JWTZ mpaka leo imeshindwa kuajiri wasomi wenye vipaji halisi, sababu hizi hapa...

JWTZ mpaka leo imeshindwa kuajiri wasomi wenye vipaji halisi, sababu hizi hapa...

Mkuu Mwita Maranya nikuhakikishie tu kuwa duniani kote hakuna kozi za wasomi na wasiosoma. Mafunzo ya kijeshi yako standard no matter what. Ukiwa katika uwanja wa medani bahati mbaya masters yako haitokusaidia kama hujaiva kimbinu. Ndo maana hata corporal ambaye ni competent anaweza kuitikisa nchi. (Nadhani unamkumbuka Iddi Amini). Tena ukihudhuria vyuo vya nje huwezi amini, ni balaa zaidi. Wanakuambia kwamba technology fails, that is why we don't use it in training. Kule kila kitu ni manual tofauti uongo wanaopeana watu. Technology utafundishwa kwenye unit yako sio chuoni. Tatizo wabongo wanafikiri digitali ina affect basic soldiering, no way.Wale wanaotamani kuonda maisha wavumilie kupitia katika kikaango kwanza, ndo wakakae maofisini na bachelors na masters za mambo ya utawala.

Na pale mnaposema vipaji maalum I can't understand what you are driving at? Jeshini vipaji maalum hupelekwa Commando, PT na sehemu nyingine zinazohitaji outstanding performance. Sasa hivi vipaji maalum sijajua ni nini. Nadhani mnamfahamu Balati. He was the greatet leader of all time katika commando, na huyo ni mmoja tu. Alipata bachelor na masters akiwa karibu kabisa na kustaafu. Kumbe basi jeshini kuna askari wengi sana wenye military knowledge ya hali ya juu kuliko most of graduates. Siwapondi hawa, isipokuwa tu kuna notion fulani imejengeka kwamba wasomi wanachukiwa jeshini, lakini ukweli ni kwamba wanaojiita wasomi wengi wao hawapendi kupitia rigorous training. Wanataka watambuliwe usomi wao wakati wa mafunzo kwamba mimi ni daktari, mhasibu, mchimi, n.k. Wakati wa training haya mambo hayana maana yoyote, na ndipo competent corporal ukimtishia elimu yako atakuwa willing kukudhihirishia kuwa katika kile ulichofuata pale, yeye ni zaidi yako. Guys, it is the matter of self discipline, that's all it takes. Otherwise mtabaki ku-lament kila siku kama hamtaki kutambua kuwa military knowledge is a profession in itself.

Daktari akifuzu mafunzo atatakiwa kutibu majeruhi mstari wa mbele, bunduki begani.
Mhasibu atatumia bachelor yake kulipa mishahara mstari wa mbele (vitani mishahara hulipwa kama kawaida).
Logistician atafanya kazi kupeleka logistics frontline (tena hawa huwindwa sana vitani).
N.k. Sasa usipokuwa trained utaperform vipi majukumu hayo? Tusilewe na kazi za jeshi wakati wa amani, kikinuka watu huvua kombati na kujificha, don't be one of them! Just do your part and everything should be fine.

MILITARY TEACHES YOU HOW NOT TO DIE!!!!!!!!!!


Military-Training-Desktop-Wallpaper-1024x768.jpg
Naongelea MENTALLY UPSTAIRS wala SIO MANGUVU YA MWILINI. ELEWA MADA KWANZA NDO UCHANGIE SIO KUKURUPUKA TU. Mnajaza seva bure!
 
Asante Nyenyere,

Kama maandishi hayatoshi, picha imefunga kazi! Tatizo la wasomi vijana la kujiona bora kuliko wengine haliko jeshini tu! Hata uraiani ni hivyo! Maofisini ndo kabisa, na bahati mbaya huko wanadekezwa. Pelekeni hoja Serikalini, vijana wote wasomi waende jeshi miezi 4 kabla ya kupata ajira si serikalini tu bali hata Makampuni binafsi.
Kaka elewa maada inazungumzia nini? Elimu bila ubunifu hamtaweza kitu. Najua wengi wenu hapa ni wanajeshi ndo maana mnatetea tu bila hata kuelewa.
 
Maisha si lazima uwe mwajiriwa wa JWTZ tu, kama unajiona una CV ya kutisha tafuta Taasisi zingine ambazo zitakunyenyekea pamoja na unanga wako, kiburi chako na utovu wako wa nidhamu, kisha na mavyeti vya kununua toka ulikotoka !!
Kwa taratibu za kkawaida tu, ukishindwa kumheshimu mdogo, je huyo wa juu yako utamheshimu kweli kwa dhati au ndio unafiki !!
Jiunge na siasa uingie Bungeni, ili umalizapo tu kiapo uanze kuwahadaa Wa-tz kwa Mikataba ya kuliuza Taifa !!
Mkubwa sihitaji kuajiliwa jeshini nina ajira tayari tena ya kujidai kiafya cozi sina elimu ya kuunga unga ambayo ingenifanya nije jeshini ok! Jadli maada.
 
Huyo mmoja ya waliotimuliwa nini sasa unataalamu gani bana wenyewe wanakuambia kila kizi ina msingi wake hayo mengine baadae ubwana umetimuliwa nini sasa kazi ya maana kwingine unataka nini kazi ya maana umaana kwako tu inatusaidia nini sisi?
 
Acheni ujinga nyie na upuuzi wenu kakosea ni ll,m ,(legum magister)

we mwenyewe umekosea,angekua amesoma asingeshidwa kutofautisha kati ya LL.B na LLM,kwa kukusaidia tu LL.B-Lex Legum Baccalaureate(LL.B,Lex Legum Magister(LL.M)
 
Samahani mkuu sikufukuzwa Monduli wala sijawahi kujiunga JWTZ na wala sitegemei sababu naitaji kuishi kwa uhuru bila kushurutishwa. HAPA MADA NI KUWA MPAKA LEO TATIZO NI NINI? HOSPITAL MNATEGEMEA URAIANI TENA KWA KUNYANYASWA, WENGI WENU MKIJA HUKU MNADAI ETI LUGALO HAKUJITOSHELEZI SHIDA NINI KAMA SIO HUO UNDAVA WA TMA? H UWEZI AJILI MTAALAMU KWA KUMLAZIMISHA AU KUMSHURUTISHA LA SIVYO MTAENDELEA KUPATA WATU WASIO COMPTANT, KAMA HUYO ANAYETAKA KUJA NA MASTER YA LLB! SOMA HISTORY THE MOST SCIETIST WALIKUWA WANATULIA NDIO MAANA MAENDELEO YAMEKUWAPO. KINGINE HUKO KWENU KILAZA ANAPEWA KUONGOZA WATU NA AKILI ZAO KISA KATEULIWA NA MKUU AU KAPENDWA NA WAALIMU JE NI SAHIHI KUPATA RIGHT PERSON HAPO. HAMUWEZI FANYENI RESEARCH MJUE KAMA MKO SAHIHI. SISI TUPO NJE YA UWANJA TUNAWAONA NA TUNAJUA SHIDA ZENU HAMTAWEZA KWA NJIA HIZO.
mkuu hukutaka kusulutishwa asietaka kusulutishwa amejiajiri alafu ukubari kuwa jeshi mpaka ulaya na amerika lipo na mfumo wake ndio huo kama unaushauli peleka serikalini na sio JF hajasaidia kitu unazani jeshi kama jeshi unataka kila huduma yao iwe zaidi ya uraiani huku raia wakiishi maisha haya hali ya jeshi inategemea hali ya nchi kiuchumi.
 
Naongelea MENTALLY UPSTAIRS wala SIO MANGUVU YA MWILINI. ELEWA MADA KWANZA NDO UCHANGIE SIO KUKURUPUKA TU. Mnajaza seva bure!

Kama unadhani UPSTAIRS uko safi, then think again. Next time uje na hoja za msingi. Kama unadhani wanajeshi wana hawako safi vichwani mwao umepotoka sana. Na kama unadhani maguvu si sehemu muhimu ya jeshi, then ni heri ukatafute kibarua cha kubofya computer. Jeshini kuna wasomi weeengi sana tena wanafanya vizuri kuliko hata unavyodhani. Sasa watu waliopigika mitaani ndo mnakuja na mada za kupotosha namna hii.

Wakati unajidanganya na kudanganya watu kuhusu upstairs, jeshi lina mfumo wake wa kupima watu waliofit vichwani, tofauti na UDSM. Ndio maana si lazima mwenye 1st class akafaa jeshini. Na pale panapohitajika ujuzi ambao haupatikani jeshini, kuna raia kibao huajiliwa kutokana na nafasi zao. SI KILA ANAYEJIDHANI YUKO FIT UPSTAIRS ATAWEZA KAZI ZA KIJESHI. Acha kupotosha watu hapa, talk sense. Mambo ya kutaka kuwa treated kama special class of soldiers ni kutaka kuleta uraia jeshini. Standards MUST be maintained, thats all mjaza server.
 
Kaka elewa maada inazungumzia nini? Elimu bila ubunifu hamtaweza kitu. Najua wengi wenu hapa ni wanajeshi ndo maana mnatetea tu bila hata kuelewa.

Umepotosha mada, swala hapa ni vipaji maalum jeshini. Labda mtuambie mlikusudia umaalum gani hasa. Na hilo suala la elimu bila ubunifu halina mashiko, why? Nionyeshe bajeti ya ulinzi ya Tanzania. Usinyooshe kidole bila kuelewa tatizo liko wapi, na ndio mwisho wa siku mnabaki kujidanganya eti jeshini hakuna wasomi, what a shame.
 
Ukiangalia mfumo mzima wa ajira utabaini yafuatayo
1. Waalimu waliopo vyuoni 90% ni kikwazo kwa wasomi wengi wanaojiunga na jeshi hilo, akitokea mwanafunzi mwenye elimu kubwa hata Phd watafanya kila mbinu wamfukuze kwa kisingizio cha utovu wa nidhamu au watacomment kuwa kafeli.

2. Trainning zao hazija base kutafuta vipaji vya kweli katika nyanja muhimu kitaifa, kama vile madaktari, Eng, nk. Mfano Nyumbu mpaka leo wameshindwa kuifanya iwe ya kizalishaji toka enzi za mwalimu. Lugalo mpaka leo hawana hata blood bank sababu wanasayansi tiba hawapo ndio maana wanashindwa kukabiliana na migomo ya MH, sababu huko wengi 80% ni AMO na CO.

3. TMA ni kikwazo kikubwa sana katika kuwapata wasomi wazuri ndani ya jeshi hilo, elimu ya rasilimali watu kwa waalimu inawezekana ikawa ni issue. So they are trying to reduce the number of students kwa visingizio vya nidhamu ambayo ukifuatilia kiundani sio nidhamu as such but ni kutojua ubaya wakumfundisha mtu at certain level na kumwachisha mafunzo. HILO N BOMU BAADAYE.

4. Mazingira dhaifu kuwawezesha wenye vipaji kubuni kwa uhuru na kutumia taaluma zao, kufanya tafiti chanya maeneo yao ya kazi, mpaka leo hatujaziona.

5. Officer aliyetokea uraiani moja kwa moja I mean those who have got a little knowledge kuwa mkufunzi, atafundisha nini kama sio kupika majungu na kukosa comfidence?

Hayo machache yaliyobainishwa hapo juu ni chanzo kikubwa cha jeshi letu kuwa kama lilivyo hivi leo.

1. a.Je, ni macadet wangapi wenye elimu kubwa waliohitimu na wangapi waliofukuzwa?
b.Je, ni unadhani ni mamlaka gani inayohusika kufukuza cadet?

2. a.Je, jeshi linatengewa bajeti kiasi gani kwa ajili ya tafiti mbali mbali?
b.Je, ni yapi majukumu ya msingi ya jeshi letu? Je jeshi linayatekeleza? Ni yapi majukumu ya ziada?
c.Je, unadhani ratio ya AMO to MD (20:80) ni uwiano mbovu kiasi hicho?
d.Je, jeshi lina vikosi vingapi? Je, kuna vituo vingapi vya afya jeshini? Je unadhani madaktari wote ni vema wawe Lugalo kusubiri migomo?
e.Je, unadhani taifa limewahi kujitosheleza katika nyanja za wataalamu mbalimbali? (mf. madaktari)
f.Je unajua ni mara ngapi kikosi cha mainjinia wamejihusisha katika kuokoa maisha ya watanzania?

3. a.Je unadhani ni wakati muafaka sasa jeshi likaondoa mafunzo magumu yanayowaudhi wasomi wetu na kuweka aina ya mafunzo yatakayovutia wasomi wazuri zaidi jeshini?
b.Je, ungependekeza wakufunzi wa TMA wawe na level gani ya elimu?
c.Je, unaonaje kama jeshi litaachana na strict discipline na kuangalia zaidi elimu ya mtu?

4. Je, unadhani msingi mkuu wa jeshi lolote lile (hata kama ni insurgents) ni nini?

Ni hhayo u.
 
Mimi ninalikubali Jeshi la wananchi kwa operations zao, ila naona wengi hapa badala ya kuongea the real bottom fact wanateteea as if wao ni wasemaji wa jeshi
1.kama wasomi wa kweli wapo jeshini mbona mambo mengi sana wapo kimya tu mfano deni la taifa linazidi kukua siku baada ya siku.huwa wanapataga nafasi ya kuisaidia kuishauri serikali hata kidogo?? au mtasema ni siasa
2.mfano jeshi la marekani au hata S.Africa bajeti yao ipo wazi hapa TZ imekaaje
3.nimegundua mawazo mbadala hayakubaliki kwa Jeshini esp yale ambayo hawajazoea:Technology inahusika sana kubalini kataeni kwa maendeleo mazuri ya jeshi towards hyo Modern army
4.mimi ni raia tuu tena mwema ..haha ila siku jeshi likinihitaji nipo tayari kujitoa kwa ajili ya nchi yangu..
N.B punguzeni mashambulizi kwa mleta mada embu angalieni the other side of coin.
 
Mimi ninalikubali Jeshi la wananchi kwa operations zao, ila naona wengi hapa badala ya kuongea the real bottom fact wanateteea as if wao ni wasemaji wa jeshi
1.kama wasomi wa kweli wapo jeshini mbona mambo mengi sana wapo kimya tu mfano deni la taifa linazidi kukua siku baada ya siku.huwa wanapataga nafasi ya kuisaidia kuishauri serikali hata kidogo?? au mtasema ni siasa
2.mfano jeshi la marekani au hata S.Africa bajeti yao ipo wazi hapa TZ imekaaje
3.nimegundua mawazo mbadala hayakubaliki kwa Jeshini esp yale ambayo hawajazoea:Technology inahusika sana kubalini kataeni kwa maendeleo mazuri ya jeshi towards hyo Modern army
4.mimi ni raia tuu tena mwema ..haha ila siku jeshi likinihitaji nipo tayari kujitoa kwa ajili ya nchi yangu..
N.B punguzeni mashambulizi kwa mleta mada embu angalieni the other side of coin.

1. Kama mawazo yenyewe mnayoyaita real bottom fact ndo haya, basi ni bora mkae kimya. Next utauliza wabunge wanazuiwa kuhoji mambo mazito bungeni na jeshi limekaa kimya tu.

2. Ongea na mbunge wako

3. Mawazo mbadala ya kutaka jeshi lisimamie deni la taifa ni kweli hayajazoeleka jeshini na hayatazoeleka, samahani kwa hilo. Hata hiyo technolojia mnayoling'ang'ania jeshi labda ipo katika idara gani hapa Tz? Mbona mnataka kulifanya jeshi letu lionekane liko kwenye sayari nyingine yenye neema tofauti na Tz? Be realistic, msing'ang'anize mawazo yenu tu.

Na hao mnaowaita WASOMI WA KWELI hebu mnipe mfano wake basi. Ni kama akina nani basi nje ya jeshi? Mtoe na mtazamo wenu kama wakichukuliwa jeshini watalifanyia nini jeshi tofauti na kilichopo hivi sasa? Inaeleweka wengi humu licha ya kutokubali ukweli kuwa ni mambumbumbu wa utendaji wa jeshi, pia hata hawajui kiini cha matatizo ya nchi yetu. Na ndio sababu wanarukia kushambulia kila taasisi kumaliza hasira zao na haziishi.

Ndo hao hao utawasikia wakishangilia eti mwanajeshi kafa kwa ajali, " ooh ndo wakome, wanajidai sana hao, wanajiona wako juu ya sheria...." upuuzi mtupu. Wanadhani mtu anapokuwa mwanajeshi anakuwa saint, kwamba isolated incidents haziwezi kutokea. Kisha wanakuja hapa kujiita wasomi wa ukweli wenye mawazo mbadala. Ukiwauliza ni mawazo yapi hayo, watakwambia hatutaki jeshi la kutumia maguvu, tunataka jeshi la kisomi. Watakao pigana wakiwa mtandaoni. Hawajui hata core soldiering ni nini. WASOMI WA UKWELI. Eti jeshini hakuna wasomi wa ukweli. I hate this word.
 
Ukiwa jeshini inabidi uwe mtii na kupokea amri bila kuuliza wasomi siku zote ni wadadisi kabla ya kutii amri watajiuliza kama hiyo amri ni sahihi au la pia wasomi wasingefumbia macho ufisadi unaoendelea hapa nchini kama kuuza rasilimali za nchi na hayo wamejifunza toka jeshi la Nigeria ambalo lilikuwa likiajili wasomi matokeo yake kila mara nchi ikawa inapinduliwa
 
Mimi ninalikubali Jeshi la wananchi kwa operations zao, ila naona wengi hapa badala ya kuongea the real bottom fact wanateteea as if wao ni wasemaji wa jeshi
1.kama wasomi wa kweli wapo jeshini mbona mambo mengi sana wapo kimya tu mfano deni la taifa linazidi kukua siku baada ya siku.huwa wanapataga nafasi ya kuisaidia kuishauri serikali hata kidogo?? au mtasema ni siasa
2.mfano jeshi la marekani au hata S.Africa bajeti yao ipo wazi hapa TZ imekaaje
3.nimegundua mawazo mbadala hayakubaliki kwa Jeshini esp yale ambayo hawajazoea:Technology inahusika sana kubalini kataeni kwa maendeleo mazuri ya jeshi towards hyo Modern army
4.mimi ni raia tuu tena mwema ..haha ila siku jeshi likinihitaji nipo tayari kujitoa kwa ajili ya nchi yangu..
N.B punguzeni mashambulizi kwa mleta mada embu angalieni the other side of coin.

wasomi wa kweli hawapo kule jeshini ila huku uraini wapo sasa kipi kinachofanywa na wasomi wetu hawa wa kiraia huku uraiani mbona na wenyewe wamekaa kulalamika tu bila kusaidi chochote kama jeshi aliwajiri utaalam wenu peleka urain tunataka inchi ya viwanda magari ya undwe hapa si kukosoa tu.
 
Ukiwa jeshini inabidi uwe mtii na kupokea amri bila kuuliza wasomi siku zote ni wadadisi kabla ya kutii amri watajiuliza kama hiyo amri ni sahihi au la pia wasomi wasingefumbia macho ufisadi unaoendelea hapa nchini kama kuuza rasilimali za nchi na hayo wamejifunza toka jeshi la Nigeria ambalo lilikuwa likiajili wasomi matokeo yake kila mara nchi ikawa inapinduliwa

Kwa hiyo duniani jeshi la wasomi ni Nigeria tu? Poor logic, do your home work. Hujui unachokiongelea na huo usomi wako haujakusaidia. You are a problem.
 
wasomi wa kweli hawapo kule jeshini ila huku uraini wapo sasa kipi kinachofanywa na wasomi wetu hawa wa kiraia huku uraiani mbona na wenyewe wamekaa kulalamika tu bila kusaidi chochote kama jeshi aliwajiri utaalam wenu peleka urain tunataka inchi ya viwanda magari ya undwe hapa si kukosoa tu.

Mkuu hawa wala si wasomi bali ni opportunists. Ukiwapa nafasi wanawazia kupiga hela tu. Hakuna hoja ya kisomi hapa zaidi ya kwamba wengi humu ni mbumbumbu wa mfumo wa majeshi. Eti wasomi wanaogopwa kwamba watahoji ufisadi na madeni makubwa. Msomi wa kweli angeangalia mumo wa serikali na vyombo vyake vya ulinzi halafu akaja na logical deductions wala si hoja za kitoto namna hii. WASOMI WA UKWELI? Aibu kubwa.
 
Kwa hiyo duniani jeshi la wasomi ni Nigeria tu? Poor logic, do your home work. Hujui unachokiongelea na huo usomi wako haujakusaidia. You are a problem.
wewe ndio unatakiwa ufanye homework kumbuka hapa tunaongelea jeshi la jwtz ndio maana nimechukulia mfano wa Nigeria ambao majeshi yao yamejaa wasomi ila kuna majeshi kama ya USA,CHINA,ISRAEL hata SOUTH AFRICA ambayo yamejaza wasomi na hata kiteknologia wako mbali usiwe unakurupuka soma uelewe
 
Asante Nyenyere,

Kama maandishi hayatoshi, picha imefunga kazi! Tatizo la wasomi vijana la kujiona bora kuliko wengine haliko jeshini tu! Hata uraiani ni hivyo! Maofisini ndo kabisa, na bahati mbaya huko wanadekezwa. Pelekeni hoja Serikalini, vijana wote wasomi waende jeshi miezi 4 kabla ya kupata ajira si serikalini tu bali hata Makampuni binafsi.

Kweli mkuu umenena vema.
 
wewe ndio unatakiwa ufanye homework kumbuka hapa tunaongelea jeshi la jwtz ndio maana nimechukulia mfano wa Nigeria ambao majeshi yao yamejaa wasomi ila kuna majeshi kama ya USA,CHINA,ISRAEL hata SOUTH AFRICA ambayo yamejaza wasomi na hata kiteknologia wako mbali usiwe unakurupuka soma uelewe

Haya nyie makanjanja mmelifanyia nini taifa? Au mpaka mpatb nafasi jeshini. Acheni upuuzi wenu, jeshi linao wasomi wengi tu. Habari za kuwaza mapinduzi ni akili zilizo choka. Wakati Foday Sanko anapindua aliongoza wasomi wangapi? Vipi kuhusu Samwel Doe? Mnadhani jeshini kila mmoja lazima awe na digrii? Mmeshindwa kushindana kwenye soko la ajira EA mmegeukia jeshi ambako hamkidhi vigezo, kisha mnaleta hoja za kutaka jeshi liendeshwe kiraia? Wacheni huo uzandiki. Kama kweli mnawazia mapinduzi, basi mmechoka vibaya.
 
Back
Top Bottom