Kadogosa: Kuna njama zinafanywa Kuhujumu treni ya SGR na hazijaanza Leo na tumeshawabaini Wanaotuhujumu!

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Kufuatia changamoto za hapa na pale zinazoipata TREN ya SGR boss wa TRC Masanja Kadogosa amesema Kuna njama zinafanywa Kuhujumu mradi huo

Njama hizi hazijaanza Leo ni za muda mrefu na tayari wameshawabaini miongoni mwa wanaowahujumu na watawashughulikia ipasavyo

Source Mwananchi

Mlale unono πŸ˜ƒ
 
Huu mradi haufiki Nyerere day
 
Yule Kadogosa ni mjinga kabisa, na ameshahisi anakwenda kufukuzwa, wote tunajua na tunaona uwezo duni wa watumishi wa umma kuweza kuendesha miradi. Mchawi mkuu wa TRC ni TRC wenyewe wakishirikiana na CCM na kwa hakika SGR itakufa kama inavyokufa mwendokasi.
 
Kwahiyo ninyi kama viongozi mnatulalamikia sisi wananchi ili iweje? Kwamba mmewabaini! Mtuhumiwa akibainika si anachukuliwa hatua za kisheria? Mmefanya hivyo?? Semeni kwamba wote ni wezi ni wahujumu uchumi, wahujumu maendeleo ya nchi..

Baba, mama, watoto wote wezi kwahiyo mnaogopana... Ninyi pigeni pesa tu mnapoona pesa imepungua tujazieni ma rundo ya kodi sisi ni maiti zilizolala hatuwezi kuamka kamwe... Kuleni nchi mazee hamjaanza leo wala jana
 
Huu ni uongo na kichaka Cha kujificha kukwepa kuwajibika Kwa sababu za uzembe.

Hakuna anaweza kufanya hivyo maana ni hatari kwake,so asitafute visingizio vya kijinga
 
Sins of our fathers, kuna katabia or tamaduni ya kushindwa kusimamua project na kulinda project zinazoanzishwa nchini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…