Kachero asimulia alivyowatorosha Nyerere, Kawawa

TISS walioshindwa zuia Twiga kupanda ndege
 
Hata marekani hawezi kuvamia Tanzania. Lazima watafute msaliti ndio wafanye hivyoo mkuu. We are strong.
 
Ulitegemea kitoke tu ?

Andika chako
 
Shukran sana ngoja takitafuta nikisome nione kama kipo sawa na habari niliambiwa na wazee wangu walioshatangulia mbele ya haki.

Kwenye story za chai na kahawa...uongo mtupu
 
ndio maana kimefanyiwa editing kaka, inawezekana hizo njia za underground bado zipo na zinatumika mpaka sasa ila wakaamua kusingizia pantoni la watu maskini


Kinacho shangaza zaidi - hivi inaingia akilini kwamba aliwapeleka viongozi hao wawili kwenye kivuko bila ya kuficha sura zao! Aliwamini vipi waendesha pantoon? Story ambayo haijakuwa watered down inaonekana wazi wazi - simulizi ya kuondoka Ikulu kwenda Kivukoni kwa hali ilivyo kuwa wakati huo, hapo naona hajafunguka vizuri.

Mataifa ya wenzetu kuna sheria inayo sema ikisha pita miaka thelathini waajiliwa wa vitengo nyeti including wanajeshi wanaruhusiwa kuandika/simulia operation zote za siri zilizo wahi kufanywa na Serikali yao ndani na nje ya nchi yao, je, hapa kwetu hilo alipo?
 
Hiki kitabu lazima nikinunue kwa gharama yoyote ile. Jamani wazee wetu andikeni vitabu kuitunza historia, big up Mr. Bwimbo kumbe alikuwa TISS niliso madarasa mojana mtoto wake mmoja wa kike na shuke moja na ndugu zake wengine na ndio nyumba za kwanza au ya pili kuona tiles maeneo yaKurasini na nilizipenda toka siku hiyo! Ila jamani those old good days, kulikuwa hamna ubishororo wa siku hizi, haijalishi umetoka class gani we were friends ( yaani na watoto tuliosoma) wazazi walikuwa loving kwa yeyote atakaeenda nyumbani kwa mwenzie!
 
Hiyo story ya kwanza tu inaonesha porojo.

Nadhani kitabu kilingoja waliomtorosha kweli waage dunia.
 
Leo hujawataja wale watani zako mkuu!!!
Mkuu hiki kitabu kimekuja wakati muafaka kabisa kwani kimesheheni shule ya kutosha kwa wale majamaa zetu wa kuzungusha mikono, mfano mzuri ni ukurasa wa 55 wa kitabu hicho ambacho , mwandishi ameelezea namna ambavyo mwalimu nyerere aliamua kujipunguzia mshahara wake ambao alikua akilipwa kipindi hicho shilingi lefu sita za kitanzania (6,000) hapo utaona kwamba kelele za hao ndugu hazina mashiko kwani Magu sio rais wa kwanza Tanzania kujipunguzia mshahara, ilishafanyika kabla.

Jambo la pili na la busara ni hao ndugu wanapopiga kelele kua magu anatumbua hadharani watu bila kuzingatia haki za binadamu, mwandishi anawajibu kwa kutoa simulizi ya namna ambavyo baba wa Taifa hili alikua akitumbua watu hadharani, mfano wa hilo ni pale ambapo mama mmoja alimfuata rais na kumlilia kwamba hakimu amempa haki mwizi wa mali zake, kwa kua huyo mama alishindwa kuleta kumbukumbu zake sahihi, Mwalimu alimwita huyo hakimu na kumuuliza maswali kwanini amemnyima huyo mama haki yake akamtumbua pale pale.

Ukijaribu kufuatilia simulizi katika kitabu hicho na ukilinganisha na makelele ya hao jamaa zetu utaona kwamba hawana elimu ya historia ya taifa hili na wanapotosha watu kwa maslahi yao binafsi. Hayo ni machache tu katika mengi niliyoyapata katika kitabu hicho.
 
ndio maana kimefanyiwa editing kaka, inawezekana hizo njia za underground bado zipo na zinatumika mpaka sasa ila wakaamua kusingizia pantoni la watu maskini
Halafu umewaza mbali sana. Inawezekana kabisa ikawa hivyo. Maana haiingii akili kwa mtu aliyekuwa akiwindwa na wanajeshi akatoroka kirahisi tu kwa kutumia pantoni.
 
Kitabu kizuri. Safi sana ni cha kutafuta. Please kama kina uwezo wa kuuzwa online au kifikishwe kaskazini, tuambiwe.

Namna historia tutaijua vizuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…