TANZIA Kaka yake na marehemu Michael Jackson aitwaye Tito Jackson amefariki duniani

TANZIA Kaka yake na marehemu Michael Jackson aitwaye Tito Jackson amefariki duniani

ukwaju_wa_ kitambo

Senior Member
Joined
Sep 15, 2024
Posts
150
Reaction score
173
images (20).jpg


Mwanamuziki Mkongwe wa kundi la Jackson 5 Tito Jackson (70) ambaye ni Kaka wa Marehemu Michael Jackson, amefariki dunia.

Siku chache kabla ya kifo chake, aliposti ujumbe akiwa nchini Ujerumani ambapo kundi lao lilitembelea eneo la kumbukumbu ya ndugu yao Michael.

Jackson 5 lilianzishwa mwaka 1964 likiwajumuisha Tito, Jackie, Jermaine, Marlon na Michael ambao ni ndugu.

Kundi hilo ambalo lilivuma sana miaka ya 60 na 70, chini ya uongozi wa baba yao marehemu Joe Jackson, limefanikiwa kuuza zaidi ya rekodi milioni 150 na kupokea tuzo mbalimbali.

Onyesho lao la mwisho wakiwa na Marehemu Tito lilikuwa tarehe 10 ya mwezi huu nchini Ujerumani,siku 5 kabla ya kifo chake kilichotokea nchini Marekani.

Ukwaju wa kitambo
0767542202
 
Poleni sana Jackson family and funs bas3 yoote
 
Back
Top Bottom