kapyela
Member
- Feb 13, 2013
- 11
- 8
Na David KAFULILA
KUNA sababu nyingi za kuchelewa kwa LNG yetu kulinganisha pengine na tulivotarajia kama nchi lakn pia kulinganisha na washindani wetu eneo hilo kama Mozambique.
Sababu kubwa kwa maoni yangu mimi ni anguko la bei ya gas duniani kwa karibu muongo mzima. Tathimini ilofanywa na taasisi ya kimataifa ya Natural Resources Governance Institute ( NRGI) kwenye report yao mwaka 2014 ilionesha kwamba kwa mazingira ya kuzalisha LNG Tanzania bei inatakiwa walau iwe $14 kwa 1mmmBtu( kufikia Break even point ). Kitu ambacho hakijatokea kwa muda sasa.
Sio kiwango cha juu sana kwani kuna miaka ilifika hata 18/mmmBtu. Hata hivyo bei ya gas iliendelea kuanguka mpaka $7/mmmBtu na hata $3.5/mmmBtu. Anguko hili la bei ya gas linawapa sababu makampuni haya( IOCs) kwanza kufikiria upya uwekezaji wao kama waendelee lkn zaidi kama wanaendelea wanalazimika kuja na terms mpya zenye mabadiliko makubwa kutokana na tofauti kubwa ya anguko la bei.
Lakn wapo wanaoweza hoji kwann Mozambique tulianza nao miaka ya 2012/13 lakn wao wakafikia muafaka kwajili ya uwekezaji( Investment Decision) kabla yetu wakati sababu za anguko la bei ni dunia nzima?
Kunaweza kuwa na sababu za ziada , lakn kwa maoni yangu moja ya sababu kubwa ni kwamba gas yao ni rahisi kuivuna kwa gharama nafuu kuliko Tanzania na hivyo wanakuwa na faida ya kuishindan. Asilimia 85% ya gas ya Mozambique ipo kinakifupi(shallow water) ambapo wastani wa kuchimba kisima ni kati ya $50m-$70m kulinganisha na Tanzania ambapo asilimia 90% ya Gas ipo kinakirefu(deepsea) ambapo wastani wa bei ya kuchimba kisima kimoja ni $100m-$120m. ( hii kwa takwimu za mwaka 2015).
Kwa mazingira hayo ni wazi kwamba ilikuwa rahisi kwa IOCs kuanza Mozambique hasa ukizingatia anguko hili kubwa la bei. Sababu nyingine ni uwezo wetu wa ndani kwenye eneo la gas ambalo mkataba mkubwa kama huu wa $30bn, unahusisha taaluma nyingi kuanzia Sayansi za gas, biashara, uchumi, sheria na zote zinahitaji uzoefu mkubwa na sio tu suala la Dr au Profesa kwani mnaenda mezani kukaa na kampuni zenye uzoefu wa zaidi ya karne eneo hilo.
Katika hali ya kawaida tunahitaji kuhusisha wazoefu wakubwa eneo hilo hata kama wanatoka nje. Tusijilazimishe kutumia wataalamu wa ndani kwenye maeneo ambayo hatujajiandaa. Kwenye dunia ya ushindani unaangalia tu unataka nn haijalishi anaekusaidia anatoka wapi.
Ndio sababu Uingereza baada ya mtiksiko wa uchumi duniani wa mwaka 2008 waliajiri Gavana wa Bank Kuu ambae ni raia wa Canada ambae amewahi kuwa Gavana wa Bank Kuu Canada.( sijiulizi kama Tz tunaweza bali nchi ngapi duniani zimefika huko? Chache mno na sio kosa).Tuangalie uwezo na tunachokitaka.
Maana yangu ni kwamba kwa mabadiliko makubwa katika eneo la gas yaliyojitokeza katika muongo mmoja ni wazi yatalazimisha fikra tofauti majadiliano ya mikataba tofauti na mazoea ya hapo kabla. Hii maanake inahitaji team yenye uwezo na mauzoefu ya kutosha eneo hili ili kutosumbuana kwenye majadiliano.
Tunawezakupata mshauri mwelekezi kutoka popote duniani sio kuamua bali kusaidia team yetu ikiwemo kujengeana ufahamu wa ziada. Nasema hili kwasababu lazma na muhimu tuamue kwa usahihi haijalishi kwa bei gani muhimu ndio bei sahihi.
Nasema haya kwasababu huko mbeleni jambo hili linaweza kuleta siasa za kwann tumekubali terms hizi wakati kwingine walifanya kwa terms nzuri zaidi bila kujua biashara hii ni complex na inategema mambo mengi ikiwemo mazingira yenu kama nilivoeleza hapo juu na zaidi muda mnaoingia mkataba kwa maana soko linazungumza nini na matarajio yapoje( market projections), impact ya COVID-19 kwenye FDI duniani na zaidi Africa ambayo itaongoza kwa anguko la FDI, pia masuala ya usalama ambapo washindani ktk biashara hizo usikute terrorism ni sehemu ya business strategy.
Nasema hili kwakuzingatia kilichotokea Mozambique juzi ambapo kampuni ya TOTAL imeahirisha uwekezaji mkubwa wa LNG ya $20bn kwa hofu za usalama kutokana na masuala ya ugaidi.sisemi kwamba tufurahie kushindwa kwa Mozambique ni fursa kwetu maana Rais wetu sio muumini wa 'zero sum game' kwamba ufaidike kwa mwenzako kuumia! Bali nachosema ni lesson tunapojipanga.
Huu ni uwekezaji mkubwa kupata kutokea kwenye ukanda wote wa africa mashariki. Ni nusu ya uchumi wa Tz, ni theluthi ya uchumi wa Kenya na ni sawa na uchumi wa Uganda au mara mbili ya uchumi wa Rwanda.
Nihitimishe kwa kusema tusiogope kutafuta mshauri popote duniani kusaidiana na wataalamu wetu kufikia mkataba bora. Sio aibu! Uingereza wakati inachakata kujitoa umoja wa Ulaya- BREXIT , ilikodi mtaalamu mshauri ( consultant) kutoka Newzland kuongoza team ya Uingereza kufikia mikataba mipya ya kibiashara na mataifa mengine dunian.
Alipohojiwa waziri Mkuu wa Uingereza kwann atafute mtaalamu nje wakati Uingereza ina heshima kubwa kwa kuwa na vyuo bora duniani alijibu kwamba Uingereza imepoteza uzoefu wake ktk kuingia mikataba ya aina hiyo kama nchi kwani kwa miaka mingi ilifanywa Brussels chini ya Umoja wa Ulaya( EU).
Zaidi, nikweli tumechelewa, lakn hatujachelewa sana kwa kuzingatia uzoefu wetu kisera na kitaasisi eneo hilo. Nakumbuka Canada, Taifa kubwa, lenye sera imara na wataalamu wakubwa na wenye uzoefu mkubwa eneo la gas kuliko sisi walifikia makubaliano na IOCs kwa mradi mmoja wa Kitimat wa $31bn( karibu sawa na wetu wa $30bn) Mwaka 2018 baada ya miaka7 ya majadiliano, na walikuwa na miradi 20, mingine 19 wakakubaliana kutokubaliana ! Yote ni makubaliano, muhimu iwe hivyo kama ni lazma sana.
Wasalaam.
MUHIMU: Haya ni maoni yangu kama David Kafulila.
KUNA sababu nyingi za kuchelewa kwa LNG yetu kulinganisha pengine na tulivotarajia kama nchi lakn pia kulinganisha na washindani wetu eneo hilo kama Mozambique.
Sababu kubwa kwa maoni yangu mimi ni anguko la bei ya gas duniani kwa karibu muongo mzima. Tathimini ilofanywa na taasisi ya kimataifa ya Natural Resources Governance Institute ( NRGI) kwenye report yao mwaka 2014 ilionesha kwamba kwa mazingira ya kuzalisha LNG Tanzania bei inatakiwa walau iwe $14 kwa 1mmmBtu( kufikia Break even point ). Kitu ambacho hakijatokea kwa muda sasa.
Sio kiwango cha juu sana kwani kuna miaka ilifika hata 18/mmmBtu. Hata hivyo bei ya gas iliendelea kuanguka mpaka $7/mmmBtu na hata $3.5/mmmBtu. Anguko hili la bei ya gas linawapa sababu makampuni haya( IOCs) kwanza kufikiria upya uwekezaji wao kama waendelee lkn zaidi kama wanaendelea wanalazimika kuja na terms mpya zenye mabadiliko makubwa kutokana na tofauti kubwa ya anguko la bei.
Lakn wapo wanaoweza hoji kwann Mozambique tulianza nao miaka ya 2012/13 lakn wao wakafikia muafaka kwajili ya uwekezaji( Investment Decision) kabla yetu wakati sababu za anguko la bei ni dunia nzima?
Kunaweza kuwa na sababu za ziada , lakn kwa maoni yangu moja ya sababu kubwa ni kwamba gas yao ni rahisi kuivuna kwa gharama nafuu kuliko Tanzania na hivyo wanakuwa na faida ya kuishindan. Asilimia 85% ya gas ya Mozambique ipo kinakifupi(shallow water) ambapo wastani wa kuchimba kisima ni kati ya $50m-$70m kulinganisha na Tanzania ambapo asilimia 90% ya Gas ipo kinakirefu(deepsea) ambapo wastani wa bei ya kuchimba kisima kimoja ni $100m-$120m. ( hii kwa takwimu za mwaka 2015).
Kwa mazingira hayo ni wazi kwamba ilikuwa rahisi kwa IOCs kuanza Mozambique hasa ukizingatia anguko hili kubwa la bei. Sababu nyingine ni uwezo wetu wa ndani kwenye eneo la gas ambalo mkataba mkubwa kama huu wa $30bn, unahusisha taaluma nyingi kuanzia Sayansi za gas, biashara, uchumi, sheria na zote zinahitaji uzoefu mkubwa na sio tu suala la Dr au Profesa kwani mnaenda mezani kukaa na kampuni zenye uzoefu wa zaidi ya karne eneo hilo.
Katika hali ya kawaida tunahitaji kuhusisha wazoefu wakubwa eneo hilo hata kama wanatoka nje. Tusijilazimishe kutumia wataalamu wa ndani kwenye maeneo ambayo hatujajiandaa. Kwenye dunia ya ushindani unaangalia tu unataka nn haijalishi anaekusaidia anatoka wapi.
Ndio sababu Uingereza baada ya mtiksiko wa uchumi duniani wa mwaka 2008 waliajiri Gavana wa Bank Kuu ambae ni raia wa Canada ambae amewahi kuwa Gavana wa Bank Kuu Canada.( sijiulizi kama Tz tunaweza bali nchi ngapi duniani zimefika huko? Chache mno na sio kosa).Tuangalie uwezo na tunachokitaka.
Maana yangu ni kwamba kwa mabadiliko makubwa katika eneo la gas yaliyojitokeza katika muongo mmoja ni wazi yatalazimisha fikra tofauti majadiliano ya mikataba tofauti na mazoea ya hapo kabla. Hii maanake inahitaji team yenye uwezo na mauzoefu ya kutosha eneo hili ili kutosumbuana kwenye majadiliano.
Tunawezakupata mshauri mwelekezi kutoka popote duniani sio kuamua bali kusaidia team yetu ikiwemo kujengeana ufahamu wa ziada. Nasema hili kwasababu lazma na muhimu tuamue kwa usahihi haijalishi kwa bei gani muhimu ndio bei sahihi.
Nasema haya kwasababu huko mbeleni jambo hili linaweza kuleta siasa za kwann tumekubali terms hizi wakati kwingine walifanya kwa terms nzuri zaidi bila kujua biashara hii ni complex na inategema mambo mengi ikiwemo mazingira yenu kama nilivoeleza hapo juu na zaidi muda mnaoingia mkataba kwa maana soko linazungumza nini na matarajio yapoje( market projections), impact ya COVID-19 kwenye FDI duniani na zaidi Africa ambayo itaongoza kwa anguko la FDI, pia masuala ya usalama ambapo washindani ktk biashara hizo usikute terrorism ni sehemu ya business strategy.
Nasema hili kwakuzingatia kilichotokea Mozambique juzi ambapo kampuni ya TOTAL imeahirisha uwekezaji mkubwa wa LNG ya $20bn kwa hofu za usalama kutokana na masuala ya ugaidi.sisemi kwamba tufurahie kushindwa kwa Mozambique ni fursa kwetu maana Rais wetu sio muumini wa 'zero sum game' kwamba ufaidike kwa mwenzako kuumia! Bali nachosema ni lesson tunapojipanga.
Huu ni uwekezaji mkubwa kupata kutokea kwenye ukanda wote wa africa mashariki. Ni nusu ya uchumi wa Tz, ni theluthi ya uchumi wa Kenya na ni sawa na uchumi wa Uganda au mara mbili ya uchumi wa Rwanda.
Nihitimishe kwa kusema tusiogope kutafuta mshauri popote duniani kusaidiana na wataalamu wetu kufikia mkataba bora. Sio aibu! Uingereza wakati inachakata kujitoa umoja wa Ulaya- BREXIT , ilikodi mtaalamu mshauri ( consultant) kutoka Newzland kuongoza team ya Uingereza kufikia mikataba mipya ya kibiashara na mataifa mengine dunian.
Alipohojiwa waziri Mkuu wa Uingereza kwann atafute mtaalamu nje wakati Uingereza ina heshima kubwa kwa kuwa na vyuo bora duniani alijibu kwamba Uingereza imepoteza uzoefu wake ktk kuingia mikataba ya aina hiyo kama nchi kwani kwa miaka mingi ilifanywa Brussels chini ya Umoja wa Ulaya( EU).
Zaidi, nikweli tumechelewa, lakn hatujachelewa sana kwa kuzingatia uzoefu wetu kisera na kitaasisi eneo hilo. Nakumbuka Canada, Taifa kubwa, lenye sera imara na wataalamu wakubwa na wenye uzoefu mkubwa eneo la gas kuliko sisi walifikia makubaliano na IOCs kwa mradi mmoja wa Kitimat wa $31bn( karibu sawa na wetu wa $30bn) Mwaka 2018 baada ya miaka7 ya majadiliano, na walikuwa na miradi 20, mingine 19 wakakubaliana kutokubaliana ! Yote ni makubaliano, muhimu iwe hivyo kama ni lazma sana.
Wasalaam.
MUHIMU: Haya ni maoni yangu kama David Kafulila.