Kabla ya Kumchagua Mwenyekiti CHADEMA Wafanye Uamuzi Huu Kwanza

Kabla ya Kumchagua Mwenyekiti CHADEMA Wafanye Uamuzi Huu Kwanza

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
Na. M. M. Mwanakijiji

Hakuna jinsi. Kinachotokea CHADEMA ni matokeo tu..

Nashauri wafanye uamuzi kuwa atakaye peperusha bendera ya mgombea wa Urais HATOKUWA Mwenyekiti wa chama na kuwa Mwenyekiti wa chama hatokuwa mgombea Urais au Ubunge. Jukumu lake liwe kwenye chama.

Wakati wa kampeni za uchaguzi atakayetangazwa kuwa mgombea wa Urais anakuwa mara moja kuwa ndiyo kiongozi mkuu wa chama hadi baada ya uchaguzi. Mgombea wa Urais kimadaraka anakuwa juu ya Mwenyekiti wa chama.

Faida za hili ni rahisi kuziona. Kubwa ni itaondoa mvutano wa madaraka. Maaana yake ni kuwa wamuombe mtu ambaye anaweza kweli kupeperusha bendera ya ugombea ili awavushe bila mtu huyo kuutaka uenyekiti wa chama.
 
Na. M. M. Mwanakijiji

....Wakati wa kampeni za uchaguzi atakayetangazwa kuwa mgombea wa Urais anakuwa mara moja kuwa ndiyo kiongozi mkuu wa chama hadi baada ya uchaguzi. Mgombea wa Urais kimadaraka anakuwa juu ya Mwenyekiti wa chama....
Mkuu Mwanakijiji
Ninapenda kutofautiana nawe kwenye hili. Kumfanya mgombea urais ama rais kuwa na madaraka ya juu ndani ya chama ni sawa na kurithi usultani wa CCM ambapo rais hawajibiki wala kuwajibishwa na chama. Rais lazima awe obedient kwa chama ili kuchechemiza uwajibikaji....


Labda kama una ufafanuzi wa kina kwenye hili
 
Mkuu Mwanakijiji
Ninapenda kutofautiana nawe kwenye hili. Kumfanya mgombea urais ama rais kuwa na madaraka ya juu ndani ya chama ni sawa na kurithi usultani wa CCM ambapo rais hawajibiki wala kuwajibishwa na chama. Rais lazima awe obedient kwa chama ili kuchechemiza uwajibikaji....


Labda kama una ufafanuzi wa kina kwenye hili
Haina maana anakuwa na madaraka ya utawala wa chama. Ni kuwa agenda ya mgombea inakuwa agenda ya Chama. Siyo mfumo wa sasa ambapo chama kinaandaa agenda halafu mgombea anaifuata.
 
Nyie chama cha mbogamboga mna kubwa zuri la kujifunza kutoka CDM... Embu ona CDM ilivyo ruhusu democracy ichukue nafasi yake ktk kugombea nafasi mbalimbali ndani ya chama... Nyie mbogamboga siku mtakayo ruhusu nafas ya m'kiti igombewe naapa mbele za Mungu mtachinjana mtauana mtapigana na kurogana mchana kweupe na mwisho wa siku ndio itakuwa kufa kwa chama.
CDM ikimaliza uchaguz wao wa ndani nawaambia CDM itakuwa imeimarika ×100 zaidi kuliko mnavyodhani.
 
Chadema wamejenga utaratibu wa fisi.

Yaani wanasubiria mkono wa CCM udondoke.

Wale wasioridhika na mchakato CCM huwa wanawabeba.
Unawaona wanaowapigania Mbowe na Lissu? Wengi wanapigania nafasi za kugombea Ubunge, udiwani, viti maalum nk. Halafu baada ya haya yoye watakatwa watu CCM watakimbilia CHADEMA na kupokelewa kwa furaha...
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Hakuna jinsi. Kinachotokea CHADEMA ni matokeo tu..

Nashauri wafanye uamuzi kuwa atakaye peperusha bendera ya mgombea wa Urais HATOKUWA Mwenyekiti wa chama na kuwa Mwenyekiti wa chama hatokuwa mgombea Urais au Ubunge. Jukumu lake liwe kwenye chama.

Wakati wa kampeni za uchaguzi atakayetangazwa kuwa mgombea wa Urais anakuwa mara moja kuwa ndiyo kiongozi mkuu wa chama hadi baada ya uchaguzi. Mgombea wa Urais kimadaraka anakuwa juu ya Mwenyekiti wa chama.

Faida za hili ni rahisi kuziona. Kubwa ni itaondoa mvutano wa madaraka. Maaana yake ni kuwa wamuombe mtu ambaye anaweza kweli kupeperusha bendera ya ugombea ili awavushe bila mtu huyo kuutaka uenyekiti wa chama.
Mgombea wa Urais atakuwaje juu ya Mwenyekiti wa Chama? Huo ni mfumo wa Marekani ambako mgombea ndie anahesabika kuwa kiongozi wa chama. Mfumo watu wa supremacy ya chama, Mwenyekiti wa Chama Tawala ana nguvu sawa au hata zaidi ya Rais. Tunakumbuka ilivyokuwa wakati wa Mwalimu na Mwinyi. Wote tunajua nani ndie alikuwa mwenye nguvu. Rais atakuwa ana mamlaka zaidi pale tu nafasi za kiutawala hazitaunganishwa na chama. As long as mgombea wa urais atakuwa anachaguliwa na chama Mwenyekiti wake atakuwa na nguvu juu yake. Kuepuka hili ndio maana CCM wakaanzisha utamaduni wa kuviunganisha vyeo hivi.

Amandla...
 
Binafsi sijali nani ni Mwenyekiti...
Hapo ndipo unapokosea. Nguvu za chama cha upinzani ni wabunge wake. Katika mazingira yetu hamna namna chama tawala kitakubali mgombea wa upinzani. Upinzani ukiwa na wabunge wa kutosha watapata nafasi ya kuisamamia serikali na hivyo kuonyesha umahiri wao na tofauti yao na chama tawala. Wakina Lissu, Halima, Heche, Suzan , wakina Esther walijijengea sifa sana kwa namna walivyokuwa wakipigania maslahi ya wananchi wakiwa Bungeni. Wakiwemo wa kutosha wataweza hata kulazimisha suala la Katiba Mpya lifanyiwe kazi. Mwenyekiti wa Chama ana nafasi kubwa ya kutambua watu wanaoweza kukiwakilisha vyema chama Bungeni. Si mti wa kudharauliwa.

Amandla...
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Hakuna jinsi. Kinachotokea CHADEMA ni matokeo tu..

Nashauri wafanye uamuzi kuwa atakaye peperusha bendera ya mgombea wa Urais HATOKUWA Mwenyekiti wa chama na kuwa Mwenyekiti wa chama hatokuwa mgombea Urais au Ubunge. Jukumu lake liwe kwenye chama.
Kwanini sasa?

Ni kwa sababu ya Tundu Lissu tu dhidi ya Freeman Mbowe?

Kwani huyu Mbowe ana nini alichobeba cha CCM kiasi cha kuja na mapendekezo haya?

Sababu ya maswali hayo ☝🏻☝🏻ni kuona kuwa watu tuliodhania siku zote ni wapigania mageuzi na mabadiliko ya kisiasa na mfumo wa utawala wa nchi hii kina Freeman Mbowe, Ansbert Ngurumo, wewe Mzee Mwanakijiji na wengine kibao kumbe siyo kabisa...

It's obvious kuwa mapendekezo yako haya ni kwa ajili ya kutafuta kila possibility ya aidha Freeman Mbowe au mtu ambaye mfumo umemwandaa toka CCM kuja kugombea u - Rais CHADEMA ili mradi Tundu Lissu asipate kabisa fursa hiyo iwapo atakuwa mwenyekiti wa CHADEMA (possibility yake mpaka sasa ni zaidi ya 80%)
Wakati wa kampeni za uchaguzi atakayetangazwa kuwa mgombea wa Urais anakuwa mara moja kuwa ndiyo kiongozi mkuu wa chama hadi baada ya uchaguzi.
Huu ni utaratibu wa wapi aisee..?

Yaani mgombea tu wa u - Rais, akipata nafasi hiyo, basi mwenyekiti aliyepo kikatiba anaacha kuwa mwenyekiti badala yake aserende uenyekiti wake kwa huyu mgombea..?

Unasema "hadi baada ya uchaguzi". Halafu baada ya hapo? Una maana akiwa ameshinda ndiyo yeye anakuwa Mwenyekiti wa chama ? Vipi huyu aliyechaguliwa kikatiba? Yeye aende wapi? Na vipi akiwa ameshindwa?
Mgombea wa Urais kimadaraka anakuwa juu ya Mwenyekiti wa chama.
Huko mliko USA na Ulaya ndivyo wanavyoendesha vyama vyao?
Faida za hili ni rahisi kuziona. Kubwa ni itaondoa mvutano wa madaraka. Maaana yake ni kuwa wamuombe mtu ambaye anaweza kweli kupeperusha bendera ya ugombea ili awavushe bila mtu huyo kuutaka uenyekiti wa chama.
Yupo Tundu Lissu...

Kamwe hawezi kuwa Freeman Mbowe....

Kamwe hawezi kuwa kapi lolote toka CCM...

CHADEMA wakirudia makosa yao ya mwaka 2015, nitawadharau na kuwafuta kabisa ktk kumbukumbu zangu...

NOTE:
1. All in all, pendekezo lako hili lina ishara zote muhimu kuwa Freeman Mbowe (anayehaha sasa kuokoa uenyekiti wake) alishaandaa mtu wake aliyepewa na Bi Samia Suluhu Hassan mwenyekiti wa CCM aje CHADEMA kugombea u - Rais..

2. Hai make sense yoyote wewe Mzee Mwanakijiji (tunayedhani unaheshimika hapa jukwaani) kuja na ushauri na pendekezo hili la ajabu kabisa..

3. We all know and understand that, mission ya haya yote ni kuhakikisha Tundu Lissu hawi mwenyekiti CHADEMA. Hili mmeshaliona kama vile linakwenda kufeli na likely kuwa limeshafeli. Na kwa kuwa uwezekano wa huyu asiyetakiwa na mfumo wa ma - CCM a.k.a "WASIOJULIKANA" kuwa kiongozi wa CHADEMA, unaelekea kufeli, umetumwa kuchokoza kwa kuleta plan C (plan A & B zote kwa mpigo ziligonga mwamba), ili kuhakikisha huyu Bwana Tundu Lissu hashindani na mama yenu a.k.a Chura Kiziwi, kwenye uchaguzi mkuu wa u - Rais mwaka huu 2025 kama utakuwepo...

Pole sana.....
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Hakuna jinsi. Kinachotokea CHADEMA ni matokeo tu..

Nashauri wafanye uamuzi kuwa atakaye peperusha bendera ya mgombea wa Urais HATOKUWA Mwenyekiti wa chama na kuwa Mwenyekiti wa chama hatokuwa mgombea Urais au Ubunge. Jukumu lake liwe kwenye chama.

Wakati wa kampeni za uchaguzi atakayetangazwa kuwa mgombea wa Urais anakuwa mara moja kuwa ndiyo kiongozi mkuu wa chama hadi baada ya uchaguzi. Mgombea wa Urais kimadaraka anakuwa juu ya Mwenyekiti wa chama.

Faida za hili ni rahisi kuziona. Kubwa ni itaondoa mvutano wa madaraka. Maaana yake ni kuwa wamuombe mtu ambaye anaweza kweli kupeperusha bendera ya ugombea ili awavushe bila mtu huyo kuutaka uenyekiti wa chama.
Mkuu Mzee Mwanakijiji , nimeipenda hii!, hii ni prediction ya matokeo ya uchaguzi mwenyekiti wa Chadema kuwa Mbowe atachaguliwa mwenyekiti, ili Lissu ndie awe mgombea urais wa Chadema 2025!.
Hata hivyo siungi mkono hoja yako hii kwasababu ni hoja ya kibaguzi inayokwenda kinyume cha ibara ya 12, 13, na 21 ya katiba ya JMT.
1737240701042.png

1737240851505.png

Ushauri wa maana kwa Chadema, ungewashauri, hata ikitokea Mbowe akashinda uenyekiti, ugombea urais wa Chadema uende kwa mtu mwenye uwezo wa kumshinda mgombea wa CCM wa 2025, kwa kuwaambia wazi kabisa bila kupepesa macho wala kumungunya maneno, Mbowe yeye hana uwezo huo!, na mtu pekee mwenye uwezo huo kwa Chadema, licha ya mapungufu yake ya kuwa ni ropo ropo, ni Tundu Lissu pekee!, na kitakachomfanya Tundu Lissu amshinde mgombea wa CCM, ndio huo u ropo ropo wake! kama nilivyoshauri hapa Japo Lowassa Alikuwa a Liability CCM, Akawa Asset Chadema. Lissu is a Very Bad Liability, but is The Only Asset Chadema Has Kuwangiza Ikulu!. Je... ?
P
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Hakuna jinsi. Kinachotokea CHADEMA ni matokeo tu..

Nashauri wafanye uamuzi kuwa atakaye peperusha bendera ya mgombea wa Urais HATOKUWA Mwenyekiti wa chama na kuwa Mwenyekiti wa chama hatokuwa mgombea Urais au Ubunge. Jukumu lake liwe kwenye chama.

Wakati wa kampeni za uchaguzi atakayetangazwa kuwa mgombea wa Urais anakuwa mara moja kuwa ndiyo kiongozi mkuu wa chama hadi baada ya uchaguzi. Mgombea wa Urais kimadaraka anakuwa juu ya Mwenyekiti wa chama.

Faida za hili ni rahisi kuziona. Kubwa ni itaondoa mvutano wa madaraka. Maaana yake ni kuwa wamuombe mtu ambaye anaweza kweli kupeperusha bendera ya ugombea ili awavushe bila mtu huyo kuutaka uenyekiti wa chama.
Mawazo yako yafanyiwa kazi baada ya uchaguzi mkuu,
 
Chama cha siasa ni taasisi (organisation).

Organisation (yeyote) ina malengo (goals and aim) iwe ya biashashara, chama siasa au Charity/NGO/Quasi-Quango.

Aim and objectives za taasisi zina tengeneza strategy ya kufikia malengo
(tunaita ilani kwenye siasa). Vyama vya kijamaa na ubepari vinatamaduni tofauti ya kuandaa ilani.

Watekelezaji wa strategy ni senior civil servant, na wapangaji ni senior management (or dedicated teams) vyama vya siasa. Either way the process is top down approach.

Mawaziri wanasimamia ilani (intervene, how best) ilani yao ifanikiwe au kusimamia kuona civil servants wanafanya kazi sahihi (kuna strategic monitoring measures kupima performance, trouble shooting, risk mitigation planning and so forth).

Raisi ana mandate ya juu kwenye kutekekeza plan ya chama ndio chief executive serikalini na ndani ya chama kwa sababu ndie anaesimamia ilani ilani (mission, goals, objectives and strategy).

Sasa mtu akishakuwa raisi anawezaje kuwa na mwingine wa kumpangia (labda vyama vya siasa viwe na managent board) inayotambulika kwenye katiba ya Tanzania, that’s the only way chama cha siasa kinaweza kum-control raisi.

Kama utasoma kwa makini, utaona upuuzi wa mapendekezo yako.

Kuna wasaa inabidi muambiwe ukweli; you can’t just write things from your heads. Lazima mjue kwanza how things work. Before you write nonsense which doesn’t make sense.

I don’t care about people feelings at times, it’s tiring reading nonsense too.
 
Back
Top Bottom