Kagera: Familia yadai ndugu yao kuuawa, Polisi wakanusha

Kagera: Familia yadai ndugu yao kuuawa, Polisi wakanusha

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Jeshi la Polisi Mkoani Kagera limesema kuwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Byamtemba, Kata ya Nsunga Wilayani Missenyi Mkoani Kagera, Jonathan Bunyaga alipata ajali na hajauawa na watu wasiojulikana kama inavyoelezwa.

Mwili wa Jonathan uliokotwa ukiwa umetelekezwa kando ya barabara inayotoka Bukoba kuelekea Mtukula mpakani mwa Tanzania na Uganda, Julai 30, 2022.

Familia ya Mwenyekiti huyo imeeleza kusikitishwa na kifo cha ndugu yao ambaye wanadai aliuawa na watu wasiojulikana na kisha mwili wake kutelekezwa kando kando mwa barabara.

Ndugu hao wanasdema ndugu yao alipigiwa simu saa tatu usiku na kuondoka akiwa na pikipipiki ambapo hakurudi nyumbani hadi walipopigiwa simu baada ya mwili wake kuonekana kandokando mwa barabara, na kwamba walipofika eneo la tukio walikuta marehemu amevaa kiatu kimoja huku kiatu kingine kikiokotwa sehemu nyingine kwenye shamba la miti ambako pia kulionekana kuwa na damu.

Aidha wanafamilia hao wamedai kuwa wakati wa kuosha mwili huo walibaini kuwepo kwa majeraha shingoni na sehemu nyingine za mwili yaliyoonesha kama amechomwa kwa kitu chenye ncha kali.

Mkuu wa Wilaya ya Missenyi Kanali Wilson Sakulo amekiri kuwepo kwa kifo hicho lakini akadai chanzo chake bado hakijafahamika na polisi wanaendelea na uchunguzi.

"Ni kweli kuna tukio la kifo cha Mwenyekiti wa Kijiji cha Byamtemba lakini chanzo cha kifo chake mimi kama Mkuu wa wilaya sifahamu, polisi wanaendelea na uchunguzi ili kubaini chanzo" amesema mkuu wa wilaya.

Akizungumza kwa njia ya simu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, William Mwampaghale amesema kuwa mwenyekiti huyo alipata ajali ya pikipiki. "Haijajulikana kama yeye ndiye aligonga au aligongwa, lakini mhusika mwingine katika ajali hiyo alikimbia baada ya tukio.

"Hiyo ndiyo taarifa rasmi ya Polisi, kama kuna watu wengine wanasema ameuawa hizo taarifa hatuna na si za kweli," anasema RPC Mwampaghale.

Source: EATV
 
Jeshi la Polisi Mkoani Kagera limesema kuwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Byamtemba, Kata ya Nsunga Wilayani Missenyi Mkoani Kagera, Jonathan Bunyaga alipata ajali na hajauawa na watu wasiojulikana kama inavyoelezwa.

Mwili wa Jonathan uliokotwa ukiwa umetelekezwa kando ya barabara inayotoka Bukoba kuelekea Mtukula mpakani mwa Tanzania na Uganda, Julai 30, 2022.

Familia ya Mwenyekiti huyo imeeleza kusikitishwa na kifo cha ndugu yao ambaye wanadai aliuawa na watu wasiojulikana na kisha mwili wake kutelekezwa kando kando mwa barabara.

Ndugu hao wanasdema ndugu yao alipigiwa simu saa tatu usiku na kuondoka akiwa na pikipipiki ambapo hakurudi nyumbani hadi walipopigiwa simu baada ya mwili wake kuonekana kandokando mwa barabara, na kwamba walipofika eneo la tukio walikuta marehemu amevaa kiatu kimoja huku kiatu kingine kikiokotwa sehemu nyingine kwenye shamba la miti ambako pia kulionekana kuwa na damu.

Aidha wanafamilia hao wamedai kuwa wakati wa kuosha mwili huo walibaini kuwepo kwa majeraha shingoni na sehemu nyingine za mwili yaliyoonesha kama amechomwa kwa kitu chenye ncha kali.

Mkuu wa Wilaya ya Missenyi Kanali Wilson Sakulo amekiri kuwepo kwa kifo hicho lakini akadai chanzo chake bado hakijafahamika na polisi wanaendelea na uchunguzi.

"Ni kweli kuna tukio la kifo cha Mwenyekiti wa Kijiji cha Byamtemba lakini chanzo cha kifo chake mimi kama Mkuu wa wilaya sifahamu, polisi wanaendelea na uchunguzi ili kubaini chanzo" amesema mkuu wa wilaya.

Akizungumza kwa njia ya simu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, William Mwampaghale amesema kuwa mwenyekiti huyo alipata ajali ya pikipiki. "Haijajulikana kama yeye ndiye aligonga au aligongwa, lakini mhusika mwingine katika ajali hiyo alikimbia baada ya tukio.

"Hiyo ndiyo taarifa rasmi ya Polisi, kama kuna watu wengine wanasema ameuawa hizo taarifa hatuna na si za kweli," anasema RPC Mwampaghale.

Source: EATV
 
Sijawahi kuwaamini polisi japo kuna wengine ni waungwana sana.Hata nikipishana nao njiani au benki nikiona wamebeba bunduki huwa napita mbali sana nahisi kama anaweza kufyatua risasi hivi.
 
Polisi wanadanganya.
Pikipiki ya marehemu ilikutwa imefichwa porini zaidi ya mita 400 kutoka eneo la ajali ikiwa nzima kabisa bila alama zozote za kuhusika na ajali.

Marehemu alikutwa amekalishwa pembezoni mwa barabara huku katikati ya barabara kukiwa na michirizi ya damu nyingi na vipande vya taa ya pikipiki na klachi ya pikipiki lakini hakukuwa na pikipiki yoyote.
Ndani ya shamba mbali kidogo ya eneo la tukio,zaidi ya mita 15 paliokotwa kiatu cha marehemu kikiwa na damu.

Eneo la tukio pia paliokotwa kandambili za watu wawili tofauti.


Mazingira hayo hayawezi kuwa ajali bali mauaji yaliyotekelezwa ndani ya shamba kisha maiti akaletwa barabarani ikatengenezwa sura ya ajali.

Iundwe timu huru ya uchunguzi maana wauaji tayari wanafahamika.
 
Aisee!?
Polisi wanadanganya.
Pikipiki ya marehemu ilikutwa imefichwa porini zaidi ya mita 400 kutoka eneo la ajali ikiwa nzima kabisa bila alama zozote za kuhusika na ajali.

Marehemu alikutwa amekalishwa pembezoni mwa barabara huku katikati ya barabara kukiwa na michirizi ya damu nyingi na vipande vya taa ya pikipiki na klachi ya pikipiki lakini hakukuwa na pikipiki yoyote.
Ndani ya shamba mbali kidogo ya eneo la tukio,zaidi ya mita 15 paliokotwa kiatu cha marehemu kikiwa na damu.

Eneo la tukio pia paliokotwa kandambili za watu wawili tofauti.


Mazingira hayo hayawezi kuwa ajali bali mauaji yaliyotekelezwa ndani ya shamba kisha maiti akaletwa barabarani ikatengenezwa sura ya ajali.

Iundwe timu huru ya uchunguzi maana wauaji tayari wanafahamika.
Hao ndio police wetu. Kwaiyo hapo wanamaanisha waliomgonga ndio walificha pikipiki yake?
 
Jeshi la Polisi Mkoani Kagera limesema kuwa aliyekuwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Byamtemba, Kata ya Nsunga Wilayani Missenyi Mkoani Kagera, Jonathan Bunyaga alipata ajali na hajauawa na watu wasiojulikana kama inavyoelezwa.

Mwili wa Jonathan uliokotwa ukiwa umetelekezwa kando ya barabara inayotoka Bukoba kuelekea Mtukula mpakani mwa Tanzania na Uganda, Julai 30, 2022.

Familia ya Mwenyekiti huyo imeeleza kusikitishwa na kifo cha ndugu yao ambaye wanadai aliuawa na watu wasiojulikana na kisha mwili wake kutelekezwa kando kando mwa barabara.

Ndugu hao wanasdema ndugu yao alipigiwa simu saa tatu usiku na kuondoka akiwa na pikipipiki ambapo hakurudi nyumbani hadi walipopigiwa simu baada ya mwili wake kuonekana kandokando mwa barabara, na kwamba walipofika eneo la tukio walikuta marehemu amevaa kiatu kimoja huku kiatu kingine kikiokotwa sehemu nyingine kwenye shamba la miti ambako pia kulionekana kuwa na damu.

Aidha wanafamilia hao wamedai kuwa wakati wa kuosha mwili huo walibaini kuwepo kwa majeraha shingoni na sehemu nyingine za mwili yaliyoonesha kama amechomwa kwa kitu chenye ncha kali.

Mkuu wa Wilaya ya Missenyi Kanali Wilson Sakulo amekiri kuwepo kwa kifo hicho lakini akadai chanzo chake bado hakijafahamika na polisi wanaendelea na uchunguzi.

"Ni kweli kuna tukio la kifo cha Mwenyekiti wa Kijiji cha Byamtemba lakini chanzo cha kifo chake mimi kama Mkuu wa wilaya sifahamu, polisi wanaendelea na uchunguzi ili kubaini chanzo" amesema mkuu wa wilaya.

Akizungumza kwa njia ya simu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, William Mwampaghale amesema kuwa mwenyekiti huyo alipata ajali ya pikipiki. "Haijajulikana kama yeye ndiye aligonga au aligongwa, lakini mhusika mwingine katika ajali hiyo alikimbia baada ya tukio.

"Hiyo ndiyo taarifa rasmi ya Polisi, kama kuna watu wengine wanasema ameuawa hizo taarifa hatuna na si za kweli," anasema RPC Mwampaghale.

Source: EATV
TAARIFA YA POLICE HATA SIIELEWI NA MIMI
 
Back
Top Bottom