Kakosa Mume wa ndoto yake: Mdogo wangu wa mwisho kakosa mume kisa ana mtoto

Husiishie kwenye kuwaombea wambie ukweli,yaani yale makavu, japo mabinti wengi hawasikii kabisa mpaka siku wayakute.

Yaani number ya mabinti Masingle mother ambao hawajavuka 20+ inakuwa kwa kasi.Kuna vibinti vinne navijua vya juzi watatu wamezaa na waume za watu,tena mmoja kashika mimba kipindi akisubiri matokeo ya form four na mwengine kazaa na muhuni,yaani unawatizama mpaka huruma.
 
Ebu kuleni hiki chuma kwanza, wewe na mdogo wako Ushuhuda mwanaume mwenzenu: Nilioa Single Mother yalioyonikuta ni haya. Nilichukua uamuzi huu...
 
I feel your concern. Changamoto ni nyingi sana kwa haya mambo.
 
Uzuri unaouongelea wewe unaweza kuwa tofauti na uzuri anaouna mwanaume kumfanya mwanamke kuwa mke.
 
Alaaniwe yule mshamba aliyemzalisha huyo binti na kuenda kuoa mwingine.

Dunia ndogo atakuja kulipia hii.
Bora wewe unayetulaani sisi wazalishaji kuliko anayelaani wanaokataa kubeba mizigo ya wengine.
Hizu nguvu na kampeni wanazozitumia kushawishi watu waoe wanawake waliozalishwa na kuwaponda wanaokataa ni vyema wangezitumia kushawishi wazalishaji wawarudie wanawake zao.
We mtu ameshazalishwa na aliyemzalisha kakwepa kuwwka ndani na kutafuta mwingine, halafu mtu anakuja jitia kuherehere kujifanya yeye ataweza.
Wawarudie hao waliowazalisha wawashawishi waone kama ni inawezekana.
 
Sijui nipo off topic , hivi kwanini watoto tuseme wanne waliozaliwa na baba tofauti ila mama ni mmoja ,Huwa hakuna ile family bond , yaani ule upendo baina ya ndugu na ndugu?[emoji848]
Haupo off topic.
Mama wa aina hiyo ana kipi cha kuwaambia watoto wake when it comes to Malezi?
Maana ni either ana akili finyu ya kutoweza kufanya chagua sahihi au hana uwezo wa kutunza na kulinda mahusiano hivyo hawezi akawa na uwezo wa kuwalea watoto kimaadili, japo hii siyo formula ila ni muhimu kwenye maangalizo.
 
Noma sana!kikubwa mchukue mtoto.huyo binti alikua kilaza
 
Angalia tamaa zitakuponza kumbe mmetamani mali zajamaa PAMBANA upate zako kwani ww mlemavu
 
Mwanamke akishaa zaa na mtu akikisha unaliona kaburi la uyo boy aliezaa nae lasivo asikudanganye sabbu ataukikuta wanaongea atakwambia wanaongea kuusu mtoto wao soma uzi kibao za singo maza walio olewa uone majanga yao
 
Wale waliozalishwa na wakaamua kutulia na kuendelea na maisha yao unadhani tuna noma nao basi? Wale wala hatuna noma nao kabisa, ni wenzetu na tunawapenda na kuwaheshimu sana.
Noma ni wale magumegume wanaoanza kujihesabia haki sawa na wengine, kulazimisha ndoa wakati tayari ni mzazi mwenza wa mtu.

Mtu ameshafikia level kawa mzazi atulie aendelee na maisha badala ya kung'ang'aniza mahusiano ya kuelekea ndoani, kama anataka ndoa arudi akamlazimishe aliyemzalisha.

Hao ambao bado, wasimamieni vizuri katika maadili na namna ya kuyashinda majaribu wasije wakavunjikia walipovunjika wenzao
 
Nakuelewa rafiki, najitahidi sana na Mungu awasaidie.

Hivi hao mabinti wazazi na walezi wao wana mtazamo gani juu ya hiko kinachoendelea?
 
Legezeni masharti mtatuua.....iwe tu hakuna mawasiliano basi walau
Mimi nikikuzalisha labda uniachie mtoto, kinyume na hapo lazima kila wiki nikupigie wewe au mume wako mnipe maendeleo ya mtoto wangu na niwapatie maelekezo ya namna ya kumlea.
Lakini ukiniachia mtoto wala sitakua na issue na wewe, na wala hautatusikia popote pale. Zaidi nitakutakia maisha mema.
 
Mimi binafsi siwezi oa single mother. Lakini sioni shida na mtu kuoa single mother. Changamoto kubwa kwa mwanaume kuona single mothers ni kutoka kwa familia. Familia nyingi haziwezi kuelewa swala la kijana wao kuoa single mother wakati Kuna mabinti ambao hawana watoto especially pale ambapo yeye Hana Bado watoto. Wanaume tunataka mwanamke awe pure, ata kama kaliwa Sasa isiwe kaliwa mbaka akazaa na mtoto. Cha msingi single mothers tafuteni wanaume watu wazima wenye watoto pia mfanye maisha.
 
Nakuelewa rafiki, najitahidi sana na Mungu awasaidie.

Hivi hao mabinti wazazi na walezi wao wana mtazamo gani juu ya hiko kinachoendelea?
Wazazi nao changamoto, kama huyo binti wa form 4 mother yake nae ni single mother,hao wengine watatu bado wapo kwa wazazi wao na watoto zao.

Ila mabinti wengi wanaangukia kwa waume za watu sababu ya tamaa ya fedha, so ukifanikiwa kumjenga binti yako kisaikolojia kwamba fedha si kila kitu,mfundishe ajue thamani ya maisha yake,thamani ya uzuri/usichana wake,thamani ya utu zidi ya fedha na awe na hofu ya Mungu utakuwa umemsaidia,kwani atakuwa na uwezo wa jinsi ya kujilinda zidi ya mimba zisizo tarajiwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…