Kagame: Hakuna Haja ya Kuwa na Mikutano ya Kila Siku Isiyo na Tija Wakati Hatua Hazichukuliwi.

Ilikuaje yeye akahudhuria ?
Amehudhuria kwenda kumwambia samia asiwe anahudhuria mikutano ambayo imemzidi uwezo wa kufikiria na haisaidii nchi yake zaidi ya yeye kupiga picha labda na kukwea pipa kama mhudumu wa ndege.
 
Amehudhuria kwenda kumwambia samia asiwe anahudhuria mikutano ambayo imemzidi uwezo wa kufikiria na haisaidii nchi yake zaidi ya yeye kupiga picha labda na kukwea pipa kama mhudumu wa ndege.
Kwa nini yeye amehudhuria? Hawezi kupiga simu akaeleza hayo Hadi achome Mafuta?
 
Yuko sahihi kabisa huyu mzalendo wa Nchi yake.Ule mkutano wa Dar ulikuwa ni vichekesho tu yaani wanazunguka kusifiana na kusema wafungue uwanja wa ndege wa goma lakini wanayemtuhumu kusababisha vita wanamwogopa kumwambia.
Halafu hakuna walichoafikiana Cha maaana, azimio yote sijaona wakisema M23 waachie maeneo
 
Kwa nini yeye amehudhuria? Hawezi kupiga simu akaeleza hayo Hadi achome Mafuta?
Hukumsikia waziri wa elimu jinsi chawa aka wadaidizi ambavyo wanawafanyia watu wakihitaji kuzungumza na bi chaudele!!?
Kagame amemwambia akae alee mme aache kidhurura
 
Bora hata Rais wa DRC hakuja. Ni pumba tu zimetamkwa hakuna muafaka wala hakuna suluhisho linalolenga chanzo cha tatizo. Sio DRC, sio Rwanda wameamriwa kuchukua hatua stahiki na kupewa consequences za kutochukua hatua.

Kilichofanyika ni kutoa "wito" jambo ambalo kwa miaka zaidi ya 20 linafanyika. Wito wangetumiwa hata kwenye barua.
 
Mikutano hiyo haina tija.

Hivi kati ya wale Viongozi wa nchi waliohudhuria mkutano huo, Je, nani pale nchini mwake hana kabisa makandokando ya kuwepo kwa Mgogoro kama huo wa huko Kivu DRC? Nani hasa pale ni msafi kiasi kwamba anaweza kuwa na uthubutu wa kuweza kumkemea Rais Paul Kagame wa Rwanda kwa yale anayotuhumiwa kuyatenda kule DRC?
Karibia maRais wote kabisa waliohudhuria mkutano huu kila mmoja ana majanga yake kwenye nchi yake.

Kimsingi, Watu wote kabisa ambao wapo kwenye hiyo Kamati ya Usuluhishi wa Mgogoro huo wa huko Goma DRC hawana uhalali wowote ule wa kuweza kutatua Mgogoro huo. Kwa kifupi ni kwamba hakuna hata Mtu mmoja kwenye hiyo Timu ya Usuluhishi iliyokutana huko Dsm Tanzania ambaye mwenye nguvu ya ushawishi ya kuweza kusitisha Mgogoro huo, they do not have a moral authority ya kuweza kutatua tatizo hili. Kila mmoja ambaye yupo kwenye Kamati hiyo nchini mwake ana makandokando yake ya kuwepo kwa migogoro sawa na hiyo iliyopo huko Goma na Bukavu, DRC.

Doctrine of equity states that "he who goes for equity must go with clean hands."

Kati ya hao Viongozi waliohudhuria huko Dsm kwenye mkutano huo wa utatuzi wa Mgogoro huo, Je, nani ana mikono misafi?
 
Aondoe vikosi vyake ambavyo havijaalikwa DRC
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…