Kafulila: Milango iko wazi kwa mtu au kikundi kununua vichwa na mabehewa ya SGR kisha kuyaendesha kwa miundombinu ya serikali kwa sharti la ubia

Kafulila: Milango iko wazi kwa mtu au kikundi kununua vichwa na mabehewa ya SGR kisha kuyaendesha kwa miundombinu ya serikali kwa sharti la ubia

CM 1774858

JF-Expert Member
Joined
May 29, 2021
Posts
5,621
Reaction score
5,029
Mkurugenzi wa Ubia nchi Bwana David Kafulila ameiambia ARIDHIO ya TBC kuwa sasa ni rasmi mtu au kikundi chochote chenye uwezo na nia ya kununua na kuendesha vichwa vya treni pamoja na mabehewa ya SGR wanakaribishwa kufanya hivyo Kwa sharti la Ubia na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

Kafulila anasema, kama ilivyo kwa miundombinu mingine ya usafiri na usafirishaji ya Serikalí akitolea mfano wa barabara za Serikali kuna watu wamenunua Mabasi na wanayaendesha na Serikali inapata kodi lakini kubwa zaidi ni Wananchi kupata huduma bora na nzuri tena kwa wakati huku akitolea mfano wa mradi mkubwa kati ya DART na Mbia ambao kwa kiwango kikubwa uko tayari na mabasi zaidi 170 yataletwa kwa kuanzia divyo itakavyokuwa kwa SGR.

Kafulila anasema Serikali inafanya haya ili kuchachusha Uchumi wa nchi (economic stimulus) ambayo ndio hasa sera halisi na makini za Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan na kwa sera hizi ndiyo zinaifanya Tanzania kuendelea kusalia kileleni kwa uchumi jumuishi kwenye nchi zote za maziwa makuu na baadhi ya nchi kusini mwa Jangwa la sahara.

 
Ngoja waje Bavicha waseme👀
BAVICHA wanahusikaje?

1722418515355.png
 
Katika jambo lolote ni vema kufanya majaribio kupima kiwango cha matokeo..mazuri, wastani, mabaya..hakuna mradi wowote wa PPP hadi sasa ambao umejaribiwa au uko kwenye majaribio..sielewi kwa nini huyu mtu kila mara anarudia kitu kile kile, anabadilishabadilisha maneno, mara..kuchachusha sijui kuvutia..anza kwanza huo wa DART kwa majaribio kupima sera ya PPP inafaa au haifai au wapi parekebishwe kabla ya hii mingine..ana matatizo gani huyu??
 
Kafulila ni mtu wa msaada sana kwa Taifa ila hajatumika ni brand new
Waziri kaongea kabla Yake
Mkurigenzi WA TRC Kadogosa aliongea kablabyake kuhusu hilo Yeye anadakia wenzie waliyoongea kabla Yake kuongea hiyo Ardhio TBC kutafuta ujiko

Wenzie waliongea kabla yake

Yeye atusaidie kujibi uongo wake aliosema Kuwa mwenfo kasi Mwekezaji ndie atatanunua mabasi wakati Mchechu kasema mabasi yatanunuliwa Kwa mkopo ambao serikali itakopa Benki ya NMB

Aseme hapa mabasi ananunua Mwekezaji au serikali? Alanushe uongo wake aliongea kwenye kipindi cha mahojiano na TV
 
Katika jambo lolote ni vema kufanya majaribio kupima kiwango cha matokeo..mazuri, wastani, mabaya..hakuna mradi wowote wa PPP hadi sasa ambao umejaribiwa au uko kwenye majaribio..sielewi kwa nini huyu mtu kila mara anarudia kitu kile kile, anabadilishabadilisha maneno, mara..kuchachusha sijui kuvutia..anza kwanza huo wa DART kwa majaribio kupima sera ya PPP inafaa au haifai au wapi parekebishwe kabla ya hii mingine..ana matatizo gani huyu??
Mkuu,

Nadhani mambo ya Serikali ni mambo ya wengi

Nadhani tuamini anachotuambia kwani hata hivyo hana muda mrefu kwenye hii nafasi.

Rais Samia ameshamiria kuinua uchumi wa Watanzania wote.

#2025 MAMA MITANO TENA
 
Waziri kaongea kabla Yake
Mkurigenzi WA TRC Kadogosa aliongea kablabyake kuhusu hilo Yeye anadakia wenzie waliyoongea kabla Yake kuongea hiyo Ardhio TBC kutafuta ujiko

Wenzie waliongea kabla yake

Yeye atusaidie kujibi uongo wake aliosema Kuwa mwenfo kasi Mwekezaji ndie atatanunua mabasi wakati Msechu kasema mabasi yataninuliwa Kwa mkopo ambao serikali itakopa Benki ya NMB

Aseme hapa mabasi ananunua Mwekezaji au serikali? Alanushe uongo wake aliongea kwenye kipindi cha mahojiano na TV
Mbona hajasema chochote kuhusu NMB?

yeye kakazia alichosema kwamba zaidi ya Mabasi 170 ya Mbia yanakuja
 
===
Mkurugenzi wa Ubia nchi Bwana David Kafulila ameiambia ARIDHIO ya TBC kuwa Sasa ni rasmi mtu au kikundi chochote chenye Uwezo na nia ya kununua na kuendesha vichwa na treni za SGR wanakaribishwa kufanya hivyo Kwa sharti la Ubia na Serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

Kafulila anasema kama ilivyo kwa miundombinu ya usafiri na usafirishaji ya Serikalí akitolea mfano wa barabara kuna watu wamenunua Mabasi na wanayaendesha na Serikali inapata kodi lakini kubwa ni Wananchi kupata huduma Bora huduma nzuri na kwa wakati ndivyo itakavyokuwa kwa SGR huku akitolea mfano wa mradi mkubwa kati ya DART na Mbia ambao kwa kiwango kikubwa uko tayari na mabasi zaidi 170 yanaletwa kwa kuanzia.

Kafulila anasema Serikali inafanya haya ili kuchachusha Uchumi wa nchi ( economic stimulus ) ambayo ndio hasa sera za Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan na kwa sera hizi ndio zinaifanya Tanzania kuendelea kusalia kileleni kwenye nchi zote za maziwa makuu.

View attachment 3057496
Hiyo njia Haina mzigo wowote wa maana kumfanya Mwekezaji aweke treni yake
 
Bakhresa atanunua tu,siku nimekuta treni inavuta behewa zaidi ya kumi za Azam pekee.
 
Huu uzi ngoja nimtag mwanangu
MamaSamia2025
Unamsikia kafulila anataka watanzania wakawekeze hapo 😄
Au sisi ndiyo mwisho wetu viwanda vya pombe,juice unga soda nk

Ova
 
Back
Top Bottom