Kababaye Mwanaume ndiii

Bob Dylan

JF-Expert Member
Joined
Dec 28, 2011
Posts
208
Reaction score
222
Wakazi wa arusha hivi mnamkumbuka mwanamazingaumbwe aliekua anaitwa kababaye miaka ya nyuma?

Nakumbuka miaka ya nyuma alivuma sana mashuleni kiingilio ilikuaga mia mbili.

Akitaka kufanya mauza uza anasema kababaye mnaitikia yee, anasema mwanaume ndi mnaitikia ndii, mwanaume ndaa, ndaaa.

Kwa anae mkumbuka atueleze yupo wapi sikuhizi.
 
Enzi izo kababaye akiii nmekumbuka mbali Mia mia zetu alizila sana
 
Na macho nirembuerembu,rembua alikuwa akikalia misumari.nilisikia alikufa.
 
Alikuwa na wimbo wake...kababa kimunyi munyi...mnaitikia zembwelaa...kababa kimunyi munyi zembwelaaa
 
Alikuwa anaishi Moshi-Soweto. Anatembea na Kinyani.....

Alishafariki long time sana
 
Halafu kulikuwa na power shinyanga akijiita black mamba.
 
Mi namkumba Hamishi Nyaloo yule kichaa hatari sana, alitusumbua sana Arusha enzi hizo,ukisikia Hamisi nyalooo hugeuki ni mbio balaa.
 
hahahahahah h unanikumbusha mpembenue wilaya ya temeke miaka ya miakam karibu na 2000
 
Du mmenikumbusha mbali kababayee na misumari dah
 
Kwa mbwembwe anachezesha kifua na kuzungusha tumbo kuajabu.staili alizoniachia mpaka leo.sema kitambi kinaniharibia.kababa ye,watu yeeeeeeh.kababa meng'enyu,meng'enyula,kababa nirembue rembu watu rembua.looong time majengo kwa mtei.asante mtoa mada
 
Wachangiaji wote mmenifanya nicheke kiaina. Hawa watu walikuwa wanazalisha ndege toka kwenye vitambaa. Mi nimecheka mpaka nalia wiiii.
 
Hawa jamaa enzi hizo walikua wanatusisimua mbaya. Ilikua ni ngumu kukosa shoo zao. Huku mazingaombwe!! Kule sarakasi! dah! Yaani wote sijui wamepotelea wapi wale! walishindwa kabisa hata kuwarithisha watu wao wa karibu?
Watoto wa sasa wa kizazi cha utandawazi wamekosa mambo mazuri yale aisee.
 
Halafu kulikuwa na mtu akiitwa maasia mote anaambatana na mtu akiitwa juju ye.akianza mambo yake anasema ni yeye juju ye,watu ye.ghafla mshikaji akaharisha lundo la sarafu zimejaa sufuria ndogo ndogo.dah wakati huo bwana.
 


Mnaimba Kababa Nibebe............. Kababa nibebeee............... MAWENZI PR SCHOOL
 
Kababayee yupo mwaka jana nilikua namuona na jamaa mmoja wa uganda tulikutana nairobi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…