Kafulila: Kwanini utekelezaji mradi wa LNG Tanzania umechelewa?

Kafulila: Kwanini utekelezaji mradi wa LNG Tanzania umechelewa?

kapyela

Member
Joined
Feb 13, 2013
Posts
11
Reaction score
8
Na David KAFULILA

KUNA sababu nyingi za kuchelewa kwa LNG yetu kulinganisha pengine na tulivotarajia kama nchi lakn pia kulinganisha na washindani wetu eneo hilo kama Mozambique.

Sababu kubwa kwa maoni yangu mimi ni anguko la bei ya gas duniani kwa karibu muongo mzima. Tathimini ilofanywa na taasisi ya kimataifa ya Natural Resources Governance Institute ( NRGI) kwenye report yao mwaka 2014 ilionesha kwamba kwa mazingira ya kuzalisha LNG Tanzania bei inatakiwa walau iwe $14 kwa 1mmmBtu( kufikia Break even point ). Kitu ambacho hakijatokea kwa muda sasa.

Sio kiwango cha juu sana kwani kuna miaka ilifika hata 18/mmmBtu. Hata hivyo bei ya gas iliendelea kuanguka mpaka $7/mmmBtu na hata $3.5/mmmBtu. Anguko hili la bei ya gas linawapa sababu makampuni haya( IOCs) kwanza kufikiria upya uwekezaji wao kama waendelee lkn zaidi kama wanaendelea wanalazimika kuja na terms mpya zenye mabadiliko makubwa kutokana na tofauti kubwa ya anguko la bei.

Lakn wapo wanaoweza hoji kwann Mozambique tulianza nao miaka ya 2012/13 lakn wao wakafikia muafaka kwajili ya uwekezaji( Investment Decision) kabla yetu wakati sababu za anguko la bei ni dunia nzima?

Kunaweza kuwa na sababu za ziada , lakn kwa maoni yangu moja ya sababu kubwa ni kwamba gas yao ni rahisi kuivuna kwa gharama nafuu kuliko Tanzania na hivyo wanakuwa na faida ya kuishindan. Asilimia 85% ya gas ya Mozambique ipo kinakifupi(shallow water) ambapo wastani wa kuchimba kisima ni kati ya $50m-$70m kulinganisha na Tanzania ambapo asilimia 90% ya Gas ipo kinakirefu(deepsea) ambapo wastani wa bei ya kuchimba kisima kimoja ni $100m-$120m. ( hii kwa takwimu za mwaka 2015).

Kwa mazingira hayo ni wazi kwamba ilikuwa rahisi kwa IOCs kuanza Mozambique hasa ukizingatia anguko hili kubwa la bei. Sababu nyingine ni uwezo wetu wa ndani kwenye eneo la gas ambalo mkataba mkubwa kama huu wa $30bn, unahusisha taaluma nyingi kuanzia Sayansi za gas, biashara, uchumi, sheria na zote zinahitaji uzoefu mkubwa na sio tu suala la Dr au Profesa kwani mnaenda mezani kukaa na kampuni zenye uzoefu wa zaidi ya karne eneo hilo.

Katika hali ya kawaida tunahitaji kuhusisha wazoefu wakubwa eneo hilo hata kama wanatoka nje. Tusijilazimishe kutumia wataalamu wa ndani kwenye maeneo ambayo hatujajiandaa. Kwenye dunia ya ushindani unaangalia tu unataka nn haijalishi anaekusaidia anatoka wapi.

Ndio sababu Uingereza baada ya mtiksiko wa uchumi duniani wa mwaka 2008 waliajiri Gavana wa Bank Kuu ambae ni raia wa Canada ambae amewahi kuwa Gavana wa Bank Kuu Canada.( sijiulizi kama Tz tunaweza bali nchi ngapi duniani zimefika huko? Chache mno na sio kosa).Tuangalie uwezo na tunachokitaka.

Maana yangu ni kwamba kwa mabadiliko makubwa katika eneo la gas yaliyojitokeza katika muongo mmoja ni wazi yatalazimisha fikra tofauti majadiliano ya mikataba tofauti na mazoea ya hapo kabla. Hii maanake inahitaji team yenye uwezo na mauzoefu ya kutosha eneo hili ili kutosumbuana kwenye majadiliano.

Tunawezakupata mshauri mwelekezi kutoka popote duniani sio kuamua bali kusaidia team yetu ikiwemo kujengeana ufahamu wa ziada. Nasema hili kwasababu lazma na muhimu tuamue kwa usahihi haijalishi kwa bei gani muhimu ndio bei sahihi.

Nasema haya kwasababu huko mbeleni jambo hili linaweza kuleta siasa za kwann tumekubali terms hizi wakati kwingine walifanya kwa terms nzuri zaidi bila kujua biashara hii ni complex na inategema mambo mengi ikiwemo mazingira yenu kama nilivoeleza hapo juu na zaidi muda mnaoingia mkataba kwa maana soko linazungumza nini na matarajio yapoje( market projections), impact ya COVID-19 kwenye FDI duniani na zaidi Africa ambayo itaongoza kwa anguko la FDI, pia masuala ya usalama ambapo washindani ktk biashara hizo usikute terrorism ni sehemu ya business strategy.

Nasema hili kwakuzingatia kilichotokea Mozambique juzi ambapo kampuni ya TOTAL imeahirisha uwekezaji mkubwa wa LNG ya $20bn kwa hofu za usalama kutokana na masuala ya ugaidi.sisemi kwamba tufurahie kushindwa kwa Mozambique ni fursa kwetu maana Rais wetu sio muumini wa 'zero sum game' kwamba ufaidike kwa mwenzako kuumia! Bali nachosema ni lesson tunapojipanga.

Huu ni uwekezaji mkubwa kupata kutokea kwenye ukanda wote wa africa mashariki. Ni nusu ya uchumi wa Tz, ni theluthi ya uchumi wa Kenya na ni sawa na uchumi wa Uganda au mara mbili ya uchumi wa Rwanda.

Nihitimishe kwa kusema tusiogope kutafuta mshauri popote duniani kusaidiana na wataalamu wetu kufikia mkataba bora. Sio aibu! Uingereza wakati inachakata kujitoa umoja wa Ulaya- BREXIT , ilikodi mtaalamu mshauri ( consultant) kutoka Newzland kuongoza team ya Uingereza kufikia mikataba mipya ya kibiashara na mataifa mengine dunian.

Alipohojiwa waziri Mkuu wa Uingereza kwann atafute mtaalamu nje wakati Uingereza ina heshima kubwa kwa kuwa na vyuo bora duniani alijibu kwamba Uingereza imepoteza uzoefu wake ktk kuingia mikataba ya aina hiyo kama nchi kwani kwa miaka mingi ilifanywa Brussels chini ya Umoja wa Ulaya( EU).

Zaidi, nikweli tumechelewa, lakn hatujachelewa sana kwa kuzingatia uzoefu wetu kisera na kitaasisi eneo hilo. Nakumbuka Canada, Taifa kubwa, lenye sera imara na wataalamu wakubwa na wenye uzoefu mkubwa eneo la gas kuliko sisi walifikia makubaliano na IOCs kwa mradi mmoja wa Kitimat wa $31bn( karibu sawa na wetu wa $30bn) Mwaka 2018 baada ya miaka7 ya majadiliano, na walikuwa na miradi 20, mingine 19 wakakubaliana kutokubaliana ! Yote ni makubaliano, muhimu iwe hivyo kama ni lazma sana.


Wasalaam.

MUHIMU: Haya ni maoni yangu kama David Kafulila.
 
New Zealand na Canada wanatofauti gani na Uingereza? Si kama nchi moja tu, bali wapo maeneo mbalimbali duniani?

Sipingi wazo la kuwa na "Mshauri/Washauri" wenye uzoefu mpana kwenye eneo husika, lakini pia ni lazima kuelewa kwamba hapa tulipofikia tunao wataalam wengi katika maeneo mbalimbali, wataalam ambao kwa hakika hawapati changamoto ya kuonyesha umahiri wao.

Kama taifa, ni muhimu tuwe na utaratibu wa kuwapa changamoto hawa watu watuonyeshe wanachoweza kufanya. Kutokuaminiwa huku kunazaa kutojiamini wao wenyewe pia kwamba hawawezi.

Tusichanganye haya tunayoyaona mara kwa mara, wachache wakipewa kazi na kuboronga, halafu tukachukulia kuwa hawawezi. Ni lazima yawepo mazingira ya kuwawezesha, na motisha mkubwa wa kuwajengea uaminifu kwa taifa lao.
Israel wamefanya mengi kwa kujiamini, hali kadharika India na kwingineko.

Ni lazima tujiamini kuwa sasa tunao uwezo wa kufanya mambo mengi yanayotuhusu sisi wenyewe. Tunapokwama na kuhitaji msaada, hiyo haiwezi kuwa aibu, duniani kote hufanya hivyo.
 
Na David KAFULILA

KUNA sababu nyingi za kuchelewa kwa LNG yetu kulinganisha pengine na tulivotarajia kama nchi lakn pia kulinganisha na washindani wetu eneo hilo kama Mozambique.

Sababu kubwa kwa maoni yangu mimi ni anguko la bei ya gas duniani kwa karibu muongo mzima. Tathimini ilofanywa na taasisi ya kimataifa ya Natural Resources Governance Institute ( NRGI) kwenye report yao mwaka 2014 ilionesha kwamba kwa mazingira ya kuzalisha LNG Tanzania bei inatakiwa walau iwe $14 kwa 1mmmBtu( kufikia Break even point ). Kitu ambacho hakijatokea kwa muda sasa.

Sio kiwango cha juu sana kwani kuna miaka ilifika hata 18/mmmBtu. Hata hivyo bei ya gas iliendelea kuanguka mpaka $7/mmmBtu na hata $3.5/mmmBtu. Anguko hili la bei ya gas linawapa sababu makampuni haya( IOCs) kwanza kufikiria upya uwekezaji wao kama waendelee lkn zaidi kama wanaendelea wanalazimika kuja na terms mpya zenye mabadiliko makubwa kutokana na tofauti kubwa ya anguko la bei.

Lakn wapo wanaoweza hoji kwann Mozambique tulianza nao miaka ya 2012/13 lakn wao wakafikia muafaka kwajili ya uwekezaji( Investment Decision) kabla yetu wakati sababu za anguko la bei ni dunia nzima?

Kunaweza kuwa na sababu za ziada , lakn kwa maoni yangu moja ya sababu kubwa ni kwamba gas yao ni rahisi kuivuna kwa gharama nafuu kuliko Tanzania na hivyo wanakuwa na faida ya kuishindan. Asilimia 85% ya gas ya Mozambique ipo kinakifupi(shallow water) ambapo wastani wa kuchimba kisima ni kati ya $50m-$70m kulinganisha na Tanzania ambapo asilimia 90% ya Gas ipo kinakirefu(deepsea) ambapo wastani wa bei ya kuchimba kisima kimoja ni $100m-$120m. ( hii kwa takwimu za mwaka 2015).

Kwa mazingira hayo ni wazi kwamba ilikuwa rahisi kwa IOCs kuanza Mozambique hasa ukizingatia anguko hili kubwa la bei. Sababu nyingine ni uwezo wetu wa ndani kwenye eneo la gas ambalo mkataba mkubwa kama huu wa $30bn, unahusisha taaluma nyingi kuanzia Sayansi za gas, biashara, uchumi, sheria na zote zinahitaji uzoefu mkubwa na sio tu suala la Dr au Profesa kwani mnaenda mezani kukaa na kampuni zenye uzoefu wa zaidi ya karne eneo hilo.

Katika hali ya kawaida tunahitaji kuhusisha wazoefu wakubwa eneo hilo hata kama wanatoka nje. Tusijilazimishe kutumia wataalamu wa ndani kwenye maeneo ambayo hatujajiandaa. Kwenye dunia ya ushindani unaangalia tu unataka nn haijalishi anaekusaidia anatoka wapi.

Ndio sababu Uingereza baada ya mtiksiko wa uchumi duniani wa mwaka 2008 waliajiri Gavana wa Bank Kuu ambae ni raia wa Canada ambae amewahi kuwa Gavana wa Bank Kuu Canada.( sijiulizi kama Tz tunaweza bali nchi ngapi duniani zimefika huko? Chache mno na sio kosa).Tuangalie uwezo na tunachokitaka.

Maana yangu ni kwamba kwa mabadiliko makubwa katika eneo la gas yaliyojitokeza katika muongo mmoja ni wazi yatalazimisha fikra tofauti majadiliano ya mikataba tofauti na mazoea ya hapo kabla. Hii maanake inahitaji team yenye uwezo na mauzoefu ya kutosha eneo hili ili kutosumbuana kwenye majadiliano.

Tunawezakupata mshauri mwelekezi kutoka popote duniani sio kuamua bali kusaidia team yetu ikiwemo kujengeana ufahamu wa ziada. Nasema hili kwasababu lazma na muhimu tuamue kwa usahihi haijalishi kwa bei gani muhimu ndio bei sahihi.

Nasema haya kwasababu huko mbeleni jambo hili linaweza kuleta siasa za kwann tumekubali terms hizi wakati kwingine walifanya kwa terms nzuri zaidi bila kujua biashara hii ni complex na inategema mambo mengi ikiwemo mazingira yenu kama nilivoeleza hapo juu na zaidi muda mnaoingia mkataba kwa maana soko linazungumza nini na matarajio yapoje( market projections), impact ya COVID-19 kwenye FDI duniani na zaidi Africa ambayo itaongoza kwa anguko la FDI, pia masuala ya usalama ambapo washindani ktk biashara hizo usikute terrorism ni sehemu ya business strategy.

Nasema hili kwakuzingatia kilichotokea Mozambique juzi ambapo kampuni ya TOTAL imeahirisha uwekezaji mkubwa wa LNG ya $20bn kwa hofu za usalama kutokana na masuala ya ugaidi.sisemi kwamba tufurahie kushindwa kwa Mozambique ni fursa kwetu maana Rais wetu sio muumini wa 'zero sum game' kwamba ufaidike kwa mwenzako kuumia! Bali nachosema ni lesson tunapojipanga.

Huu ni uwekezaji mkubwa kupata kutokea kwenye ukanda wote wa africa mashariki. Ni nusu ya uchumi wa Tz, ni theluthi ya uchumi wa Kenya na ni sawa na uchumi wa Uganda au mara mbili ya uchumi wa Rwanda.

Nihitimishe kwa kusema tusiogope kutafuta mshauri popote duniani kusaidiana na wataalamu wetu kufikia mkataba bora. Sio aibu! Uingereza wakati inachakata kujitoa umoja wa Ulaya- BREXIT , ilikodi mtaalamu mshauri ( consultant) kutoka Newzland kuongoza team ya Uingereza kufikia mikataba mipya ya kibiashara na mataifa mengine dunian.

Alipohojiwa waziri Mkuu wa Uingereza kwann atafute mtaalamu nje wakati Uingereza ina heshima kubwa kwa kuwa na vyuo bora duniani alijibu kwamba Uingereza imepoteza uzoefu wake ktk kuingia mikataba ya aina hiyo kama nchi kwani kwa miaka mingi ilifanywa Brussels chini ya Umoja wa Ulaya( EU).

Zaidi, nikweli tumechelewa, lakn hatujachelewa sana kwa kuzingatia uzoefu wetu kisera na kitaasisi eneo hilo. Nakumbuka Canada, Taifa kubwa, lenye sera imara na wataalamu wakubwa na wenye uzoefu mkubwa eneo la gas kuliko sisi walifikia makubaliano na IOCs kwa mradi mmoja wa Kitimat wa $31bn( karibu sawa na wetu wa $30bn) Mwaka 2018 baada ya miaka7 ya majadiliano, na walikuwa na miradi 20, mingine 19 wakakubaliana kutokubaliana ! Yote ni makubaliano, muhimu iwe hivyo kama ni lazma sana.


Wasalaam.

MUHIMU: Haya ni maoni yangu kama David Kafulila.
Kafulila hapa umeeleza kwa kitaalam saana na nina hakika utakuwa umepewa hizi nondo na wataalam walioko kwenye sekta.Kitakashosikitisha ni kwamba lile kundi linalompinga mama halitaki huu mradi kwa sababu wanaamini kuwa mama akifanimiwa kwenye huu mradi ambao ndio utakuwa mkubwa kuliko miradi yote Afrika ,mama atakuwa si tu amefanikiwa kuwezasha kuuza gesi yetu nchi za nje bali atakuwa amefungua rasmi mikoa ya kusini kama new players kwenye uchumi wa Tanzania
 
New Zealand na Canada wanatofauti gani na Uingereza? Si kama nchi moja tu, bali wapo maeneo mbalimbali duniani?

Sipingi wazo la kuwa na "Mshauri/Washauri" wenye uzoefu mpana kwenye eneo husika, lakini pia ni lazima kuelewa kwamba hapa tulipofikia tunao wataalam wengi katika maeneo mbalimbali, wataalam ambao kwa hakika hawapati changamoto ya kuonyesha umahiri wao.

Kama taifa, ni muhimu tuwe na utaratibu wa kuwapa changamoto hawa watu watuonyeshe wanachoweza kufanya. Kutokuaminiwa huku kunazaa kutojiamini wao wenyewe pia kwamba hawawezi.

Tusichanganye haya tunayoyaona mara kwa mara, wachache wakipewa kazi na kuboronga, halafu tukachukulia kuwa hawawezi. Ni lazima yawepo mazingira ya kuwawezesha, na motisha mkubwa wa kuwajengea uaminifu kwa taifa lao.
Israel wamefanya mengi kwa kujiamini, hali kadharika India na kwingineko.

Ni lazima tujiamini kuwa sasa tunao uwezo wa kufanya mambo mengi yanayotuhusu sisi wenyewe. Tunapokwama na kuhitaji msaada, hiyo haiwezi kuwa aibu, duniani kote hufanya hivyo.
Nadhani changamoto kubwa ya wasomi/ wataalamu wetu ni kuwa elimu zao zimewapa 'arrogance' badala ya 'confidence'.

With 'arrogance' wasomi/wataalamu wetu wamekuwa vinara wa kutumia elimu zao kudharau/kupuuza/kutukana wenzao na kutaka wao ndio wasikilizwe bila kujali ni nini wanaamua.

Tabia hii tumeshuhudia ikijirudia mara kadhaa na orodha ni ndefu. Utaona hata bungeni 'vijembe' dhidi ya wasomi na elimu yetu vimeahamiri simply kwa kuwa wasomi hawa hawaoneshi tija na kuvurunda kwao ndio kitu pekee kilicho kwenye record za kiutendaji.

With 'confidence' wasomi/wataalamu hutumia hekima ikiwa ni pamoja na ku-engage wataalam wengine ili kupata 'collective productivity' yenye tija bila kujali ni nani kahusika.

Utaona imekuwa ni kawaida kubeza hata maoni/hoja zenye tija toka kwa upinzani kwa mawazo kuwa zikitekelezwa zitawapa 'credit' wapinzani.

Muhongo, Mwakyembe, Kabudi et al ni miongoni mwa 'wasomi' walio/wanao angushwa na 'self arrogance'. Watu hawa pamoja na kuaminiwa na kupewa nafasi nyeti nadhani kila mtu ni shahidi wa kilicho endelea.

Kwa maoni yangu nadhani shida tuliyo nayo si wasomi bali ni aina ya wasomi/wataalam wetu na may be mfumo wa siasa zetu unachangia kuwafanya wawe walivyo.
 
Mikataba inatakiwa kuwa reviewed kuendana na hali halisi

Tumalizane tu hiyo LNG KWA MIKATABA YA HALI HALISIA YA SASA

Teknolojia zinabadilika kwa kasi sana tutakuja jikuta tuna mali useless mbeleni.Kinachoweza kufanyika sasa kifanyike

Mimi nilishauri hata CHUMA tuharakishe mikataba tuchimbe teknolojia zinabadilika tutakuja jikuta tuna lichuma ardhini lisilo na faida yeyote.Mfano tuna madini kibao ya ulanga hayo madini yalikuwa yana soko kubwa mno zamani sababu yalikuwa yakitumika kutengeneza vioo vyote viwe wa nyumba ,viwe vya magari nk kila nyumba ukiona ina kioo ujue ulanga!! Sasa hivi soko dogo mdo na bei chini mno!!

Nilifurahi kusikia uranium kule mikoa ya kusini inaanza kuchimbwa karibuni

Tuchimbe na makaa ya mawe kwa nguvu kubwa .Dangote alishaonyesha nia ya kuyataka kwa wingi lakini sielewi tatizo nini!! Uzalishaji wenyewe nasikia wa kusua sua tu hakuna uwekezaji mkubwa

Tuende na hali halisi .Hakuna mwekezaji anakuja kuja kula hasara lazima aangalie hali halisi na sisi tuangalie hali halisi wao wapate na sisi tupate
 
New Zealand na Canada wanatofauti gani na Uingereza? Si kama nchi moja tu, bali wapo maeneo mbalimbali duniani?
.
Ni kweli wote kiongozi wao mkuu ni malkia wa Uingerereza

Nadhani alichomaanisha ni kuwa tutusisite kutumia wataalamu wabobezi wa nje pia japo tuna wetu ambao nao wapo na wamekaa nje sana na wana uzoefu mkubwa pia kwenye maeneo hayo.

Mikataba mikubwa kama hiyo haitakiwi kufanywa na kundi moja pekee tunahitaji Consultants au advisors kutusaidia ku counter cheki pia .Wazawa pekee mmmm tunaweza kuja laumiana mbeleni !! AWEZA pewa pombe tu akakesha usiku kucha asubuhi akaamka nazo akasaini mkataba wa hovyo

Tusiachie tu maofisa wa serikali!!!

Nashauri ikifika mikataba ya mafuta na gesi ni vizuri kushirikisha pande tatu ziwemo kwenye team moja watu wazoefu kwenye biashara husika mfano ya gesi waliobobea waijuayo hiyo sekta ndani nje kutoka kwenye private sekta waliopo nchini ,pili wawepo wataalamu wa serikali wabobezi kwenye hiyo sekta na tatu CONSULTANTS au ADVISORS wa kutoka nje wabobezi kwenye hiyo sekta.Hawa ndio wawe team ya kutengeneza hiyo mikataba
 
Ni kweli wote kiongozi wao mkuu ni malkia wa Uingerereza

Nadhani alichomaanisha ni kuwa tutusisite kutumia wataalamu wabobezi wa nje pia japo tuna wetu ambao nao wapo na wamekaa nje sana na wana uzoefu mkubwa pia kwenye maeneo hayo.

Mikataba mikubwa kama hiyo haitakiwi kufanywa na kundi moja pekee tunahitaji Consultants au advisors kutusaidia ku counter cheki pia .Wazawa pekee mmmm tunaweza kuja laumiana mbeleni !! AWEZA pewa pombe tu akakesha usiku kucha asubuhi akaamka nazo akasaini mkataba wa hovyo

Tusiachie tu maofisa wa serikali!!!

Nashauri ikifika mikataba ya mafuta na gesi ni vizuri kushirikisha pande tatu ziwemo kwenye team moja watu wazoefu kwenye biashara husika mfano ya gesi waliobobea waijuayo hiyo sekta ndani nje kutoka kwenye private sekta waliopo nchini ,pili wawepo wataalamu wa serikali wabobezi kwenye hiyo sekta na tatu CONSULTANTS au ADVISORS wa kutoka nje wabobezi kwenye hiyo sekta.Hawa ndio wawe team ya kutengeneza hiyo mikataba

Mkuu YEHODAYA, itawezekanaje kuhusisha 'third party' kwenye kujadili mikataba ikiwa serikali ya CCM imeng'ang'ania kuifanya siri hiyo mikataba?

Kitendo tu cha serikali kufanya mikataba kuwa siri kwa kiwango ambacho umma wenyewe haujui kinacho endelea ni dalili tosha kwamba kuna 'madudu' ya kutosha humo wamesaini ndio maana nyie 'wanyonge' hamrusiwi kujua na mmeridhika.
 
Mkuu YEHODAYA, itawezekanaje kuhusisha 'third party' kwenye kujadili mikataba ikiwa serikali ya CCM imeng'ang'ania kuifanya siri hiyo mikataba?

Kitendo tu cha serikali kufanya mikataba kuwa siri kwa kiwango ambacho umma wenyewe haujui kinacho endelea ni dalili tosha kwamba kuna 'madudu' ya kutosha humo wamesaini ndio maana nyie 'wanyonge' hamrusiwi kujua na mmeridhika.
Usiwe mtumwa wa historia.Reforms nyingi tu kama hujui private sekta ilikuwa ikihusishwa.Lakini hata wao wakihusishwa itaendelea kuwa siri sababu mkataba ni kati ya pande mbili zinazosaini.

Lakini pia si kweli kuwa wananchi huwa hawajui hiyo mikataba.Wanajua sana kupitia wabunge wao waliowachagua.Kuna kamati za bunge za kisekta hata Lisu ALIKUWEMO HUMO!!! HIYO MIKATABA kamati hizo za bunge huwa wanaiona vizuri tu.
 
Usiwe mtumwa wa historia.Reforms nyingi tu kama hujui private sekta ilikuwa ikihusishwa.Lakini hata wao wakihusishwa itaendelea kuwa siri sababu mkataba ni kati ya pande mbili zinazosaini.

Lakini pia si kweli kuwa wananchi huwa hawajui hiyo mikataba.Wanajua sana kupitia wabunge wao waliowachagua.Kuna kamati za bunge za kisekta hata Lisu ALIKUWEMO HUMO!!! HIYO MIKATABA kamati hizo za bunge huwa wanaiona vizuri tu.

Ni mara kadhaa nimekuwa nikikuhoji kuhusu uelewa wako wa mambo, hebu pitia hicho ulicho kiandika kwa mara nyingine then ujihoji mwenyewe haya maswali:

1. Kama mikataba hiyo siyo siri, ni kwa nini mara kadhaa wabunge hasa wa upinzani wamekuwa wakidai iletwe bungeni na kujadiliwa kwa uwazi na mara zote serikali inagoma?

2. Hao wananchi unaosema wanajua kupitia wabunge wao, inawezekanaje wao wajue wakati wabunge wao wenyewe hawaijui kwa kuwa imefanywa siri na ndio maana wanadai kila siku ipelekwe kujadiliwa bungeni?

Hiyo mikataba unayoita ni siri ya pande mbili, tambua kuwa upande mmoja ndio hao wananchi ambao unataka wafichwe.

Jiulize kisha ukipata majibu yatunze kwa faida yako wala usijisumbue kuandika.
 
Ni mara kadhaa nimekuwa nikikuhoji kuhusu uelewa wako wa mambo, hebu pitia hicho ulicho kiandika kwa mara nyingine then ujihoji mwenyewe haya maswali:

1. Kama mikataba hiyo siyo siri, ni kwa nini mara kadhaa wabunge hasa wa upinzani wamekuwa wakidai iletwe bungeni na kujadiliwa kwa uwazi na mara zote serikali inagoma?
Ni uongo

Wabunge wanajua hasa wa kamati mfano mdogo nikueleze.Kamati ya bunge ya sheria na Katiba mikataba yote huwa wanaiona .Lisu alikuwemo humo ila sema wanaiona lakini hawaruhusiwi kuitangaza ila ku recommend kwenye kamati hu recommend

Walioko kwenye kamati huiona vizuri iwe ya mambo ya nje ya biashara nk
 
Ni uongo

Wabunge wanajua hasa wa kamati mfano mdogo nikueleze.Kamati ya bunge ya sheria na Katiba mikataba yote huwa wanaiona .Lisu alikuwemo humo ila sema wanaiona lakini hawaruhusiwi kuitangaza ila ku recommend kwenye kamati hu recommend

Walioko kwenye kamati huiona vizuri iwe ya mambo ya nje ya biashara nk
Let's assume unacho kisema ni sahihi, sasa kama wanaiona na hawaruhusiwi kuitangaza hao wananchi wameijuaje kupitia wabunge wao?

Ni wabunge wangapi wanaokuwa kwenye kamati ya sheria hadi useme wananchi wanaijua kupitia wabunge wao?
 
Kafulila usikariri tu please hakuna kisima cha dola 100 Million kisima chenye changamoto kubwa hakizidi Million 10 na hivyo ni deep mpaka feet alfu 11 acheni kukariri tu. suala la bei halihusiani na unachosema iwe bei ya Mafuta au Gas ziku zote zinabadilika leo hivi kesho vile mradi wowote ni kuangalia ukubwa wa resevoir ndio msingi sio kuangalia bei ya leo. sasa leo kama bei ni kubwa mradi unaanza baada ya miaka mitani mradi unakamilika kabla haujaanza bei imeanguka utafunga mradi? futa hiyo story yako haina mashiko. Uganda wana heavy Oil na heavy Oil bei yake chini lakini kwa sababu wanajuwa reservoir yao kwa hiyo ni commercial.
 
Na David KAFULILA

KUNA sababu nyingi za kuchelewa kwa LNG yetu kulinganisha pengine na tulivotarajia kama nchi lakn pia kulinganisha na washindani wetu eneo hilo kama Mozambique.
Sababu kubwa ni moja TU! Political Will iliyokuwa inawekwa kwenye kichaka cha "maslahi ya taifa"! Maslahi ya taifa kama yale ya kutuaminisha kwamba ni Acacia peke yake ndio walikuwa wezi wa madini yetu wakati kampuni zote za madini nchi hii zimekuwa zikituibia tangu late 1990's!
Sababu kubwa kwa maoni yangu mimi ni anguko la bei ya gas duniani kwa karibu muongo mzima. Tathimini ilofanywa na taasisi ya kimataifa ya Natural Resources Governance Institute ( NRGI) kwenye report yao mwaka 2014 ilionesha kwamba kwa mazingira ya kuzalisha LNG Tanzania bei inatakiwa walau iwe $14 kwa 1mmmBtu( kufikia Break even point ). Kitu ambacho hakijatokea kwa muda sasa.
Wakati Kampuni za Gas na Mafuta zinataka kuwekeza USD 30 Billion hawakufahamu kwamba kuna anguko la bei ya gas duniani?

Hata uikangalia bei ya gas kwa miaka 25 iliyopita, utaona mara ya mwisho LNG kuuzwa above (by average) USD 5/ MMBtu ni mwaka 2008.

Both Mozambique and TZ, ugunduzi mkubwa wa gas ulikuwa kuanzia 2010 to 2014, na katika kipindi hicho bei ilikuwa around USD 4.

Ukitoa kipindi cha corona, mwaka 2015 na 2016 ndo kilikuwa worst period kwa bei ya gas, lakini ni ndo muda huo huo Wawekezaji walikuwa tayari kujenga Gas Processing Plant kule Lindi.

That being said, ingawaje nakubaliana na hoja ya kushuka kwa bei ya gas lakini hiyo haiwezi kuwa sababu na ndo maana pamoja na kushuka huko bado uwekezaji ulitaka kuendelea!

Na hawawezi kuacha kuwekeza kwa kuogopa kushuka kwa bei kwa sababu, hata kama shughuli za uwekezaji zingeendelea bado hadi kufikia kufanya gas export ingechukua angalau miaka 5 baadae.

That being said, wangeongozwa sana na matarajio ya bei ya gesi angalau miaka 5 baadae (price forecast) kuliko kuangalia bei ya wakati huo.
Sio kiwango cha juu sana kwani kuna miaka ilifika hata 18/mmmBtu.
Haijawahi kutokea over the past 25 years!!
Hata hivyo bei ya gas iliendelea kuanguka mpaka $7/mmmBtu
Hicho ndo moja ya bei za juu kabisa kupata kutokea over the past 25 years!
na hata $3.5/mmmBtu.
Hii ndo average price kwa muongo mmoja sasa! Wakati plant inataka kujengwa pale Lindi, average price kwa mwaka ilikua chini ya USD 3/MMBtu
Anguko hili la bei ya gas linawapa sababu makampuni haya( IOCs) kwanza kufikiria upya uwekezaji wao kama waendelee lkn zaidi kama wanaendelea wanalazimika kuja na terms mpya zenye mabadiliko makubwa kutokana na tofauti kubwa ya anguko la bei.
Uwekezaji kwenye sekta ya gas unachukua at least 5 years, na kama nilivyosema hapo juu, maamuzi yangeangalia matarajio ya bei ya ges kwa miaka ya baadae!

Na katika kufanya hili wala wasingetumia regression analysis na kupandikiza secondary gas prices ili ku-forecast bei kwa miaka 5 hadi 10 ijayo, bali wangeangalia uchumi wa dunia kwa mapana yake in the next 5-10 years!

Kwa mfano, kama unaona China na EU uwekezaji unaongezeka kwa kasi, hapo moja kwa moja una-predict uwezekano wa demand for energy!

Kama takwimu za kiuchumi zinashawishi kuongezeka tabaka la watu wa kima cha kati barani Afrika, hapo moja kwa moja unapata picha ya shift kutoka matumizi ya kuni to vyanzo vingine vya nishati kama vile gas, na kuongezeka uzalishaji wa viwanda ambavyo navyo vitahitaji nishati!
Lakn wapo wanaoweza hoji kwann Mozambique tulianza nao miaka ya 2012/13 lakn wao wakafikia muafaka kwajili ya uwekezaji( Investment Decision) kabla yetu wakati sababu za anguko la bei ni dunia nzima?
Of course, ningehoji na kuanzia hapo andiko lote lisingekuwa na maana tena!!!
Kunaweza kuwa na sababu za ziada , lakn kwa maoni yangu moja ya sababu kubwa ni kwamba gas yao ni rahisi kuivuna kwa gharama nafuu kuliko Tanzania na hivyo wanakuwa na faida ya kuishindan. Asilimia 85% ya gas ya Mozambique ipo kinakifupi(shallow water) ambapo wastani wa kuchimba kisima ni kati ya $50m-$70m kulinganisha na Tanzania ambapo asilimia 90% ya Gas ipo kinakirefu(deepsea) ambapo wastani wa bei ya kuchimba kisima kimoja ni $100m-$120m. ( hii kwa takwimu za mwaka 2015). Kwa mazingira hayo ni wazi kwamba ilikuwa rahisi kwa IOCs kuanza Mozambique hasa ukizingatia anguko hili kubwa la bei.
Sijafanya utafiti kuhusu "gharama ya kuchimba kisima" huko Mozambique! Hata hivyo, takwimu zilizopo, including hizo za Tanzania sio gharama za kuchimba hasa bali ni gharama za utafutaji kwa kisima!!

Ambacho kimefanyika ni gas exploration, na kwa Tanzania, ni sahihi gharama kwa kisima ilikuwa inafika hadi USD 100M... kama mtakumbuka, ndo maana Msema Ovyo, Sospeter Muhongo alisema "Wafanyabiashara ya Tanzania hamna pesa ya kuchimbia gesi"!

Ilikuwa ni kauli ya kukera lakini ni UKWELI MTUPU!!!

Kama nilivyosema, hizo USD 100M sio kuchimba gas bali kutafuta gas! Kwamba, unapewa eneo ambalo data zinashawishi kwamba "hapa" panaweza kuwa na gas! Ili kujiridhisha kama kweli gas ipo, na kama ipo ni kwa kiasi gani (kuangalia kama ni economically viable kuichimba), ndipo unachimba kisima cha kwanza kujiridhisha!!!

Baada ya kuchimba, unaweza kukuta gas ambayo kiuchumi unaweza kufanya uwekezaji ili kuchimba rasmi, au unaweza kukuta gas ambayo ukisema ufanye shughuli za kuchimba, gas itakayopatikana inaweza isirudishe gharama, au unaweza usikute gas kabisa!!

Case ya II na III ina maana pesa ulizowekeza kwenye kuchimba hicho kisima zinakuwa zimeenda na maji!!!!

So, hizo ni gharama za utafutaji na sio uchimbaji

Pamoja na yote hayo, leo ndo mara yangu ya kwanza kusikia gas ya Mozambique inapatikana kwenye shallow water...

For what I know, maeneo makubwa yaliyogunduliwa gas Mozambique yamepewa jina la Area I na ARea IV. Hii Area I, ipo zaidi ya 30KM kutoka ufukweni, na Area IV ipo zaidi ya 40K kutoka ufukweni!!

Hiyo haiwezi kuwa shallow water, and in fact, both Mozambique na TZ, kiwango kikubwa cha gas kipo deep sea!!
Sababu nyingine ni uwezo wetu wa ndani kwenye eneo la gas ambalo mkataba mkubwa kama huu wa $30bn, unahusisha taaluma nyingi kuanzia Sayansi za gas, biashara, uchumi, sheria na zote zinahitaji uzoefu mkubwa na sio tu suala la Dr au Profesa kwani mnaenda mezani kukaa na kampuni zenye uzoefu wa zaidi ya karne eneo hilo.
Hapa Kafulila alikuwa anajaribu kusema nini?! Kwani huko Mozambique hayo mambo wanayo?
Katika hali ya kawaida tunahitaji kuhusisha wazoefu wakubwa eneo hilo hata kama wanatoka nje. Tusijilazimishe kutumia wataalamu wa ndani kwenye maeneo ambayo hatujajiandaa. Kwenye dunia ya ushindani unaangalia tu unataka nn haijalishi anaekusaidia anatoka wapi.
Na hata huko Mozambique watatumia watu wa nje!!
Ndio sababu Uingereza baada ya mtiksiko wa uchumi duniani wa mwaka 2008 waliajiri Gavana wa Bank Kuu ambae ni raia wa Canada ambae amewahi kuwa Gavana wa Bank Kuu Canada.( sijiulizi kama Tz tunaweza bali nchi ngapi duniani zimefika huko? Chache mno na sio kosa).Tuangalie uwezo na tunachokitaka.

Maana yangu ni kwamba kwa mabadiliko makubwa katika eneo la gas yaliyojitokeza katika muongo mmoja ni wazi yatalazimisha fikra tofauti majadiliano ya mikataba tofauti na mazoea ya hapo kabla. Hii maanake inahitaji team yenye uwezo na mauzoefu ya kutosha eneo hili ili kutosumbuana kwenye majadiliano.

Tunawezakupata mshauri mwelekezi kutoka popote duniani sio kuamua bali kusaidia team yetu ikiwemo kujengeana ufahamu wa ziada. Nasema hili kwasababu lazma na muhimu tuamue kwa usahihi haijalishi kwa bei gani muhimu ndio bei sahihi.

Nasema haya kwasababu huko mbeleni jambo hili linaweza kuleta siasa za kwann tumekubali terms hizi wakati kwingine walifanya kwa terms nzuri zaidi bila kujua biashara hii ni complex na inategema mambo mengi ikiwemo mazingira yenu kama nilivoeleza hapo juu na zaidi muda mnaoingia mkataba kwa maana soko linazungumza nini na matarajio yapoje( market projections), impact ya COVID-19 kwenye FDI duniani na zaidi Africa ambayo itaongoza kwa anguko la FDI, pia masuala ya usalama ambapo washindani ktk biashara hizo usikute terrorism ni sehemu ya business strategy.

Nasema hili kwakuzingatia kilichotokea Mozambique juzi ambapo kampuni ya TOTAL imeahirisha uwekezaji mkubwa wa LNG ya $20bn kwa hofu za usalama kutokana na masuala ya ugaidi.sisemi kwamba tufurahie kushindwa kwa Mozambique ni fursa kwetu maana Rais wetu sio muumini wa 'zero sum game' kwamba ufaidike kwa mwenzako kuumia! Bali nachosema ni lesson tunapojipanga.

Huu ni uwekezaji mkubwa kupata kutokea kwenye ukanda wote wa africa mashariki. Ni nusu ya uchumi wa Tz, ni theluthi ya uchumi wa Kenya na ni sawa na uchumi wa Uganda au mara mbili ya uchumi wa Rwanda.

Nihitimishe kwa kusema tusiogope kutafuta mshauri popote duniani kusaidiana na wataalamu wetu kufikia mkataba bora. Sio aibu! Uingereza wakati inachakata kujitoa umoja wa Ulaya- BREXIT , ilikodi mtaalamu mshauri ( consultant) kutoka Newzland kuongoza team ya Uingereza kufikia mikataba mipya ya kibiashara na mataifa mengine dunian.

Alipohojiwa waziri Mkuu wa Uingereza kwann atafute mtaalamu nje wakati Uingereza ina heshima kubwa kwa kuwa na vyuo bora duniani alijibu kwamba Uingereza imepoteza uzoefu wake ktk kuingia mikataba ya aina hiyo kama nchi kwani kwa miaka mingi ilifanywa Brussels chini ya Umoja wa Ulaya( EU).

Zaidi, nikweli tumechelewa, lakn hatujachelewa sana kwa kuzingatia uzoefu wetu kisera na kitaasisi eneo hilo. Nakumbuka Canada, Taifa kubwa, lenye sera imara na wataalamu wakubwa na wenye uzoefu mkubwa eneo la gas kuliko sisi walifikia makubaliano na IOCs kwa mradi mmoja wa Kitimat wa $31bn( karibu sawa na wetu wa $30bn) Mwaka 2018 baada ya miaka7 ya majadiliano, na walikuwa na miradi 20, mingine 19 wakakubaliana kutokubaliana ! Yote ni makubaliano, muhimu iwe hivyo kama ni lazma sana.


Wasalaam.

MUHIMU: Haya ni maoni yangu kama David Kafulila.
Hapo, sawa kabisa!
 
Mikataba inatakiwa kuwa reviewed kuendana na hali halisi

Tumalizane tu hiyo LNG KWA MIKATABA YA HALI HALISIA YA SASA

Teknolojia zinabadilika kwa kasi sana tutakuja jikuta tuna mali useless mbeleni.Kinachoweza kufanyika sasa kifanyike

Mimi nilishauri hata CHUMA tuharakishe mikataba tuchimbe teknolojia zinabadilika tutakuja jikuta tuna lichuma ardhini lisilo na faida yeyote.Mfano tuna madini kibao ya ulanga hayo madini yalikuwa yana soko kubwa mno zamani sababu yalikuwa yakitumika kutengeneza vioo vyote viwe wa nyumba ,viwe vya magari nk kila nyumba ukiona ina kioo ujue ulanga!! Sasa hivi soko dogo mdo na bei chini mno!!

Nilifurahi kusikia uranium kule mikoa ya kusini inaanza kuchimbwa karibuni

Tuchimbe na makaa ya mawe kwa nguvu kubwa .Dangote alishaonyesha nia ya kuyataka kwa wingi lakini sielewi tatizo nini!! Uzalishaji wenyewe nasikia wa kusua sua tu hakuna uwekezaji mkubwa

Tuende na hali halisi .Hakuna mwekezaji anakuja kuja kula hasara lazima aangalie hali halisi na sisi tuangalie hali halisi wao wapate na sisi tupate
Hii nchi ni tajri sana tatizo imechezewa sana CCM!
 
Mkuu YEHODAYA, itawezekanaje kuhusisha 'third party' kwenye kujadili mikataba ikiwa serikali ya CCM imeng'ang'ania kuifanya siri hiyo mikataba?

Kitendo tu cha serikali kufanya mikataba kuwa siri kwa kiwango ambacho umma wenyewe haujui kinacho endelea ni dalili tosha kwamba kuna 'madudu' ya kutosha humo wamesaini ndio maana nyie 'wanyonge' hamrusiwi kujua na mmeridhika.
Mkataba ni siri wew unataka ianikwe tu Kama a
Hadithi ya za bunuasi

Sent from my SM-A015F using JamiiForums mobile app
 
Mkataba ni siri wew unataka ianikwe tu Kama a
Hadithi ya za bunuasi

Sent from my SM-A015F using JamiiForums mobile app
Unafahamu kazi za bunge?

Bunge linawezaje kuishauri na kuisimamia serikali ikiwa serikali inaingia mikataba ya siri kiasi ambacho bunge lenyewe halitakiwi kuijua?
 
Nadhani changamoto kubwa ya wasomi/ wataalamu wetu ni kuwa elimu zao zimewapa 'arrogance' badala ya 'confidence'.

With 'arrogance' wasomi/wataalamu wetu wamekuwa vinara wa kutumia elimu zao kudharau/kupuuza/kutukana wenzao na kutaka wao ndio wasikilizwe bila kujali ni nini wanaamua.

Tabia hii tumeshuhudia ikijirudia mara kadhaa na orodha ni ndefu. Utaona hata bungeni 'vijembe' dhidi ya wasomi na elimu yetu vimeahamiri simply kwa kuwa wasomi hawa hawaoneshi tija na kuvurunda kwao ndio kitu pekee kilicho kwenye record za kiutendaji.

With 'confidence' wasomi/wataalamu hutumia hekima ikiwa ni pamoja na ku-engage wataalam wengine ili kupata 'collective productivity' yenye tija bila kujali ni nani kahusika.

Utaona imekuwa ni kawaida kubeza hata maoni/hoja zenye tija toka kwa upinzani kwa mawazo kuwa zikitekelezwa zitawapa 'credit' wapinzani.

Muhongo, Mwakyembe, Kabudi et al ni miongoni mwa 'wasomi' walio/wanao angushwa na 'self arrogance'. Watu hawa pamoja na kuaminiwa na kupewa nafasi nyeti nadhani kila mtu ni shahidi wa kilicho endelea.

Kwa maoni yangu nadhani shida tuliyo nayo si wasomi bali ni aina ya wasomi/wataalam wetu na may be mfumo wa siasa zetu unachangia kuwafanya wawe walivyo.
gspain, unajua tatizo la hawa watu kujiona wao ni zaidi ya wengine (arogance) inaanzia wapi?

Inatoka kwa wanasiasa, watawala. Hawa wengine wote ni waigaji tu toka kwa hao watawala.

Wasomi hawa wanapoona arrogance ya wanasiasa, tena ambao hata kusoma ni shida, basi wao ndio wanatumia usomi wao kujionyesha.

Wewe chukulia haya mambo ya kujitambulisha kila sehemu na digrii zao, Dr, Professor; Advanced Diploma, Honours, Engineer; na hata kuweka vyuo vyao, kama ni vyuo vyenye sifa duniani..., yote haya ni njia za kujihami tu na yalikuja kushamiri sana hapa nyumbani baada ya wanasiasa kuwa wanaburuza watu na kujifanya wao ni bora zaidi ya wengine.

Hiyo arrogance si tatizo hata kidogo kama nchi ikipania kuwatumia hawa wasomi kwa manufaa ya taifa. Msomi wa kweli hahangaiki kamwe na masifa kama hayo kama anajua taifa linamthamini kwa kazi zake nzuri anazofanya.

Kazi muhimu ni kuwajengea mazingira tu ili waonyeshe uzalendo wao. Mbona nchi nyingine wanaweza?
 
gspain, unajua tatizo la hawa watu kujiona wao ni zaidi ya wengine (arogance) inaanzia wapi?

Inatoka kwa wanasiasa, watawala. Hawa wengine wote ni waigaji tu toka kwa hao watawala.

Wasomi hawa wanapoona arrogance ya wanasiasa, tena ambao hata kusoma ni shida, basi wao ndio wanatumia usomi wao kujionyesha.

Wewe chukulia haya mambo ya kujitambulisha kila sehemu na digrii zao, Dr, Professor; Advanced Diploma, Honours, Engineer; na hata kuweka vyuo vyao, kama ni vyuo vyenye sifa duniani..., yote haya ni njia za kujihami tu na yalikuja kushamiri sana hapa nyumbani baada ya wanasiasa kuwa wanaburuza watu na kujifanya wao ni bora zaidi ya wengine.

Hiyo arrogance si tatizo hata kidogo kama nchi ikipania kuwatumia hawa wasomi kwa manufaa ya taifa. Msomi wa kweli hahangaiki kamwe na masifa kama hayo kama anajua taifa linamthamini kwa kazi zake nzuri anazofanya.

Kazi muhimu ni kuwajengea mazingira tu ili waonyeshe uzalendo wao. Mbona nchi nyingine wanaweza?
Uko sahihi, nadhani tunahitaji kujenga taasisi imara zisizo athiriwa na maslahi binafsi ya wanasiasa ili tuweza kuwa monitor wasomi wetu watuletee tija tarajiwa.

Hata pale wanasiasa wanapo jaribu kutuaminisha kuwa wanatekeleza ushauri wa wataalam/wasomi, deep down wasomi hao tunao ambiwa huwa wanashauri kwa kufuata maslahi ya wanasiasa pengine kulinda 'ugali' wao.

Wanasiasa wanatuambia tuwasikilize wataalam wakati wataalam wana wasikiliza wanasiasa, yaan wasomi wetu wamegeuzwa speaker za wanasiasa.
 
Back
Top Bottom