Kaduma alikuwa the best Cartoonist. Hizi kazi zinaweza kuwa animated?

Kaduma alikuwa the best Cartoonist. Hizi kazi zinaweza kuwa animated?

John kaduma(r.i.p) gwiji la michoro afrika mashariki na kati. Yeye mwenyewe akiijita 'fogastar'. Alikuwa moto wa kuotea mbali. Hii ilinifanya nipende kuchora pia. Alichora kiuhalisia, hadithi na michoro yake vilizungumza. Yamkini, alikuwa na mchango mkubwa katika tasnia hiyo. Palikuwa vilevile, na kina Dikwe ndoto, fortunatus ndilla, willy kisangas, chriss katembo, ibra radi washokera, maggie, N.k. Lakini kaduma kwa maoni yangu aliwakuwa the best. Sijui vipaji hivi vinathaminiwaje, sijui watu hawa wanakumbukwaje, sijui wamenufaikaje pia na vipaji vyao. Wizara yenye dhamana, ina wajibu wa kuwaangalia wasanii wachoraji. Binafsi, nilikuwa najichorea na kutunga kwa ajili ya burudani tu enzi nikiwa primary na secondary. Ifikie pahala, sanaa(fani) iwe ni maisha. Na sio kuburudisha, kuelimisha na kuonya tu. Nakumbuka hadithi zao, murua za Kistoni ninja,pablo zungu , (mchoraji kaduma), mlinzi wa zamu(fortunatus ndilla), pwani yawanyonge(mchoraji chris katembo). Mlikuwa na mchango na hakika kazi zenu mlizifanya kattika mazingira magumu ya teknolojia.
Hakukuwa na mazingira magumu! Bali yale ndio yalikuwa uhalisia wa maisha ya wakati ule.
Ukigundua kiberiti usijidanganye kuwa eti aliyekuwa anapekecha moto alikuwa anapata tabutabu.
 
Pimbi ni bingwa wa kutongoza lakini hajawahi kula mzigo hata siku moja.
 
Sijui nini kilitokea kwa Sani maana badae lilikuja kuibuka jarida la Bongo huko nako kulikua hatari riwaya km Msako wa hayawani; Msako wa Mr.X; Anga za wenyewe;Dunia gunia; zilikua moto wa kuotea mbali
Kwa Sani riwaya ya Ole na Linda ilinisisimua sana!
 
Kama mtu unajua kuchora bila shaka lazima uwatambue hao 'malegends'...
 
Ahahaa.....Jarida la sani lilikuwa noma....ukilinganisha na mingine kama tabasamu
 
Au pambano la Zena na Betina mi nilijua ni kweli wapo Dar hao wadada wawili enzi hizo.
Aisee acha tuu, nakumbuka kipindi hicho tunashindana kuwachora hao cartoon darasani mpaka mwenzetu alipata zawadi kiwilaya,
 
Hii nchi sijui ina laana! Hawa watu kwa kazi walizokuwa wakizifanya ingekuwa ni tunu kubwa sana kwa taifa hili kama wangetaka kuangalia kwa jicho la tatu. Teknolojia ilivyokuwa hivi sisi kwetu inatumika kwenye siasa tu. Upumbavu mkubwa huu, wakati hapa nchini kuna wigo mpana mno wa ajira ila wahusika hawana muda nao, wamekaa kufungia fungia tu kazi za wanaojituma
 
Hii avatar yako inabidi uniundie nami hilo begu jeusi hapo kwangu liwe linachezacheza pia
Hiyo ni mbegu ya mti unaofanana na mnazi unapatikana visiwa vya Shelisheli; Mbegu zinaumbile la kati la mwanamke (love seed)
 
Fortunatus Ndila yuko wapi siku hizi? Nakumbuka alikua na a.k.a yake akijiita mtaalamu.
 
Back
Top Bottom