Muongezee
Son of Gamba afanye refer za Baltic Crusade, Spanish invasion of South America, Crusades
Ndugu yangu nataka nikuambie kitu ukielewe vizuri.
Iko hivi :
Wakristo wa KWELI huwa hawabebi silaha wala hawajihusishi na vita ya kimwili ya aina yoyote ile. Mkristo wa KWELI haruhusiwi "kuua", tena siyo kuua tu hata kumtukana mtu au kumpiga mtu kibao ni sawa na dhambi ya kuua.
Hao waliokuwa wanajiita "crusaders" au wabeba misalaba kwa tafsiri rahisi ya kiswahili walikuwa sio Wakristo wa KWELI.
Sifa kuu za MKRISTO wa KWELI ni kuishi kwa kuzishika Amri za MUNGU na imani ya YESU KRISTO.
Hao "crusaders" ni zao la ukristo fake, yaani ukristo wa uongo ambao ni mchanganyiko wa mafundisho na desturi za "kipagani", vikachanganywa na Injili. Mchanganyiko huo ndio uliozaa "ukristo" mnaoujua ninyi leo hii. Ukristo unaopingana na Amri za MUNGU na imani ya YESU KRISTO.
Aina hii ya "ukristo fake" ilienezwa duniani kote na kanisa katoliki na mpaka leo hii ndio "ukristo" unaotambulika na watu wengi duniani.
Limebakia kundi dogo sana la watu wachache mno ambao bado wameushika UKRISTO wa KWELI mpaka leo na wataendelea kuushika UKRISTO huo wa KWELI mpaka ile siku atakaporudi tena BWANA YESU.
Hivyo basi naomba uelewe hao waliokuwa wakiitwa "crusaders" kiuhalisia sio WAKRISTO ingawa walijiita "wakristo". Matendo yao ya kujihusisha na vita, uuaji, utekaji nyara, ubakaji nk hayaendani kabisa na UKRISTO wa KWELI.
-Mkristo wa kweli hata ukimtukana hawezi kukurudishia tusi.
-Mkristo wa kweli ukimpiga hawezi kukurudishia.
-Mkristo wa kweli haendi vitani wala hapigani vita ya mwilini bali siku zote hueneza amani na kuhubiri amani kwa watu wote.
-Mkristo wa kweli huongozwa na upendo, haki, huruma, uvumilivu, heshima, adabu kwa watu wote, kiasi, ustahimilivu, upole na usafi wa moyo.
-Mkristo wa kweli hutoa alivyonavyo kwa ajili ya wengine na kamwe hawezi kuchukua vya wengine ili kujilimbikizia mali.
-Mkristo wa kweli hali kiapo cha aina yoyote ile wala haapi kabisa iwe ni kwa namna yoyote ile.
-Mkristo wa kweli haambatani na sanamu ya aina yoyote ile. Wala habebi msalaba wa aina yoyote ile.
-Mkristo wa kweli huzishika Amri zote za MUNGU na imani ya YESU KRISTO.
Mtu yeyote au kikundi chochote kile cha watu wanaojiita "wakristo" kama hawana hizo sifa hapo juu, hao siyo WAKRISTO. Crusaders hawakuwa WAKRISTO.