Kahama VS Njombe/Mafinga

Soko la mazao makambako lenye ekari za kutosha ujenzi bado unaendelea
 

MRADI WA UCHIMBAJI CHUMA WATAMBULISHWA WILAYANI MAKETE​

Tarehe Iliyowekwa: March 5th, 2024
Kampuni ya Uchimbaji wa Chuma Fujian Hexingwang imetambulisha mradi wa Uchimbaji wa Mawe katika Kijiji cha Ipepo Kata ya Ipepo Wilayani Makete Mkoani Njombe.

Mradi huo umetambulishwa leo tarehe 5 Machi, 2024 kwa Wananchi wa Kijiji hicho mbele ya Viongozi mbalimbali ngazi ya Wilaya ya Makete akiwepo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji (W) ambaye ni Afisa Maendeleo ya Jamii Bi. Jackline Mrosso , Watalaamu ngazi ya Wilaya na Diwani Kata ya Ipepoo Mhe. Manase Nyaulawa.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji (W) ambaye ni Afisa Maendeleo ya Jamii Bi. Jackline Mrosso amesema ujio wa Mradi huo mkubwa wa Uchimbaji wa Chuma ni fursa kubwa ya Ajira na kukuza uchumi wa Wananchi Wilayani Makete na Tanzania kwa ujumla.

Naye, Mkurugenzi wa Kampuni ya Fujan Fujian Hexingwang, Bwana Xu Xing Da amesema Mazingira mazuri ya Uwekezaji Wilayani Makete, yamepelekea kampuni hiyo, kujikita Wilayani humo sambamba na Usimamizi mzuri wa Serikali ya Awamu ya 6 chini ya Rais Samia Suluhu Hassan.

Kwa Upande wake, Diwani wa Kata ya Ipepo Mhe. Manase Nyaulawa amewashukuru wawekezaji hao kwa kuamua kuwekeza katika kata hiyo na kuwaomba kushirikiana na Wananchi wa Kijiji hicho katika kazi mbalimbali za Maendeleo.

Wananchi wa Kijiji cha Ipepo wamewakaribisha wawekezaji hao na kuwaahidi kutoa ushirikiano wakati wote na kuomba kupewa kipaumbele kwenye masuala ya Ajira pindi mradi utakapoanza kutekelezwa.
 
UWANJA WA NDEGE NDANI YA HIFADHI YA RUAHA WAZINDULIWA MBEYA

Serikali Kwa kushirikiana na wawekezaji kutoka taasisi ya Six Rivers Africa wamezindua uwanja wa ndege wenye urefu wa kilomita 1.2 ndani ya hifadhi ya taifa ya Ruaha mkoani Mbeya, Kwa lengo la kukuza utalii Kwa ukanda wa kusini, kupitia watalii kutoka maeneo mbalimbali duniani kutua kwenye uwanja huo na kutembelea vivutio Kwenye hifadhi za taifa.

Kamishna msaidizi mwandamizi wa uhifadhi Godwill Ole Meng'ataki ni mkuu wa hifadhi ya taifa ya Ruaha, anasema uwanja huo mdogo ndani ya hifadhi umekwisha sajiliwa katika mamlaka za usimamizi wa viwanja vya ndege Tanzania na tayari wamepokea maombi mbalimbali ya watalii kuanza kutua kwenye uwanja huo na kutembelea hifadhi za Taifa pamoja na vivutio vilivyopo maeneo ya ukanda wa kusini.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Taasisi ya Six Rivers Africa Glenn Turner, ameipongeza serikali ya Tanzania Kwa kutenga eneo kubwa zaidi kuliko Nchi yeyote duniani ambalo limehifadhiwa, huku kaimu Katibu tawala Mkoa wa Mbeya akiwaomba wahusika kuzingatia usalama wa watu wanaotumia uwanja huo pamoja na wanyama kwakua uwanja huo upo ndani ya hifadhi.

Akimwakilisha Katibu mkuu wa Wizara ya maliasiri na utalii, mkuu wa Wilaya ya Mbarali Kanali Denis Mwila, ametaka uwanja huo kutunzwa ili utumike Kama uwanja wa dhararu wa kutua ndege za abiria pindi zinapotokeza hitirafu mbalimbali.

Cc @enocksaimon
#WasafiDigital
 
Kumbe surfacing yake sio lami? Ule wa Nyerere NP una lami kabisa.
 
Mkoa wa njombe UNAKWENDA level zingine kitendo Cha kuwa mji wa viwanda na madini ya chuma ndo yanayo tegemewa zaidi kwenye shughuli nyingi unaenda kupindua meza kwenye GDP nk na walisha azimia viwanda kujengwa ndani ya mkoa wao vya kuchakata chuma na kazi imeanza mkoa wa njombe UNAKWENDA kuwa na mji mkubwa wa biashara na viwanda πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡"VIWANDA KUJENGWA NJOMBE KUCHAKATA MAKAA YA MAWE, MAKAA YA MAWE KUNUFAISHA WANANCHI - YouTube"
View: https://m.youtube.com/watch?v=ENuLDwmGtLc&pp=ygUYdml3YW5kYSB2eWEgY2h1bWEgbmpvbWJl
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…