Jurgen Klopp kutimuliwa Liverpool ?

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Sasa ni dhahiri kwa mwenendo wa timu ya Liverpool , hakuna namna nyingine ya kuiokoa zaidi ya kumtimua kocha wake .

Mpaka dk 64 ilishatandikwa mabao 4-1 na timu ya kawaida sana ya Totenham Hotspurs , hakuna dalili ya kukomboa mabao haya , na hii ni ishara mbaya mno kwa Liver , Kwa ilipofikia Klopp atupiwe virago vyake timu ianze upya.

Klopp ni bingwa wa kuongea na kubwabwaja huku akisahau kwamba soka si sawa na Ngonjera .
 
Reactions: BAK
Hakuna timu isiyofungwa!
Jana tu "mropokaji"katulizwa.
Ligi bado mbichi .
 
Ahahahahaha duuh watu mna munkari kufungwa kawaida tu ligi bado
 
kumbe spurs ni timu ya kawaida sana
 
Jamani, tukubali kitu kimoja, liver ni timu ya kawaida siku hizi, tusilazimishe iwe timu kubwa kwa sasa. Walipo sasa ni saizi yao.
 
Mpira umechezwa vizuri tu, hilo ndo game siyo unaingia uwanjani umejihakikishia ushindi! Man U mwenyewe pamoja na kuwa na kikosi hatari kapgwa 2-1 sasa tatizo liko wapi? Liverpool wakifanikiwa kupata beki za uhakika itasaidia sana, Lovren na Matip siwakubali kihivyo! Labda VvD akitua Liverpool hiyo January itasaidia! Jana Liverpool kamiliki mpira vizuri tu wala siyo uzembe wa Jurgen Klopp!
 
Hivi kwenye timu zenye kikosi kikali Man U kumbe nayo imo !
 
Hivi kwenye timu zenye kikosi kikali Man U kumbe nayo imo !
Mkuu yakiingia uwanjani huwa yanatisha!! Ila yakifungwa huwa yanatepeta!! Sisi Liverpool tatizo letu ni mabeki. Jana tumemiliki mpira mwanzo mwisho, lakini tukipigwa shambulizi lazima tufungwe!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…