Kafaulu freshi form 4 anataka aende kusomea computer, Aende kusomea Taaluma ipi na chuo gani ?

baada ya kuifatilia nimeona hii kozi ina demand kubwa nchi za ulaya na Marekani lakini kibongo bongo bado sana, inaweza kumpa taabu baada ya kuhitimu
Umefanyaje tafiti hapa Bongo na kupata hitimisho kuwa cyber security bado sana?
 
Kuna vyuo pia nimeona vinatoa dip za computer science, wakiingia degree ni muendelezo.

Lengo ni afike degree, hivyo ataanza diploma kisha degree

Hio cyber security ina soko hapa bongo ?
 
Mtu aliefanya vizuri form four kwa div 1 or 2 akienda diploma ya Engineering course akafaulu vizuri pia diploma, Degree anaruhusiwa kusoma course yoyote inayohusiana na Engineering.

Labda huko kwenye afya na sanaa.
 
Kozi hii nimeona inaweza kumpa shida baada ya kuhitimu, yeye kachukua ushauri kwenye forums za marekani.

Ina pesa nyingi sana Ulaya na Marekani lakini kwa bongo kuna fursa chache.
Ushauri wangu kama ni mvulana mpeleke akasome diploma ya Mechanical engineering or Civil Engineering.

1. Civil Engineering

2.Mechanical engineering

Kama anampango wakuja kuajiriwa, lakini kama anampango wa kujiajiri muache akasome mambo ya Computer.
 
Nakujibu hapa.
Kama target ya mhitimu wa form four ni kuja kusoma degree yoyote katika fani anayoipenda basi njia iliyonyooka ni kusoma A-level kwanza. Kitendo cha mhitimu wa kidato cha nne kukimbilia kusoma diploma fulani katika hiyo field maana yake kwa zaidi ya 90% ni kujifunga kusoma degree inayooana na hiyo diploma tu. Diploma ya phylosophy haikupi mlango wa moja kwa moja kuja kusomea degree ya sheria. Sijui ni vyuo gani kwa hapa Tanzania vya sheria vinavyodahili mhitimu wa diploma ya phylosophy kusoma degree ya sheria lakini ni maajabu makubwa kwao waache kuwachukua kwanza wahitimu wa form six au wahitimu wa diploma ya sheria ili kumchukua mhitimu wa diploma ya phylosophy.

Kwa mhitimu wa form six aliyegundua alikosea kusoma degree of phylosophy, akitaka kusoma degree tofauti, anaomba upya na kuanza kusoma degree nyingine.
 
Tatizo unaongea bila ushahidi.

Wanafunzi wengi wa diploma wanajiendeleza degree na mikopo wanapata, Kigezo cha diploma kuingia degree awe na gpa ya 3.0+

Nenda TCU uone vigezo vya vyuo vyote kwa wahitimu wanaotoka Diploma kwenda Degree

unashangaa diploma ya philosophy kwenda kusomea degree ya sheria ? Udsm kusome uhasibu unahitaji diploma ya aina yoyote unahitaji uwe na C kwenye hesabu form 4 au diploma

 
Mtu aliefanya vizuri form four kwa div 1 or 2 akienda diploma ya Engineering course akafaulu vizuri pia diploma, Degree anaruhusiwa kusoma course yoyote inayohusiana na Engineering.

Labda huko kwenye afya na sanaa.
Mkuu Engineer ni kitu kipana sana, sasa unazungumzia engineer ipi?
Kwa mfano zipo Engineer za Chemical, Biotechnology, Computer, Civil, Mechanical, Automobile, Aircraft, Architecture, Oil, Mineral, nuclear etc.

Sasa mhitimu wa kidato cha nne akienda kusoma diploma ya Computer engineer hawezi kuja kuitumia hiyo diploma kama tiketi ya kutaka kusoma degree ya civil engineer, kwa sababu hizo ni field mbili tofauti kabisa japokuwa zote ni engineer.
 
Hicho ulichokikopi ni kipande cha maelezo lakini ukakifafanua vibaya, ukiwa na mapungufu kwa 100%.
Kwa mfano embu nawe tafakari, ni vipi mhitimu wa diploma ya fani za afya (udaktari, ufamasia, uuguzi etc) akawa na sifa za kusoma degree of accounting&commerce pale UDSM?

Let be realistic.
 
Hapana anaweza soma sema lazima usome miaka mnne
 
Hapana anaweza soma sema lazima usome miaka mnne
Embu fafanua hapa ili tuelewe, ni vipi Computer science inaoana na Civil engineer kiasi ambacho diploma ya kozi mojawapo inakupa nafasi ya kusoma degree ya fani nyingine.

Upande wa pili, karibu vyuo vyote hapa Tanzania, kozi za engineer ni miaka minne kwa wanafunzi wote.
 
Ukitoka diploma na computer Engineering , unaweza soma degree ya civil Engineering.

Kama unaendelea na course Ile Ile unasoma degree miaka mitatu, lakini ukichangua course nyingine unasoma miaka minne.

Ukiwa umesoma diploma ya Mechanical ukataka usome degree ya Mechanical unaanzia mwaka wa pili degree.

Lakini kama umesoma Mechanical diploma,ukataka usome degree ya Civil Engineering unaanzia mwaka wa kwanza degree.

Mimi nimesoma Mechanical engineering, ingawa nilitoka form six kwenda chuo, nawatu waliokuwa wanatoka diploma tulikua tunakutana nao mwaka wa pili. Na hii ni kwa sababu ukiwa unasoma degree mwaka wa kwanza course zote mnasoma kitu kinachofanana, masomo yote yanakua ni "Basic engineering" Labda kama utaratibu umebadilika hivi karibuni, mimi nilimaliza 2018.
 
utachosha vidole vyako, huyo jamaa yupo very subjective
 
Nashukuru, kwa maelezo yako mapana.
Sasa, embu kuwa specific na logic.
Tupe miongozo hapa ya TCU au Vyuo husika inayotoa nafasi ya mhitimu yoyote wa diploma ya engineer kuingia kusoma kozi yoyote ya engineer kwa ngazi ya degree.

Upande wa pili, kwa mfano tupe logic ya kusema diploma ya Computer engineer ni equivallent relevant ya kudahiliwa kusoma degree ya Civil engineer, ama diploma ya biotech engineer ikawa ni equivalent qualification kuingia kusoma degree ya computer engineer wakati ni field mbili tofauti kabisa.

Mwisho kabisa, masomo basic for engineer yanatofautiana mnoo na field. Field ya Computer, Mechanical, Chemical, Biological hayawezi kuwa kwenye kapu moja, hivyo basic hayawezi kuwekwa kwenye basic moja.
 
Ukisoma diploma ya civil Ukitaka kusoma degree civil utasoma miaka mitatu ila aliyetoka faculty nyingine au A level atasoma miaka mnne sijui utakuwa umenielewa?
 
Mkuu nazungumzia kipindi nasoma ilikua hivyo labda kama sasa imebadilika, watu wa civil/Mechanical/Electric/Telecom/computer Engineering wote mwaka wa kwanza tulikua tunafanana module. Labda kwa sasa kama mambo yamebadilika.

Chini hapa ni screen shot ya Admission guide book kutoka diploma kwenda degree ya 2024/2025.

Hizi ni qualifications za DIT, duration mi miaka 3 kwa mwanafunzi anaetok diploma kwenda degree, nimeangalia haraka haraka.

Angalia hio mining/Biomedical, kesho nikitulia ntapitia zote kwa utulivu.

Karibu kama unajambo lingine.

Cc much know

 
utachosha vidole vyako, huyo jamaa yupo very subjective
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…