Kafulila: Rais Mkapa alijutia kuiua PSRC Parastatal Sector Reform Commission, PPP haiuzi Mali za Umma bali inazilinda kwa kipindi chote cha mkataba

Kafulila: Rais Mkapa alijutia kuiua PSRC Parastatal Sector Reform Commission, PPP haiuzi Mali za Umma bali inazilinda kwa kipindi chote cha mkataba

View attachment 3140086
View attachment 3140340
Hiki ndicho alichoandika Director wa PPP Tanzania Bw. David Kafulila huko kwenye akaunti yake ya X zamani tweeter.

Mkurugenzi huyo ameandika haya ili kuwatoa hofu wanaodhani huenda nchi yetu ikapata hasara ya mali na fedha kwa kuingia Ubia na Sekta binafsi toka ndani au nje ya Tanzania.

KAFULILA anarejelea Serikali ya awamu ya tatu Chini ya Hayati Rais Dkt. Benjamin Mkapa ambae katika kitabu chake Cha "My Life My Purpose " anasema baada ya kuuza mali za Umma kwa ubinafsishaji yakiwemo mashirika makubwa kama NBC kwa kupitia PSRC yaani Parastatal Sector Reform Commission anakiri alifanya makosa kuifuta tume hiyo ili ifanye ufuatiliaji wa mali zake zote ilizozifanyia ubinafshaji jambo lililozaa watu kuchukua mali za umma na kuzibadilishia matumizi, kukopea benki na uharibifu mwingine mwingi.

Kafulila anasema kwenye PPP Serikali na Sekta binafsi watamiliki mradi kwa pamoja na Serikali itakuwa ndio mwangalizi mkuu wa mradi kwa muda wote wa Mkataba na hii ndio tofauti kati ya Ubinafsishaji wa kipindi cha awamu ya tatu na Ubinafsishaji huu wa awamu ya sita kwa njia salama ya PPP.

Kafulila anasema PPP haiuzi mali za umma kama ilivyokuwa kwa PSRC bali inakodisha kwa kipindi maalum na baada kukodisha Serikali haiondoki kwenye mradi kwa kipindi chote cha Mkataba.

Na kwa ile miradi mipya itakayojengwa kwa Ubia kama zile Hosteli pale CBE baada ya muda wa Ubia kuisha miradi ile inarudi kuwa mali ya Serikali kwa asilimia 100.

Hata hivyo, ingawa haimaanishi Ubinafsishaji wa awamu ya tatu lilikuwa ni jambo baya hapana kwani ilikuwa ni njia sahihi ya kujenga Uchumi wa kisasa "modern economy" lakini matatizo hayawezi kuisha kabisa ila uamuzi wa Mzee Benjamin Mkapa wa ubinafshaji umekuwa na faida nyingi kuliko hasara Leo.


Pia soma Kwani Tulifeli vipi kwenye Ubinafsishaji wa Awamu ya 2 hadi Tufaulu sasa kwenye PPP ya David Kafulila?
Namwelewa sana Kafulila ni Bora akagombee ubunge akalisaidie Bunge
 
Navutiwa sana na staili ya kiuongozi ya David, umma wa Watanzania unataka majibu tu Wala sio pesa kama wengi wanavyofikiria.
Haka kanyani kanapiga tu porojo endelenii kuuza mali za umma na mikataba ya ovyo ya PPP kama wa DP World
 
Tatizo Kafulila hajui kitu chochote kile kuhusu masuala haya ya Miradi ya PPP hapa Tanzania. Mpaka Sasa, Serikali ya Tanzania tayari imeingia Mikataba mingi tu ya Miradi ya PPP kabla hata Rais Magufuli na Samia waingie madarakani, Je, huyo Kafulila ameshawahi kujiuliza kwamba nchi hii imekuwa ikinufaika Nini na hiyo Miradi ya PPP???

Tayari kuna Mikataba mingi ya Miradi ya PPP kati ya Tz na Makampuni mbalimbali kutoka nchini China, Je, Tanzania mpaka Sasa inanufaika nini kutokana na kuwepo kwa Miradi hiyo ya Ubia Kati ya Tz na China?? Kwanza huyo Kafulila mpaka Sasa anaijua Miradi hiyo ya Ubia ambayo tayari ipo kwenye utekelezaji tangu miaka mingi iliyopita??

Kafulila aache kupiga Domo na kupiga Propaganda za Siasa kuhusu suala hili la Miradi ya Ubia Kati ya Serikali na Sekta Binafsi, kwani hili ni suala gumu ambalo liko nje ya uwezo wake wa akili, na hata kwenye hii Serikali iliyopo Hakuna Watu ambao wako competent enough wa kuweza kuli-handle suala hili la Ubia. Wengi waliopo hawana uelewa wa kutosha kuhusiana na masuala haya ya Ubia na jinsi Miradi ya Ubia inavyoweza kutekelezwa kwa kuzalisha faida.
Nakazia hapa, mzee afanye yake aondoke aache kuwa dalali..
 
View attachment 3140086
View attachment 3140340
Hiki ndicho alichoandika Director wa PPP Tanzania Bw. David Kafulila huko kwenye akaunti yake ya X zamani tweeter.

Mkurugenzi huyo ameandika haya ili kuwatoa hofu wanaodhani huenda nchi yetu ikapata hasara ya mali na fedha kwa kuingia Ubia na Sekta binafsi toka ndani au nje ya Tanzania.

KAFULILA anarejelea Serikali ya awamu ya tatu Chini ya Hayati Rais Dkt. Benjamin Mkapa ambae katika kitabu chake Cha "My Life My Purpose " anasema baada ya kuuza mali za Umma kwa ubinafsishaji yakiwemo mashirika makubwa kama NBC kwa kupitia PSRC yaani Parastatal Sector Reform Commission anakiri alifanya makosa kuifuta tume hiyo ili ifanye ufuatiliaji wa mali zake zote ilizozifanyia ubinafshaji jambo lililozaa watu kuchukua mali za umma na kuzibadilishia matumizi, kukopea benki na uharibifu mwingine mwingi.

Kafulila anasema kwenye PPP Serikali na Sekta binafsi watamiliki mradi kwa pamoja na Serikali itakuwa ndio mwangalizi mkuu wa mradi kwa muda wote wa Mkataba na hii ndio tofauti kati ya Ubinafsishaji wa kipindi cha awamu ya tatu na Ubinafsishaji huu wa awamu ya sita kwa njia salama ya PPP.

Kafulila anasema PPP haiuzi mali za umma kama ilivyokuwa kwa PSRC bali inakodisha kwa kipindi maalum na baada kukodisha Serikali haiondoki kwenye mradi kwa kipindi chote cha Mkataba.

Na kwa ile miradi mipya itakayojengwa kwa Ubia kama zile Hosteli pale CBE baada ya muda wa Ubia kuisha miradi ile inarudi kuwa mali ya Serikali kwa asilimia 100.

Hata hivyo, ingawa haimaanishi Ubinafsishaji wa awamu ya tatu lilikuwa ni jambo baya hapana kwani ilikuwa ni njia sahihi ya kujenga Uchumi wa kisasa "modern economy" lakini matatizo hayawezi kuisha kabisa ila uamuzi wa Mzee Benjamin Mkapa wa ubinafshaji umekuwa na faida nyingi kuliko hasara Leo.


Pia soma Kwani Tulifeli vipi kwenye Ubinafsishaji wa Awamu ya 2 hadi Tufaulu sasa kwenye PPP ya David Kafulila?
______
Hii mada ni kubwa sana ila Kwa ujinga wa wabonge hawataweza kuipa nguvu kabisa
 
Kafulila anapambana sana jambo mambo ya nchi hii ni magumu by nature
 
Back
Top Bottom