Junior Kasanga na raia wa China, wakamatwa wakitorosha dhahabu waliyochimba

Junior Kasanga na raia wa China, wakamatwa wakitorosha dhahabu waliyochimba

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Mkuu wa wilaya ya Ulanga, Ngolo Malenya na kamati yake ya usalama wamemkamata mwekezaji Mtanzania Junior Kasanga akishirikiana na watu wengine wakiwemo raia kutoka nchini China wakitorosha madini ya dhahabu waliyochimba kwenye mgodi uliopo kijiji cha Isyanga wilayani humo.

--
Serikali wilayani Ulanga mkoani Morogoro imewakamata watu saba akiwemo mwekezaji mzawa Junior Kasanga na raia wawili wa China kwa tuhuma za kutorosha madini ya dhahabu yenye thamani ya shilingi milioni 337.5 kutoka katika mgodi uliopo kijiji cha Isyanga wilayani humo.

Akizungumzia tukio hilo Mkuu wa wilaya ya Ulanga, Ngolo Malenya, amesema kuwa dhahabu iliyokamatwa ina uzito wa gramu 2,640 sawa na kilogramu 2.64 ambapo amebainisha serikali bado inaendelea kuwafuatilia wawekezaji wengine ambao wamekuwa na tabia ya kutorosha madini na kusababisha kupotea kwa mapato ya serikali.

Kwa upande wake Kaimu Afisa Migodi wilaya ya Ulanga, Edward Ngulinja, ameeleza awali wawekezaji hao walifika katika ofisi ya madini ya wilaya hiyo kwa ajili ya taratibu za kisheria ndipo walipo watiliashaka kuwa kuna udanganyifu wanafanya na kuvitaarifu vyombo vya ulinzi na usalama.

IMG_20210602_110052_997.jpg
 
Mkuu wa wilaya ya Ulanga Ngolo Malenya na kamati yake ya usalama wamemkamata mwekezaji Mtanzania Junior Kasanga akishirikiana na watu wengine wakiwemo raia kutoka nchini China wakitorosha madini ya dhahabu waliyochimba kwenye mgodi uliopo kijiji cha Isyanga wilayani humo.View attachment 1805686
Tutafika kweli?
 
Mkuu wa wilaya ya Ulanga Ngolo Malenya na kamati yake ya usalama wamemkamata mwekezaji Mtanzania Junior Kasanga akishirikiana na watu wengine wakiwemo raia kutoka nchini China wakitorosha madini ya dhahabu waliyochimba kwenye mgodi uliopo kijiji cha Isyanga wilayani humo.View attachment 1805686
Nchi imefunguliwa, acha mzunguko wa pesa uje mtaani
 
Uzalendo ni msamiati mgumu mnoo kwetu, sababu wizi unaanzia kwa wale tuliowaamini na kuwapa madaraka..

Kila mtu akipata nafasi anapiga tu, hata mimi ikitokea mazingira ya kupiga nitapiga(unafiki sipendi)

Bahati mbaya kwa mwamba kanaswa tu.
Asilimia kubwa ya waTanzania ni wezi ambao hawajapata fursa ya kuiba, hayo makelele unayoyasikia sio uzalendo ni chuki ya kupitiwa mbali na mgao huo.
 
Mtoa mada hii mbona hujaifanyia utafiti suala hili?wanatorosha kupeleka wapi?na WHY umetoa picha yao kabla hawajasimama mahakamani?

Nchi now inaendeshwa kisheria na sisi ni wajibu wetu kuishi kisheria,hawa ni suspects na haki zao bado zipo kama mimi na wewe,sasa ikitokea walikamatwa kimakosa na wakaachiwa huoni utakua umewakosea?maana kuwatoa hadharani tayari umeshawahukumu.
 
Mkuu wa wilaya ya Ulanga Ngolo Malenya na kamati yake ya usalama wamemkamata mwekezaji Mtanzania Junior Kasanga akishirikiana na watu wengine wakiwemo raia kutoka nchini China wakitorosha madini ya dhahabu waliyochimba kwenye mgodi uliopo kijiji cha Isyanga wilayani humo.View attachment 1805686
Wachina na Wakorea si ndiyo rafiki kindaki ndaki wa mwendazake?
 
Get rich or die trying
Tajirika au kufa ukijaribu! [emoji38][emoji38][emoji38][emoji23][emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji377][emoji377][emoji377][emoji125][emoji125][emoji125]
 
Ma nchi kama haya ambayo watu wake kuiba wanaona ni moja ya njia ya kujipatia kipato ni bora kuwa na viongozi madikiteta tu kwa maana democrasia haiwezi kufanya kazi kwa Africa hata siku moja .
Lakini wachina ni rafiki wakubwa dikteta magufuri kuanzia viwanda,madini,usalama na uchaguzi.
 
Ma nchi kama haya ambayo watu wake kuiba wanaona ni moja ya njia ya kujipatia kipato ni bora kuwa na viongozi madikiteta tu kwa maana democrasia haiwezi kufanya kazi kwa Africa hata siku moja .
Kama hata huyo kiongozi ambaye ni dikteta naye ni mwizi tu, inakuwaje?mfano mzuri tumeuona je ilisaidia huo wizi kuisha?
 
Uzalendo ni msamiati mgumu mnoo kwetu, sababu wizi unaanzia kwa wale tuliowaamini na kuwapa madaraka..

Kila mtu akipata nafasi anapiga tu, hata mimi ikitokea mazingira ya kupiga nitapiga(unafiki sipendi)

Bahati mbaya kwa mwamba kanaswa tu..
Aisee pole yake kwakweli bahati mbaya tu imetokea Kuna mtu kawachomea si bure
 
Back
Top Bottom