Kakonko, Ngara, na Biharamulo kataeni makao makuu ya mkoa kuwa Chato - Nyakanazi liwe pendekezo lenu

Kakonko, Ngara, na Biharamulo kataeni makao makuu ya mkoa kuwa Chato - Nyakanazi liwe pendekezo lenu

Kabende Msakila

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2020
Posts
1,809
Reaction score
1,692
MKOA MPYA NA MAKAO MAKUU MAPYA NYAKANAZI:
Anaandika Msakila M Kabende - Economist

KWA WAHESHIMIWA:-
(i). Aloyce Kamamba - Mbunge wa Jimbo la Buyungu
(ii). Ezra John Chiwelesa - Mbunge wa Jimbo la Biharamulo
(iii). Ndaisaba G. Luhoro - Mbunge wa Jimbo la Ngara
(iv). Fidel Chiza Nderego - Mwenyekiti wa H/W Kakonko
(v). Lushahu - Mwenyekiti wa H/W Biharamulo
(vi). Wilberd J Bambara - Mwenyekiti wa H/W Ngara.

YAH: PINGAMIZI LA MAKAO MAKUU YA MKOA MPYA WA CHATO KUWA CHATO

Kwanza, niwapongeze sana kwa kuendelea kutumikia wananchi wenu ktk majimbo yenu na halmashauri zenu kwa uadilifu na uaminifu.

Pili, niwaombe muunganishe nguvu zenu kukataa, kupinga na kutokuwa sehemu ya vikao vitakavyobariki ktk kuweka MAKAO makuu ya mkoa mpya wa Chato kuwa Chato. Hii ni kutokana na ukweli kwamba sisi wananchi tunaosogezewa huduma tutakuwa mbali na makao hayo makuu. Iwapo Serikali yetu ina dhamira njema i.e kuchochea maendeleo yetu, kupunguza adha kwa wananchi na ufanisi wa utoaji huduma kwa jamii basi tunapendekeza MAKAO makuu ya mkoa mpya yawekwe NYAKANAZI kwa kuwa:-

(a). Kakonko - Nyakanazi 45Kms
(b). Ngara - Nyakanazi 79Kms
(c). Biharamulo - Nyakanazi 45Kms
(d). Chato - Nyakanazi 113Km.

Sasa kwa ujumla makao makuu kuyaweka njia panda ya Nyakanazi itakuwa na tija kwa wilaya zetu zote kwa kuwa ipo katikati ya maeneo yote yanayounda mkoa mpya.

Nimewaandikia hili ili muunganishe nguvu za hoja hii ktk vikao vyote vya kisheria kama Regional Consultative Committee (RCC); District Consultative Committee (DCC); Regional Road Boards (RRB) na vikao vingine vingi.

Wananchi wa maeneo yote yanayounda mkoa mpya wa Chato tunamuunga mkono, na kumkumbuka Hayati Dkt John Pombe Magufuli lkn kumbukumbu zetu hatutaki zigeuke kero kwetu kwa kusafiri umbali mrefu kufuata huduma za kijamii na kiuchumi.

Naamini kwa umoja wetu Mungu atatuvusha katika kipindi hiki cha kupata mkoa mpya na makao mapya ya mkoa.

Mungu awabariki sana.

Msakila M Kabende
= Mgombea ubunge kura za maoni CCM jimbo la Buyungu 2010, 2015, 2018, na 2020.

= Mgombea Uenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa mwaka 2017.
 
Unapoteza muda mapendekezo yameshawasilishwa Tamisemi kwa hatua zaidi.
 
Mama samia akikubali tu kubariki maamuzi hayo, nitaanza harakati zakumpinga waziwazi. Chato ibaki kuwa wilaya tu. Wala haiana hata hadhi ya kuwa wailaya.ilililazimishwa tu na wanasiasa.
 
Mama samia akikubali tu kubariki maamuzi hayo, nitaanza harakati zakumpinga waziwazi. Chato ibaki kuwa wilaya tu. Wala haiana hata hadhi ya kuwa wailaya.ilililazimishwa tu na wanasiasa.
Jiandae kwa maumivu mkuu. Mkoa wa Chato umeshapita subiri siku ya kuzima Mwenge wa Uhuru tarehe 14/10/2021
 
14 Oct 2021 ndio siku maumivu kwacwakazi wengi wilaya pendwa kuvutwa kuundwa Mkoa wa Chato......tunasubiri kwa hamu yoooo
 
Ngara-Chato= Km!?
Biharamulo-Chato= Km!?
Kakonko-Chato= Km!?
Kwani mkuu uliwahi kusoma hesabu(samahani lakini) kwani swali ulilouliza hata mtoto wa darasa la tatu anaweza akalijibu!!kutokana na data hizo ulizopewa hapo juu, kama katikati ni NYAKANAZI, na umbali wa kutoka sehemu hizo hadi nyakanazi umepewa, kweli umbali wa kutoka chato hadi ngara huwezi upata hapo?!!daaa kazi kweli kweli
 
CHATO NI MKOA na makao makuu ni CHATO! ... PERIOD!

1622394375442.png
 
Unahisi huo umbali ambao yeye kauandika kwenye andiko lake ningetaka kuupata bila yeye kuuandika nisingeweza kuupata!?

Ukionyesha kwamba kutoka A kwenda C ni karibu kwa km/mile/m kadhaa kisha ukasema kutoka A kwenda H ni mbali pasipo kuonyesha kama ulivyoonyesha mwanzo ukiwaza kuwa msomaji atajiongeza nadhani,kwa mawazo yangu si njia bora sana.
Kwani mkuu uliwahi kusoma hesabu(samahani lakini) kwani swali ulilouliza hata mtoto wa darasa la tatu anaweza akalijibu!!kutokana na data hizo ulizopewa hapo juu, kama katikati ni NYAKANAZI, na umbali wa kutoka sehemu hizo hadi nyakanazi umepewa, kweli umbali wa kutoka chato hadi ngara huwezi upata hapo?!!daaa kazi kweli kweli
 
MKOA MPYA NA MAKAO MAKUU MAPYA NYAKANAZI:
Anaandika Msakila M Kabende - Economist

KWA WAHESHIMIWA:-
(i). Aloyce Kamamba - Mbunge wa Jimbo la Buyungu
(ii). Ezra John Chiwelesa - Mbunge wa Jimbo la Biharamulo
(iii). Ndaisaba G. Luhoro - Mbunge wa Jimbo la Ngara
(iv). Fidel Chiza Nderego - Mwenyekiti wa H/W Kakonko
(v). Lushahu - Mwenyekiti wa H/W Biharamulo
(vi). Wilberd J Bambara - Mwenyekiti wa H/W Ngara.

YAH: PINGAMIZI LA MAKAO MAKUU YA MKOA MPYA WA CHATO KUWA CHATO

Kwanza, niwapongeze sana kwa kuendelea kutumikia wananchi wenu ktk majimbo yenu na halmashauri zenu kwa uadilifu na uaminifu.

Pili, niwaombe muunganishe nguvu zenu kukataa, kupinga na kutokuwa sehemu ya vikao vitakavyobariki ktk kuweka MAKAO makuu ya mkoa mpya wa Chato kuwa Chato. Hii ni kutokana na ukweli kwamba sisi wananchi tunaosogezewa huduma tutakuwa mbali na makao hayo makuu. Iwapo Serikali yetu ina dhamira njema i.e kuchochea maendeleo yetu, kupunguza adha kwa wananchi na ufanisi wa utoaji huduma kwa jamii basi tunapendekeza MAKAO makuu ya mkoa mpya yawekwe NYAKANAZI kwa kuwa:-

(a). Kakonko - Nyakanazi 45Kms
(b). Ngara - Nyakanazi 79Kms
(c). Biharamulo - Nyakanazi 45Kms
(d). Chato - Nyakanazi 113Km.

Sasa kwa ujumla makao makuu kuyaweka njia panda ya Nyakanazi itakuwa na tija kwa wilaya zetu zote kwa kuwa ipo katikati ya maeneo yote yanayounda mkoa mpya.

Nimewaandikia hili ili muunganishe nguvu za hoja hii ktk vikao vyote vya kisheria kama Regional Consultative Committee (RCC); District Consultative Committee (DCC); Regional Road Boards (RRB) na vikao vingine vingi.

Wananchi wa maeneo yote yanayounda mkoa mpya wa Chato tunamuunga mkono, na kumkumbuka Hayati Dkt John Pombe Magufuli lkn kumbukumbu zetu hatutaki zigeuke kero kwetu kwa kusafiri umbali mrefu kufuata huduma za kijamii na kiuchumi.

Naamini kwa umoja wetu Mungu atatuvusha katika kipindi hiki cha kupata mkoa mpya na makao mapya ya mkoa.

Mungu awabariki sana.

Msakila M Kabende
= Mgombea ubunge kura za maoni CCM jimbo la Buyungu 2010, 2015, 2018, na 2020.

= Mgombea Uenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa mwaka 2017.
Mimi naona Buseresere au Bwanga ni sahihi zaidi
 
Kwa maoni yangu hata mkoa ukiwa nyakanazi bado haitakuwa na tija yoyote , kwa sababu mkoa huo ulianzishwa kwa hila nyingi huku zikifanyika hila za kudidimiza wilaya za jirani kimaemdelleo kuipandisha moja ( chato ) na hizohizo ndio mnataka ziungane hiyo si sawa.

lakini mkumbuke CHATO Ilikuwa ni kijiji ndani ya BIHARAMULO wilaya kongwe ni BIHARAMULO katika ukanda huo na BIHARAMULO ndio ilizaa ngara nayo ni kongwe pia hata serikai ya kikoloni makao yake yalikuwa Biharamulo kama kuna nia safi mkoa mpya uitwe mkoa wa biharamulo kwani BIHARAMULO Ni maarufu zaidi ya CHATO ila zimekuwa zikifanyika hujuma za makusudi kuipandiaha CHATO na kuidunisha BIHARAMULO , mbuga ya Burigi ipo wilaya ya BIHARAMULO kwa asilimia 100 na biharamulo game reserve ipo biharamulo kwa asilimia zaidi ya 90 lakini yaliyofanyika kila mtu anayajua mbuga badala ya kuitwa Burigi BIHARAMULO majina Ambayo yalikuwepo tayari yakitumika ikaitwa Burigi CHATO . Kifupi CHATO ina vigezo vya kuokoteza tuu na ndio maana inahitaji kukopa maeneo mengine .


kwanini Serikali isiangalie mikoa mikubwa kama ya Tabora Morogoro etc ambayo yenyewe yanajitosheleza kutengeneza mkoa mwingine ndani yake bila hata kuazima maeneo na inakidhi vigezo vyote na kuna mahitaji ya kufanya hivyo?

Hakuna eneo lolote la mkoa wa kagera ambalo linazidi masaa zaidi ya sita kufika makao makuu ya mkoa.

na iwapo mkoa utapitishwa basi ingependeza uitwe mkoa wa BIHARAMULO sbb BIHARAMULO ni kubwa kuliko chato kihistoria. Tuwaheshimu watu wa biharamulo na ngara na kulinda historia yao ktk ujenzi wa Taifa hili wakati huo Chato ikiwa ni kijiji tu.
 
MKOA MPYA NA MAKAO MAKUU MAPYA NYAKANAZI:
Anaandika Msakila M Kabende - Economist

KWA WAHESHIMIWA:-
(i). Aloyce Kamamba - Mbunge wa Jimbo la Buyungu
(ii). Ezra John Chiwelesa - Mbunge wa Jimbo la Biharamulo
(iii). Ndaisaba G. Luhoro - Mbunge wa Jimbo la Ngara
(iv). Fidel Chiza Nderego - Mwenyekiti wa H/W Kakonko
(v). Lushahu - Mwenyekiti wa H/W Biharamulo
(vi). Wilberd J Bambara - Mwenyekiti wa H/W Ngara.

YAH: PINGAMIZI LA MAKAO MAKUU YA MKOA MPYA WA CHATO KUWA CHATO

Kwanza, niwapongeze sana kwa kuendelea kutumikia wananchi wenu ktk majimbo yenu na halmashauri zenu kwa uadilifu na uaminifu.

Pili, niwaombe muunganishe nguvu zenu kukataa, kupinga na kutokuwa sehemu ya vikao vitakavyobariki ktk kuweka MAKAO makuu ya mkoa mpya wa Chato kuwa Chato. Hii ni kutokana na ukweli kwamba sisi wananchi tunaosogezewa huduma tutakuwa mbali na makao hayo makuu. Iwapo Serikali yetu ina dhamira njema i.e kuchochea maendeleo yetu, kupunguza adha kwa wananchi na ufanisi wa utoaji huduma kwa jamii basi tunapendekeza MAKAO makuu ya mkoa mpya yawekwe NYAKANAZI kwa kuwa:-

(a). Kakonko - Nyakanazi 45Kms
(b). Ngara - Nyakanazi 79Kms
(c). Biharamulo - Nyakanazi 45Kms
(d). Chato - Nyakanazi 113Km.

Sasa kwa ujumla makao makuu kuyaweka njia panda ya Nyakanazi itakuwa na tija kwa wilaya zetu zote kwa kuwa ipo katikati ya maeneo yote yanayounda mkoa mpya.

Nimewaandikia hili ili muunganishe nguvu za hoja hii ktk vikao vyote vya kisheria kama Regional Consultative Committee (RCC); District Consultative Committee (DCC); Regional Road Boards (RRB) na vikao vingine vingi.

Wananchi wa maeneo yote yanayounda mkoa mpya wa Chato tunamuunga mkono, na kumkumbuka Hayati Dkt John Pombe Magufuli lkn kumbukumbu zetu hatutaki zigeuke kero kwetu kwa kusafiri umbali mrefu kufuata huduma za kijamii na kiuchumi.

Naamini kwa umoja wetu Mungu atatuvusha katika kipindi hiki cha kupata mkoa mpya na makao mapya ya mkoa.

Mungu awabariki sana.

Msakila M Kabende
= Mgombea ubunge kura za maoni CCM jimbo la Buyungu 2010, 2015, 2018, na 2020.

= Mgombea Uenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Taifa mwaka 2017.
Miaka yote unagombea hujawahi hata kuwa diwani? aibu yako
 
Kwa maoni yangu hata mkoa ukiwa nyakanazi bado haitakuwa na tija yoyote , kwa sababu mkoa huo ulianzishwa kwa hila nyingi huku zikifanyika hila za kudidimiza wilaya za jirani kimaemdelleo kuipandisha moja ( chato ) na hizohizo ndio mnataka ziungane hiyo si sawa.

lakini mkumbuke CHATO Ilikuwa ni kijiji ndani ya BIHARAMULO wilaya kongwe ni BIHARAMULO katika ukanda huo na BIHARAMULO ndio ilizaa ngara nayo ni kongwe pia hata serikai ya kikoloni makao yake yalikuwa buharamulo kama kuna nia safi mkoa mpya uitwe mkoa wa biharamulo kwani BIHARAMULO Ni maarufu zaidi ya CHATO ila zimekuwa zikifanyika hujuma za makusudi kuipandiaha CHATO na kuidunisha BIHARAMULO , mbuga ya Burigi ipo wilaya ya BIHARAMULO kwa asilimia 100 na biharamulo game reserve ipo biharamulo kwa asilimia zaidi ya 90 lakini yaliyofanyika kila mtu anayajua mbuga badala ya kuitwa Burigi BIHARAMULO kama kulikuwa na Nina Safi majina Ambayo yalikuwepo tayari ikaitwa Burigi CHATO . Kifupi CHATO ina vigezo vya kuokoteza tuu na ndio maana inahitaji kukopa maeneo mengine .


kwanini Serikali isiangalie mikoa mikubwa kama ya Tabora Morogoro etc ambayo yenyewe yanajitosherleza kutengeneza mikoa mwingine ndani yake bila hata kuazima maeneo na i Alison vigezo vyote na kuna mahitaji ya kufanya hivyo?

Hakuna eneo lolote la mkoa wa kagera ambalo linazidi masaa zaidi ya sita kufika makao makuu ya mkoa.

na iwapo mkoa utapitishwa uitwa mkoa wa BIHARAMULO sbb BIHARAMULO ni kubwa kuliko chato kihistoria. Tuwaheshimu watu wa biharamulo na ngara na kulinda historia yao ktk ujenzi wa Taifa hili wakati huo Chato ikiwa ni kijiji tu.
Option ya pili mkoa wa geita ubadili jina uitwe chato ili wafurahu
 
Poleni sana, wakitaka lao lazima litimie...
 
Kwani mkuu uliwahi kusoma hesabu(samahani lakini) kwani swali ulilouliza hata mtoto wa darasa la tatu anaweza akalijibu!!kutokana na data hizo ulizopewa hapo juu, kama katikati ni NYAKANAZI, na umbali wa kutoka sehemu hizo hadi nyakanazi umepewa, kweli umbali wa kutoka chato hadi ngara huwezi upata hapo?!!daaa kazi kweli kweli
Ungekuwa umejibu swali vizuri kwa kutoa ufafanuzi kuliko kutoa dharau. Kwa wewe unayejua hesabu, unaweza kutuambia kuwa kati ya mji P na Q ni upi una optimal distances kutoka miji A, B na C? Hafalu pia semea je density kubwa ya watu iko wapi?
1622593595053.png
 
Back
Top Bottom