Copa Libertadores.
 
hakuna sehemu ameipta bila kuonesha umwamba wake katika shughuli za mipira iliyokufa
 
Utasemaje master wa eneo moja,wakati timu ikiwa imezidiwa au kuwa nyuma kwa goal/goals wachezaji wenzake wanajitahidi kutafuta faulo popote karibu na lango la wapinzani na ikitokea anawaweka?hiyo ndio Plan B.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
100%

Huyo mwamba [emoji91][emoji91]

Ukuta hata wakae watu 30 atapitisha mpira[emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umenikumbusha mbali sana sio vijana was juzi hawa wanapiga kelele hapa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Utakuwa na makengeza wewe.

Nyuma ya mafanikio ya Olympic Lyon ya 7 years consecutive titles alikuwa Juninho Penambucano.

Lyon hawa walimtoa Real Madrid kwa miaka mitatu mfululizo kwenye UEFA champions League quarterfinals.

Juninho ndiye alikuwa fundi wa pale central midfield akitawanya mipira kama hana akili timamu.

Unazungumzia timu kubwa kutomhitaji ? Mbona Allan Shearer hakuwahi kuhitajiwa na hizo timu za Real Madrid unazozitaja hapa.?
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…