Kadiri siku zinavyokwenda Seminari za Kanisa Katoliki zinabaki kuwa kwa ajili ya watoto wa matajiri na wenye vipato vikubwa.

Kadiri siku zinavyokwenda Seminari za Kanisa Katoliki zinabaki kuwa kwa ajili ya watoto wa matajiri na wenye vipato vikubwa.

This is...

JF-Expert Member
Joined
Dec 28, 2014
Posts
5,050
Reaction score
5,204
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu.

Seminari hizi za kikatoliki hawana habari na mtoto wa maskini.

Nilimpeleka mtoto wa ndugu yangu aliyesoma shule za serikali kufanya interview kwa ajili ya kujiunga na kidato cha kwanza.

Nilipomfikisha pale seminari nilikutana na mdau na ni mtu wa kanisa/kasisi ambaye nilisoma nae chuo kikuu akiwa mwalimu pale.

Katika maongezi akaniambia kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne kila darasa lina wanafunzi 110 na ktk wote hao watoto waliosoma Kayumba hawazidi kumi.

Wanachukua watoto wa English Meadium na hizi zinzoitwa Academy.

Na baada ya kufuatilia baadae niligundua kwamba kwa mwaka huu 2024 ambao ndiyo kijana alipaswa kujiunga form one walichukua kijana mmoja tu kutoka kayumba.

Si kwamba hawa vijana hawana uwezo kitaaluma la hasha.

Mdau yule nilimdodosa na kumuuliza kwa nini kupotezea watu muda na rasilimali bila sababu.UKIZINGATIA mchakato wa usaili unaanzia Parokia anayotoka kijana. Pia wanafanya usaili kwenye vikarieti written na oral mara mbili na baada ya hapo ndipo wanaitwa kwenye seminari husika kwa usaili tena na kote huko unalipia.

Jibu alilonipa ni kwamba wanataka wazazi wenye uwezo wa kulipa ada kwa uhakika. Kuchangia harambee mbalimbali zinazoitishwa na mambo mengine mengi.

Kigezo kingine umahiri ktk kuzungumza kiingereza.(Hili nilishangaa kidogo sababu najua kabisa kuongea kiingeeza kunarahisisha ufundishaji lakin kujua kiingereza si kigezo cha uwezo wa kiakili wa mtoto.) Ni vitu viwili tofauti.

Hivyo inaonyesha kadiri miaka inavyosogea hata katika imani tutajikuta tunaongozwa na makasisi kutoka familia za kitajiri na maskini hana chake hata ktk kanisa.

Seminari ninayoizungumzia iko moshi marangu mlimani huko. Ni maarufu sana. Japo siku hizi haivumi sana kama zamani katika rank za kitaifa.
 
Wewe Mtoto wako alifeli mtihani wa kujiunga na seminari .
Ili uthibitishe kwamba alifaulu ila kwa kuwa alisoma kanumba akafelishwa.
Seminari kwenye usaili wao hawaulizi mtoto anasoma shule gani?
Ni hivi mtoto anaweza kuwa darasa la sita kama yupo vizuri akienda kupiga pepa ya usaili seminari akafaulu akachaguliwa.
Mitihani ya kujiunga na seminari nyingi inafanyika kabla ya kufanya mitihani ya drs la Saba.
Seminari wanachojali ni nidhamu na akili ya darasani ingekuwa wanajali sana fedha wasingekuwa wanachuja na kuwafukuza wanaofeli.
Na huyo mdau wako uliyemuuliza atakuwa amekudanganya eti kila darasa lina wanafunzi 110 (form one hadi form four).
Yaani seminari form One waanze 110 wafike form four 110.
Sio kweli mimi nilisoma seminari tulianza form One 48 tukamaliza form four 31 kuna wengine walifeli wakafukuzwa wengine walifukuzwa kwa utovu wa nidhamu
Embu tuwekee hapa matokeo ya mtihani wa kujiunga na seminari aliyofanya moto wako.
Na pia sio kweli kwamba kila mtoto anayesoma kanumba mzazi wake hatakuwa na uwezo wa kulipa ada na michango ya huko seminari
Mitihani inafanywa kwa namba na Matokeo yanabandikwa jimboni hadi Kwenye maparokia. Na cut point inatajwa
Tatizo ni shule zetu za kanumba elimu ya huko ni duni sana angalia hata Kwenye mitihani ya kitaifa nyingi zinafanya vibaya
 
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu.

Seminari hizi za kikatoliki hawana habari na mtoto wa maskini.

Nilimpeleka mtoto wa ndugu yangu aliyesoma shule za serikali kufanya interview kwa ajili ya kujiunga na kidato cha kwanza.

Nilipomfikisha pale seminari nilikutana na mdau na ni mtu wa kanisa/kasisi ambaye nilisoma nae chuo kikuu akiwa mwalimu pale.

Katika maongezi akaniambia kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne kila darasa lina wanafunzi 110 na ktk wote hao watoto waliosoma Kayumba hawazidi kumi.

Wanachukua watoto wa English Meadium na hizi zinzoitwa Academy.

Na baada ya kufuatilia baadae niligundua kwamba kwa mwaka huu 2024 ambao ndiyo kijana alipaswa kujiunga form one walichukua kijana mmoja tu kutoka kayumba.

Si kwamba hawa vijana hawana uwezo kitaaluma la hasha.

Mdau yule nilimdodosa na kumuuliza kwa nini kupotezea watu muda na rasilimali bila sababu.UKIZINGATIA mchakato wa usaili unaanzia Parokia anayotoka kijana. Pia wanafanya usaili kwenye vikarieti written na oral mara mbili na baada ya hapo ndipo wanaitwa kwenye seminari husika kwa usaili tena na kote huko unalipia.

Jibu alilonipa ni kwamba wanataka wazazi wenye uwezo wa kulipa ada kwa uhakika. Kuchangia harambee mbalimbali zinazoitishwa na mambo mengine mengi.

Kigezo kingine umahiri ktk kuzungumza kiingereza.(Hili nilishangaa kidogo sababu najua kabisa kuongea kiingeeza kunarahisisha ufundishaji lakin kujua kiingereza si kigezo cha uwezo wa kiakili wa mtoto.) Ni vitu viwili tofauti.

Hivyo inaonyesha kadiri miaka inavyosogea hata katika imani tutajikuta tunaongozwa na makasisi kutoka familia za kitajiri na maskini hana chake hata ktk kanisa.

Seminari ninayoizungumzia iko moshi marangu mlimani huko. Ni maarufu sana. Japo siku hizi haivumi sana kama zamani katika rank za kitaifa.
MAua au St james iyo
 
Kuna shule za Sekondari kwa sasa St. Kuna kila sababu za kujenga msingi mzuri wa elimu kwa watoto, Huo ndio ukweli.
 
Jamaa hawataki longolongo🤣🤣🤣mamaeh
👇👇

Screenshot_20250116-083152_Chrome.jpg
 
Back
Top Bottom