Kafaulu sana lakini kapangiwa shule haina maabara

Kafaulu sana lakini kapangiwa shule haina maabara

kichenchele

JF-Expert Member
Joined
Jun 28, 2010
Posts
539
Reaction score
176
Poleni na majukumu ndugu zangu.

Naombeni ushauri wa mawazo ya nini cha kufanya au wapi pa kuanzia, kuna mdogo wangu mtoto wa Shangazi yangu, amemaliza form 4 Mzumbe na kubahatika kufaulu kwa daraja la kwanza na point 12 na katika combination yake ya PCB. ana B+,B+,A.

Lakini amepangiwa shule ambayo kiukweli kwa mjibu wa maelezo yake haina hata maabara na ndo imeanzishwa mwaka huu kwa maana wao ndo wanaanza na form five. Huyu mtoto ni yatima na amesomeshwa na babu yake lakini naona anawaza sana kwa maana anasema juhudi zake ndo zimepelekwa pale?

Sasa mimi kama ndugu yake nimeona nije humu kuomba ushauri wa mawazo juu ya nini afanye walau apate shule nzuri na yenye ushindani aweze kuendelea na juhudi zake kama mwanzo, nawaombeni tu msaada wa mawazo ili kama uwezekano ahame katika hii shule maana mimi sielewi process unaanzia wapi na je uwezekano upo?

Tumsaidie kama mdogo wetu sote apate walau shule nzuri.
 
tafuta mtu wizara ya elimu anaehusika na mambo ya kuhama amfanyie mpango ahame
 
Sasa mkuu hutaki ndugu yako aende katika hiyo shule, akina nani watasoma hapo kama kila mtu atakuwa na mawazo au fikra kama zako, muache awe mmoja wa waanzilishi, hizo changamoto zipo kila mahali chini ya serikali ya ccm.
 
Sasa mkuu hutaki ndugu yako aende katika hiyo shule, akina nani watasoma hapo kama kila mtu atakuwa na mawazo au fikra kama zako, muache awe mmoja wa waanzilishi, hizo changamoto zipo kila mahali chini ya serikali ya ccm.

Namshangaa na mimi.
 
Sasa kwa BRN hata serikali inajua kuwa hajafaulu bali kafaulishwa
 
Nenda mzumbe shule aliyomaliza o levo.. Kaongea na head master kama kuna nafasi atakubaliwa kuhamia..
 
Sasa mkuu hutaki ndugu yako aende katika hiyo shule, akina nani watasoma hapo kama kila mtu atakuwa na mawazo au fikra kama zako, muache awe mmoja wa waanzilishi, hizo changamoto zipo kila mahali chini ya serikali ya ccm.

umeongea kisomi na kizalendo
 
hawez kubaliwa,atleast angekua na A,A,A au A,A,B+ kwenye kombi yake.

Kijana nakielewa ninachozungumza pcb wanachukua mwisho points 5.yan b+, b+ na A.
Mzumbe nilipoiacha mim ilikua inachukua wanafunzi 30 tu wa pcb. Na kati ya hao weng walikuwa na point 5.
Kwa matokeo yake ya brn inawezkana kuwa watu wa pcb wamefaulu wengi ndo mana katika ushindani akatupwa nje.
Wanafunzi watakaochaguliwa hapo mzumbe sio wote watakaoripot, ina maana kuna nafasi zitabakia wazi ambazo watu wenye sifa kama yeye waliokosa mara ya kwanza wanaruhusiwa kuzijaza hizo nafasi.
 
Lakini amepangiwa shule ambayo kiukweli kwa mjibu wa maelezo yake haina hata maabara na ndo imeanzishwa mwaka huu kwa maana wao ndo wanaanza na form five.
[/SIZE][/FONT][/QUOTE]
ungethibitisha kwanza alichokwambia huyo dogo kuhus uwepo wa maabara ndo ungelikuja jf.
 
Poleni na majukumu ndugu zangu.

Naombeni ushauri wa mawazo ya nini cha kufanya au wapi pa kuanzia, kuna mdogo wangu mtoto wa Shangazi yangu, amemaliza form 4 Mzumbe na kubahatika kufaulu kwa daraja la kwanza na point 12 na katika combination yake ya PCB. ana B+,B+,A.

Lakini amepangiwa shule ambayo kiukweli kwa mjibu wa maelezo yake haina hata maabara na ndo imeanzishwa mwaka huu kwa maana wao ndo wanaanza na form five. Huyu mtoto ni yatima na amesomeshwa na babu yake lakini naona anawaza sana kwa maana anasema juhudi zake ndo zimepelekwa pale?

Sasa mimi kama ndugu yake nimeona nije humu kuomba ushauri wa mawazo juu ya nini afanye walau apate shule nzuri na yenye ushindani aweze kuendelea na juhudi zake kama mwanzo, nawaombeni tu msaada wa mawazo ili kama uwezekano ahame katika hii shule maana mimi sielewi process unaanzia wapi na je uwezekano upo?

Tumsaidie kama mdogo wetu sote apate walau shule nzuri.
Aende akasome tu, haina shida. Hata mimi nilisoma A level shule haikua na maabara lakini tulifaulu.
 
Back
Top Bottom