Kafulila: UNDP imetoa orodha ya nchi 54 duniani zilizoelemewa na deni la Taifa. 25 zinatoka Afrika Tanzania haipo, tukope zaidi tujenge Uchumi zaidi

Kwa hiyo Kafulila anashauri tujitahidi mpaka tuingie kwenye hiyo 25 bora?.

Sasa nimeamini akili ya Mwanasiasa ni kama mwili wa Kinyonga, hubadilika kuendana na mazingira aliyopo wakati huo...Sidhani kama angeongea hivi kama angekuwa upinzani.
 
Kwa hiyo Kafulila anashauri tujitahidi mpaka tuingie kwenye hiyo 25 bora?.

Sasa nimeamini akili ya Mwanasiasa ni kama mwili wa Kinyonga, hubadilika kuendana na mazingira aliyopo wakati huo...Sidhani kama angeongea hivi kama angekuwa upinzani.
Hujasema tuingie Ila ameonesha kuwa sio kweli nchi yetu imekopa sana,
 
Anaakili kama za kwangu nampongeza kwa uoni wake mikopo ya kimaendeleo kwa taifa sio mikopo ya kuuzia vitumbua hii ni mikopo endekevu ya kuendeleza taifa.
 
Kafulila bwana 😁😁 sijui ni Kiazi wa wapi huyu.
 
Anamainisha tukope ili na sisi tuelemewe na madeni au tujitahidi kujitegemea
 
Naunga mkono hoja,tupoke kwa ajili ya kujenga Uchumi.
 
Mara nyingi na kwa uzoefu wangu Pesa nyingi zinazopotea Ni Pesa za makusanyo ya ndani..

Pesa ya mkopo hata ikipoyea Ni kwenye utekelezaji wa mradi aidha ku overprice au kujenga chini ya kiwango.
 
Kwani uliambiwa hiyo til.21 inakuja kugawiwa Mtaani?

Inajenga miundombinu ambayo payback sio leo Wala kesho
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…