Kabla wabantu hatujaingia Tanzania, inaonekana nchi ilijaa mbilikimo

Kabla wabantu hatujaingia Tanzania, inaonekana nchi ilijaa mbilikimo

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Wengi tukisikia mbilikimo huwa tunawaza wale wa misitu ya Congo, lakini historia inaonyesha kusini yote ya Africa, yaani kuanzia misitu ya Congo, kuja Uganda, Kenya kidogo, Tanzania yote hadi Africa kusini kulijaa mbilikimo na Wasan (Wabushemen). Wabantu walipokuja wakachanganyana na mbilikimo na kutuzaa sisi watu wa eneo la kusini mwa Africa.

Kitabu cha historia ya Wagogo kinaonyesha kuwa kabla ya Wagogo, nchi ya Ugogo ilikaliwa na mbilikimo walioitwa Wagomvia. Kitabu kingine kuhusu asili ya Wachagga kinasema kuwa kabla ya Wachagga, miteremko ya Kilimanjaro ilikaliwa na mbilikimo walioitwa Wakonongo. Inaonekana mbilikimo hawa wawindaji walitapakaa nchi yetu hii yote.

Watanzania na watu wengi wa kusini mwa Africa si Wabantu halisi. Tu wabantu na mbilikimo.
 
Kuna nyuz kadhaa humu jamaa wakishangazwa na ufupi wa watz

Kuna takwimu zinasema asilimia 70 ya wabongo ni wafupi
Sababu kubwa ni hiyo. Wengi tu machotara wa wabantu na mbilikimo. Nahisi mbilikimo wa Milimani milimani kama Wakinga na Waluguru hawakufikwa na Wabantu kwa wingi ndiyo maana wengi wao wafupi.
 
Back
Top Bottom