Kaa Mbali Na Watu Ambao ni Sumu Kwako

Kaa Mbali Na Watu Ambao ni Sumu Kwako

Etugrul Bey

JF-Expert Member
Joined
Aug 6, 2020
Posts
6,514
Reaction score
15,247
Screenshot_20241125_164615_Quora.jpg


Kuna watu ambao hakika ni sumu katika maisha yetu na wanatuua kidogo kidogo bila wenyewe kujua,wanaweza kuwa ni wazazi,ndugu zetu,waume na wake zetu,wafanyakazi wenzetu na watu ambao tunakutana nao kila siku katika maisha yetu

Watu hawa watanyonya nguvu yako,na kukuacha hoi bini taabani,watapandikiza nguvu hasi katika maisha yako kwa matusi,kejeli,dharau,na kukukandamiza kwa kila namna,utajikuta unakufa pole pole bila kujijua.

Watakufanya upoteze thamani yako,raha yao kukuona unakuwa mtu na mwenye kukosa hadhi mbele za watu na jamii kwa ujumla,hawakawii kukutungia habar za uwongo ili mradi hadhi yako na heshima yako ipotee,kuwa makini sana

Screenshot_20241125_171952_Chrome.jpg

Wapo tayar kuhakikisha haufanikiwi katika maisha yako ya utafutaji,wakiwa nawe wanajifanya ni watu wema kwako lkn kiuhalisia wanakutakia mabaya katika maisha yako.

Kumbuka upweke ni wa mpito tu ni bora uwe mpweke kwa mda fulani kuliko kuwa karibu na watu hawa,kwani hathari ya kuwa na watu hawa maishani mwako ina madhara ya mda mrefu sana

Ni hayo tu!
 
Kuonyesha wazazi pia wanaweza kuwa toxic sikia hii,binti mmoja wa miaka 16 alilazimishwa na mama yake mzazi acheze filamu za watu wazima kwa ajili ya pesa

Na binti huyo huyo ambaye mwenye asili ya uheshia na uhairishi,basi akiwa na umri wa miaka 12 tu,mama yake alitaka afanyiwe operesheni ya macho ili awe na macho makubwa kama yakimarekani,huyu ni mzazi toxic sana kwa mwanawe

Mifano ipo mingi sana katika jamii zetu,tusiwe sumu katika jamii yetu
 
Kuonyesha wazazi pia wanaweza kuwa toxic sikia hii,binti mmoja wa miaka 16 alilazimishwa na mama yake mzazi acheze filamu za watu wazima kwa ajili ya pesa

Na binti huyo huyo ambaye mwenye asili ya uheshia na uhairishi,basi akiwa na umri wa miaka 12 tu,mama yake alitaka afanyiwe operesheni ya macho ili awe na macho makubwa kama yakimarekani,huyu ni mzazi toxic sana kwa mwanawe

Mifano ipo mingi sana katika jamii zetu,tusiwe sumu katika jamii yetu
Mzazi ananilazimisha kwenda kanisani.

Hiyo sio kuingilia uhuru?
 
Halafu hawo watu sumu walio katika maisha ya watu,muhusika unakuja kuwajuwa muda umeenda na mambo mengi yamekwenda mrama.
Kweli kabisa boss na unakuta uharibifu mkubwa umepatikana

Kuna binti mmoja ilibidi atoroke nyumbani akiwa na miaka 16 tu,anasema alikuwa na wazazi toxic sana kiasi kwamba hujui nini kitatokea kesho yake

Anasema sasa hivi ni mtu mzima lkn karibia ujana wake wote alipitia kupata ushauri wa kisaikolojia,maana aliathirika sana

Huku Afrika hatuna washauri kama hawa ambao wanaweza kumfanya mtu akakaa sawa,kilochabaki ni kujinyonga au kuwa na sonona maisha yako yote
 
Back
Top Bottom