Wapendwa sana!
Ndio nimeingia Dodoma; kuiweka sawa familia ambapo muda wote tangu juzi nimekuwa nkiwasiliana nao kwa simu! kweli tumesawijika lakin pia kwa niaba ya familia nawashukuru wote kwa faraja zenu! kwa kweli kwa sasa ni kitu tunachokihitaji sana!
Kijana aliyefariki ndio alikuwa sababu kuu ya mimi kuwapa lifti wapiganaji wale yaani yeye pamoja na wenziwe kwa kuwa alikuwa na undugu na mtu ambaye aliwahi kunifundisha kazi huko miaka ya nyuma! kwa kweli huwa sitoi lifti na asilani kwa watu nisiowafahamu kabisa!
Lakini ndo hivyo yametokea;
Nawasiliana na wadau wangu wa kazi hapa Dodoma na pia familia kwa chochote kinachoweza kutokea! Woga upo siwezi kukataa.......ni kwa mara ya kwanza najikuta katika situation hii.........sina xperience ya chochote hivyo mawazo mliyotoa na mtayoendelea kutoa hapa nitayafanyaia kazi.
Labda nisahihishe kidogo kuwa kesi itaendeshwa katika mahakama ya wilaya ya Kilosa; hivyo nitasafiri kuelekea Mkikumi na hatimaye Kilosa katika tarehe zilizotajwa.
Asanateni sana
Guys sio pole nyingi zinatolewa hapa,yeah nakubali kutoa pole kwa marehemu na pia hata bwana M_J ila pia mwishoni ni kuangalia njia gani ya kuweza kumsaidia bwana M_J kwa ushauri au hata kwa lolote lile ambapo ataweza kufanikiwa huko mahakamani maana mahakamani sio sehemu ya kuchezea isitoshe imetokea ajali na mtu kafa so tujaribu kuangalia kama kuna njia yoyote ya haraka haraka ya kumsaidia jamaa.Hapa sasa ndio ubinadamu unapoonekana sio kwenye raha tu kusifiana bila mpango wowote........Nawakilisha!!
Guys sio pole nyingi zinatolewa hapa,yeah nakubali kutoa pole kwa marehemu na pia hata bwana M_J ila pia mwishoni ni kuangalia njia gani ya kuweza kumsaidia bwana M_J kwa ushauri au hata kwa lolote lile ambapo ataweza kufanikiwa huko mahakamani maana mahakamani sio sehemu ya kuchezea isitoshe imetokea ajali na mtu kafa so tujaribu kuangalia kama kuna njia yoyote ya haraka haraka ya kumsaidia jamaa.Hapa sasa ndio ubinadamu unapoonekana sio kwenye raha tu kusifiana bila mpango wowote........Nawakilisha!!