Kaduma alikuwa the best Cartoonist. Hizi kazi zinaweza kuwa animated?

N'yadikwa

JF-Expert Member
Joined
Aug 10, 2014
Posts
7,427
Reaction score
10,905
Jamaa pamoja na crew yake enzi za gazeti la sani walikuwa wanachora real life na kwa viwango...yaani unafuatilia vile vibonzo na unafurahika kabisa, huku Madenge akiwa ndo stelingi kwenye hii series ya jaridani enzi za dahari huko...Nashauri wahusika mzikusanye hizi kazi mziweke katika mfumo wa mjongeo (video ) ....muwaumbe hao characters vilevile tuendelee kupata burudani ktk simu zetu.
Mfano kina Quimby kazi zao za akina Tommy and Jerry bado zinaishi.
Madenge ni mfano halisi wa baadhi ya watoto wa siku hizi ambao hawataki kusikia la mkuu.
Ulimkubali nani kwenye series hii ya Sani.
Vielelezo vina hakimiliki
 
hela za kununua dvd moja tsh 10000 mnazo!!?..au ndo mnataka watu wahangaike kutengeneza nyie mchomeane kirahisi tu!!?
 
John kaduma(r.i.p) gwiji la michoro afrika mashariki na kati. Yeye mwenyewe akiijita 'fogastar'. Alikuwa moto wa kuotea mbali. Hii ilinifanya nipende kuchora pia. Alichora kiuhalisia, hadithi na michoro yake vilizungumza. Yamkini, alikuwa na mchango mkubwa katika tasnia hiyo. Palikuwa vilevile, na kina Dikwe ndoto, fortunatus ndilla, willy kisangas, chriss katembo, ibra radi washokera, maggie, N.k. Lakini kaduma kwa maoni yangu aliwakuwa the best. Sijui vipaji hivi vinathaminiwaje, sijui watu hawa wanakumbukwaje, sijui wamenufaikaje pia na vipaji vyao. Wizara yenye dhamana, ina wajibu wa kuwaangalia wasanii wachoraji. Binafsi, nilikuwa najichorea na kutunga kwa ajili ya burudani tu enzi nikiwa primary na secondary. Ifikie pahala, sanaa(fani) iwe ni maisha. Na sio kuburudisha, kuelimisha na kuonya tu. Nakumbuka hadithi zao, murua za Kistoni ninja,pablo zungu , (mchoraji kaduma), mlinzi wa zamu(fortunatus ndilla), pwani yawanyonge(mchoraji chris katembo). Mlikuwa na mchango na hakika kazi zenu mlizifanya kattika mazingira magumu ya teknolojia.
 
Lakini nadhan mchoraji mkuu alikuwa ndugulu kwanza then walaja akina kaduma
 
Alikua na mdogo wake anaitwa James Kaduma naye alifata nyendo za kaka yake "vile vile" sijui aliishia wapi tena.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…