Kala Pina na Fid Q Nani Zaidi

Kala Pina na Fid Q Nani Zaidi

fredito13

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2012
Posts
213
Reaction score
146
Kuna baadhi ya wasanii wa 'hip hop' ambao wamekuwa wakijiita ni 'bora zaidi' na wao wanafaham misingi ya Hip Hop! Kati ya wasanii wanaojiita hivyo ni Kalapina na kundi lake la kikosi cha mizinga!
Kwa upande mwingine kuna wale wasiozungumza, lakini sanaa yao inakubalika zaidi kwa mashabiki! Upande huu unaongozwa na Fid Q - Ngosha the Don a.k.a Jeshi la mtu mmoja

Kati ya Fid Q na Kalapina (Kikosi cha Mizinga) ni nani anayefanya hip hop ya kweli (zingatia ujumbe, beat, sauti na miondoko)

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
kubanda anatisha mzee usimlinganisha zitto na ben saanane
 
kubanda anatisha mzee usimlinganisha zitto na ben saanane
Nimeuliza swali hili nikiwa nimeficha hisia zangu ili kutoharibu maana halisi ya swali kwa ku-influence majibu.


Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Hakuna MC hapo! Watoto mlioanza kusikiliza muziki juzi ndio kauli zenu hizi.
FID Q asili ya style yake ni Mapacha (maujanja supplier) na ni bingwa wa kucopy hadi mistari.
Ipo siku sanaa itarudi kwa wenyewe kama enzi zile!
 
Unafunga nguvu kwa vyuma ku-rap we goi goi-Fid Q
 
Hakuna MC hapo! Watoto mlioanza kusikiliza muziki juzi ndio kauli zenu hizi.
FID Q asili ya style yake ni Mapacha (maujanja supplier) na ni bingwa wa kucopy hadi mistari.
Ipo siku sanaa itarudi kwa wenyewe kama enzi zile!

Unaposema ka-copy mistari unatakiwa useme ni mistari ipi na style ya mapacha na Fid ni tofauti kabisa...
 
Hiphop ni (movement) harakati zilizobeba maarifa, hiphop ni jinsi unavyoishi, na rap ni kile unachofanya, utamaduni wa hiphop umeshikiriwa na nguzo muhimu nne 1.Uchenguaji (Emceeing), uchezeaji santuri (Deejaying), kuvunja (break dancing) na uchoraji machata (graffiti).

KRS One akitoa Darsa katika chuo kikuu cha Harvad, anasema zimefika element 9, zilizoongezeka ni 5. Beat Boxing, 6.Street fashion (Mitindo ya mavazi ya mtaa) 7. Street language (lugha za mtaani, jamii ya wana hip hop), 8. Street Knowledge (Elimu ya mtaani) na hapa alitoa mfano wa slogan ya NO JUSTICE NO PEACE imetoka mtaani. 9. Street Entrepreneurialism (Ujasiliamali wa mtaani).
Ukiangalia maelezo yangu kwa ufupi ni dhahiri utapata majibu ya nani mkali kati ya Fid Q na Kala Pina. Kwa ufupi wote wako katika same movement na wanaishi katika utamaduni mmoja isipokua wanazidiana katika vitu vichache. Fid anamzidi Kalapina katika Nguzo ya saba yaani lugha za mtaani hasa katika kuandika na uchenguaji pia yuko vizuri. Kala Pina nae yuko vizuri katika kuandika lakini sio mzuri katika street language.
Katika harakati hizi naweza pia kusema Kalapina amekua imara kwa muda mrefu na hasa katika kusimamia na kuhakikisha misingi ya utamaduni wa hiphop inafuatwa tofauti na Emcees wengine!
Sasa wewe utaamua nani zaidi…Mimi nimewasilisha tu baadhi ya tofauti kwa uelewa wangu!
Pina.jpgfid.jpg
 
Unaposema ka-copy mistari unatakiwa useme ni mistari ipi na style ya mapacha na Fid ni tofauti kabisa...

Nitakuwa najaza server za JF tu bure mkuu wangu tumeshajadili sana hawa wasanii kitambo pekenyua humu utapata kila kitu.
 
Hiphop ni (movement) harakati zilizobeba maarifa, hiphop ni jinsi unavyoishi, na rap ni kile unachofanya, utamaduni wa hiphop umeshikiriwa na nguzo muhimu nne 1.Uchenguaji (Emceeing), uchezeaji santuri (Deejaying), kuvunja (break dancing) na uchoraji machata (graffiti).

KRS One akitoa Darsa katika chuo kikuu cha Harvad, anasema zimefika element 9, zilizoongezeka ni 5. Beat Boxing, 6.Street fashion (Mitindo ya mavazi ya mtaa) 7. Street language (lugha za mtaani, jamii ya wana hip hop), 8. Street Knowledge (Elimu ya mtaani) na hapa alitoa mfano wa slogan ya NO JUSTICE NO PEACE imetoka mtaani. 9. Street Entrepreneurialism (Ujasiliamali wa mtaani).
Ukiangalia maelezo yangu kwa ufupi ni dhahiri utapata majibu ya nani mkali kati ya Fid Q na Kala Pina. Kwa ufupi wote wako katika same movement na wanahishi katika utamaduni mmoja isipokua wanazidiana katika vitu vichache. Fid anamzidi Kalapina katika Nguzo ya saba yaani lugha za mtaani hasa katika kuandika na uchenguaji pia yuko vizuri. Kala Pina nae yuko vizuri katika kuandika lakini sio mzuri katika street language.
Katika harakati hizi naweza pia kusema Kalapina amekua imara kwa muda mrefu na hasa katika kusimamia na kuhakikisha misingi ya utamaduni wa hiphop inafuatwa tofauti na Emcees wengine!
Sasa wewe utaamua nani zaidi…Mimi nimewasilisha tu baadhi ya tofauti kwa uelewa wangu!
View attachment 93761View attachment 93762

KRS One ni legendary lakini nae anajiongezea tu nguzo utafikiri ana mamlaka flani hivi ya Hip hop!!!
 
kumbe ndio maana watu huwa wanafeli

Mtu unaulizwa nani Mkali kati ya Kala P na Fid Q mtu unashindwa kutoa straight answer ...

kwa upande wangu sijui nani zaidi maana haya makitu yana wenyewe
 
Hakuna MC hapo! Watoto mlioanza kusikiliza muziki juzi ndio kauli zenu hizi.
FID Q asili ya style yake ni Mapacha (maujanja supplier) na ni bingwa wa kucopy hadi mistari.
Ipo siku sanaa itarudi kwa wenyewe kama enzi zile!

walikuwa wanajiita MACHIZI WA HATARI!!!nakumbuka sana kipindi hiko
 
Fid q ndo kila ki2 ndo maana wasanii wengi wa hphop hapa tanzania wanamtaja kama ndio role model wao e.g niki mbishi, young kila,stamina n.k
 
Nitakuwa najaza server za JF tu bure mkuu wangu tumeshajadili sana hawa wasanii kitambo pekenyua humu utapata kila kitu.

Fid Q hana nyimbo nyingi kiasi hicho cha kujaza server ya JF we weka link watu tusome nitapekenyua kitu ambacho sijui hata thread inaitwaje?

Fareed ni habari nyingine hao Mapacha wanasubiri mbali sana
 
Back
Top Bottom