..Kafulila alitakiwa atueleze ni asilimia ngapi ya wahitimu hapa Tz wanapata ajira mara baada ya kumaliza masomo.
..kwa maoni yangu Kafulila amekusanya takwimu na anazutumia kujenga hoja ambayo haiendani na uhalisia wa Tanzania.
..asilimia 60++ ya NGUVU KAZI ya Tanzania wako kwenye KILIMO. Kwa hiyo Kafulila alitakiwa ajenge hoja yake akizingatia ukweli / uhalisia huo.
..Badala yake Kafulila anajenga hoja kwa data zinazoelezea mazingira ya nchi zilizoko ktk hatua tofauti ya kimaendeleo na Tanzania.
..Huyu bwana nimemfuatilia ana tabia ya kusomba takwimu / data na kuzitumia ktk hoja zake bila kuzingatia uhalisia na mazingira ya Tanzania.
..Kunukuu data / takwimu ni jambo moja, na mara nyingi huwa ni jambo jepesi. Tatizo liko ktk kuelewa takwimu zinaeleza nini, na namna sahihi ya kuzitumia.
Cc
Mwananchi Huru