Kafulila: UNDP imetoa orodha ya nchi 54 duniani zilizoelemewa na deni la Taifa. 25 zinatoka Afrika Tanzania haipo, tukope zaidi tujenge Uchumi zaidi

Acha uongo moody wametoa credit rating ya B+
 
Nchi Nyingi maskini ziko kwenye rating hiyo
Ndio maana nikatumia analogue ya failure upate 39% au 0% it’s still a failure, sasa we unataka kuongelea failure yenye afadhali.

No one will lend you money directly and with low interest at B2 rating. Kwa ivyo huna tofauti na lower ratings wengine ambao wote mikopo yenu ni ya IMF/WB programmes; that is kama kuna huyo mpuuzi wa kukopesha nchi yenye B2 bila ya kupitia WB.
 
Hamna kitu ulichoongeaa apoo trillion 91 na umejenga nn ipo siku utanambia
 
Hakuna Maendeleo bila kukopa ,taja Nchi iliyoendelea bila kukopa
Narudia,mmelishwa utopolo.Kwanza mmedanganywa kuhusu maana ya maendeleo.Wenzenu wanachokiita maendeleo sio maendeleo.Maendeleo ni positive change ambayo hai athiri your culture,health,social well being and integrity.

Halafu wakaendelea kuwadanganya kwamba wanachokiita maendeleo ni muhimu,kumbe sio.Then wakawadanganya kwamba hicho kinachoitwa maendeleo kukipata lazima ukope,kumbe si kweli.Yaani kama mazuzu hivi.Very sad.
 
Hakuna anayeombea mabaya yatokee Tanzania Bali ni uongozi mbaya wa CCM . Deni limefika Trilioni 91 kwa uchache. Nani atatusaidia kulipa Hilo Deni?
Wana mpango wa Debt/Equity swaps ambao tayari umeshabuniwa.So Nia ya kutukopesha sio njema sana,lazima tuwe makini.The Debt Exchange, Inc. (also known as DebtX) ni kati ya makampuni yao makubwa yanayofanya kazi hizo.

Sasa najiuliza,sisi tutakapo-shindwa kulipa deni letu,tuta exchange or swap for what,Kilimanjaro Region,Manyara or Arusha?Yetu macho.
 
Orodha haituondolei ukweli kwamba tunadaiwa Trilioni 91.

Na majuzi tumeambiwa ni lazima tukope...yaani sisi bila.kukopa hatuwezi endesha nchi yetu.

Miaka 62 na uhuru inapoteza uhalisia kama ndiyo kwanza tunazidisha utegemezi.
 
Mbona mataifa makubwa yanakopa Sisi ni nan hata,nchi kubwa uko zinadaiwa matrilioni ya dola Sisi ivyo vibilion tunaona ni vingi sana tukope mradi tufanye vitu vya msingi
 
Mtu ambaye analalamika Kwamba nchi hii haiwez kujiendesha bila kukopa ni mjinga maana Hana uelewa wa kutosha
 
Mbona mataifa makubwa yanakopa Sisi ni nan hata,nchi kubwa uko zinadaiwa matrilioni ya dola Sisi ivyo vibilion tunaona ni vingi sana tukope mradi tufanye vitu vya msingi
Very misled.Hiyo ni misemo yao potofu ya kutufanya tukope.Ingekuwa mikopo inatoa,tungefika mahali tukaacha kukopa.Ukishakuwa debt dependent wewe ni mtumwa.Akopaye ni mtumwa wa akopeshaye,huo ndio ukweli mchungu.Mkopaji hana ujasiri wowote kwa aliyemkopesha.
 
Kafulila anasema, Ripoti ya UNDP Nov2022, imetaja nchi54 zenye hali mbaya ya deni la Taifa Dunian, huku 25 zikitoka Afrika wala Tanzania sio miongoni mwao,
Mpumbavu sana huyu tumbili,
Kwahiyo anataka tuwe wa 26 kwenye ligi!?
What if tungekuwa wa 1 -25 angesemaje
 
Tulishaambiwa huyo ni tumbili. Hivyo msishangae tumbili anatafiuta tawi la kurukia!😀😀😀
 
Nakurupuka hapa, kwani sijasoma yote yaliyojibiwa.

Hata wakati wa Serikali iliyoongozwa J.P.M ilisifiwa, ikaondolewa kwenye orodha kadha kadha hasi na kupachikwa vile vile kwenye orodha kadha kadha chanya...Mwisho wake tunajua.

Muulizeni bila kumumunya huyo Kafulila yeye amechangia ngapi katika kulipa madeni?? kwa namna yeyote ile???

Vilevile na sio siri kuwa utumwa na wizi wa Rasilimali za Africa, pamoja na sadaka za Kanisani na kwingine baada na wakati wa vita hivyo vikuu ndivyo vilivyopeleka hizo nchi za Ulaya kuujenga uchumi wao...! Na hiyo mikopo(kama deni lina maana ya mkopo) ilikuwa inatoka kwa wafanya biashara na makampuni yao....

Bado tuna kazi, tutafika, niko tayari kuumbuka huko mbele, niko tayari kusahihishwa lakini uwongo mwingine ni hatari, upotoshaji ni hatari.

ati "Msuli wa uchumi!" siku warudi wadai walipwe kwa msuli badala ya fedha je?
 
Kuna watu wanautafuta Ugali kwa njia nyingi- halali na haramu.
Swali: Je, njia ya uchawa ni halali au haramu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…