Alvajumaa
JF-Expert Member
- Jul 5, 2018
- 5,039
- 6,253
Uso wa Mo Dewji katikati ya ujanja na ujinga wa Haji Manara
Kalamu ya Ally Kamwe
Kwa Jicho lingine. Kwa mtazamo mwingine, Press ya Simba Sc leo imetuonyesha kilichojifisha katikati ya ujanja na ujinga wa Haji Manara.
Ni mkutano uliobeba majibu ya viongozi juu ya sin'tofahamu iliyotokeza hivi karibuni kati ya Haji Manara na mashabiki wa Simba.
Mbele ya waandishi wa habari, Simba SC leo imesemewa na watu wawili wakubwa ndani ya klabu hiyo. Mwekezaji Mohammed Dewji na Mwenyekiti Swedi Nkwabi. Wawili tu.
Haji Manara hakushiriki kwa lolote. Si kwa kuonekana kwenye mkutano wala kupost taarifa ya mkutano huu kwenye mitandao ya kijamii. Na si kawaida yake.
Hii Tafsiri yake ni nini? Kuna kosa Haji Manara alilifanya hivi karibuni. Japo alitumia nguvu kubwa kujisafisha/ kulikanusha, lakini ukweli ni kuwa kosa lile liliacha madhara makubwa sana katika kazi yake.
Haji aligombana na mashabiki wa Simba. Watu waliowahi kumuamini kama Kibwetele alivyoaminika na wafuasi wake.
Ni mashabiki hao aliowaita "mashabiki maandazi" ndio waliibeba na kuiamini ile hoja yake kuwa Simba ingeweza kuifunga Barcelona na PSG.
Wakajazana uwanjani kwa furaha. Wakanunua jezi. Wakaimba na kucheza kila Simba ilipokuwa ikicheza hata mchana wa Jua kali.
Kukosana na watu hawa kwa kigezo 'eti ametukaniwa mzazi mitandaoni', lilikuwa ni miongoni mwa makosa kubwa kuwahi kufanywa na Haji katika maisha yake. Pengine analijutia wakati huu.
Mpira si mchezo wa kiungwana kiasi. Umekusanya mashabiki tofauti tofauti wenye hisia zisizofanana. Wakati mwingine tunasema soka ni mchezo wa wendawazimu.
Ndio. Ngoja nikupe mfano wa uwendawazimu kwenye soka.
Kwa mfano wewe ni shabiki wa Chelsea, baba ako ni shabiki wa liverpool... Mkiwa mnaangalia mechi yenu pamoja, ukakerwa na jambo na ukajikuta umetukana (ashakum sio matusi) "Hawa Liver wote wasenge tu"...
Kimaana hapa unakua umemjumlisha na baba yako. Lakini kuna mtu alishawahi kuadhiwa kwa kosa hili na mzazi wake? Pengine utastaajabu na baba ako akakujibu hivyo hivyo, mkacheka, mpira ukaisha na maisha yakaendelea.
Haji alitakiwa kuelewe vitu vidogo na vikubwa na maana yake huku kwenye mpira. Kwa vyovyote, majibishano yale kati yake na mashabiki hayakutakiwa.
Madhara yake ni kama haya tuliyoyaona leo. Imebidi Mo Dewji na Swedi Nkwabi wajitokeze mbele ya waandishi wafanye kazi yake.
Tena amewatesa kweli kweli mabosi wake!
Wamejikuta wakilazimika kueleza na mipango mingi ya siri mbele ya waandishi ili wafikie lengo lao la kutangaza viingilio vya mechi.
Yes. Ni MO DEWJI aliyetangaza kuwa mechi itachezwa saa 10 na viingilio ni Tsh 2000. Kiwango kidogo kabisa kulinganisha na thamani na ubora wa mechi yenyewe.
Ilibidi iwe hivyo kwa sababu Haji Manara haaminiki na kundi kubwa la watu kama zamani. Ameshawaga wapenzi wa Simba. Hata angetangaza kiingilio ni buku bado watu wangeacha kujadili mechi na kuanza kumshughulikia yeye.
Siamini kama huu ndio mwisho wake, ila naamini hili ni FUNZO KUBWA analoweza kujifunza kama kichwa chake kitapenda kujifunza.
"Mafuta ya taa robo tu yanaweza kuharibu Maji pipa zima."
Sent using Jamii Forums mobile app
Kalamu ya Ally Kamwe
Kwa Jicho lingine. Kwa mtazamo mwingine, Press ya Simba Sc leo imetuonyesha kilichojifisha katikati ya ujanja na ujinga wa Haji Manara.
Ni mkutano uliobeba majibu ya viongozi juu ya sin'tofahamu iliyotokeza hivi karibuni kati ya Haji Manara na mashabiki wa Simba.
Mbele ya waandishi wa habari, Simba SC leo imesemewa na watu wawili wakubwa ndani ya klabu hiyo. Mwekezaji Mohammed Dewji na Mwenyekiti Swedi Nkwabi. Wawili tu.
Haji Manara hakushiriki kwa lolote. Si kwa kuonekana kwenye mkutano wala kupost taarifa ya mkutano huu kwenye mitandao ya kijamii. Na si kawaida yake.
Hii Tafsiri yake ni nini? Kuna kosa Haji Manara alilifanya hivi karibuni. Japo alitumia nguvu kubwa kujisafisha/ kulikanusha, lakini ukweli ni kuwa kosa lile liliacha madhara makubwa sana katika kazi yake.
Haji aligombana na mashabiki wa Simba. Watu waliowahi kumuamini kama Kibwetele alivyoaminika na wafuasi wake.
Ni mashabiki hao aliowaita "mashabiki maandazi" ndio waliibeba na kuiamini ile hoja yake kuwa Simba ingeweza kuifunga Barcelona na PSG.
Wakajazana uwanjani kwa furaha. Wakanunua jezi. Wakaimba na kucheza kila Simba ilipokuwa ikicheza hata mchana wa Jua kali.
Kukosana na watu hawa kwa kigezo 'eti ametukaniwa mzazi mitandaoni', lilikuwa ni miongoni mwa makosa kubwa kuwahi kufanywa na Haji katika maisha yake. Pengine analijutia wakati huu.
Mpira si mchezo wa kiungwana kiasi. Umekusanya mashabiki tofauti tofauti wenye hisia zisizofanana. Wakati mwingine tunasema soka ni mchezo wa wendawazimu.
Ndio. Ngoja nikupe mfano wa uwendawazimu kwenye soka.
Kwa mfano wewe ni shabiki wa Chelsea, baba ako ni shabiki wa liverpool... Mkiwa mnaangalia mechi yenu pamoja, ukakerwa na jambo na ukajikuta umetukana (ashakum sio matusi) "Hawa Liver wote wasenge tu"...
Kimaana hapa unakua umemjumlisha na baba yako. Lakini kuna mtu alishawahi kuadhiwa kwa kosa hili na mzazi wake? Pengine utastaajabu na baba ako akakujibu hivyo hivyo, mkacheka, mpira ukaisha na maisha yakaendelea.
Haji alitakiwa kuelewe vitu vidogo na vikubwa na maana yake huku kwenye mpira. Kwa vyovyote, majibishano yale kati yake na mashabiki hayakutakiwa.
Madhara yake ni kama haya tuliyoyaona leo. Imebidi Mo Dewji na Swedi Nkwabi wajitokeze mbele ya waandishi wafanye kazi yake.
Tena amewatesa kweli kweli mabosi wake!
Wamejikuta wakilazimika kueleza na mipango mingi ya siri mbele ya waandishi ili wafikie lengo lao la kutangaza viingilio vya mechi.
Yes. Ni MO DEWJI aliyetangaza kuwa mechi itachezwa saa 10 na viingilio ni Tsh 2000. Kiwango kidogo kabisa kulinganisha na thamani na ubora wa mechi yenyewe.
Ilibidi iwe hivyo kwa sababu Haji Manara haaminiki na kundi kubwa la watu kama zamani. Ameshawaga wapenzi wa Simba. Hata angetangaza kiingilio ni buku bado watu wangeacha kujadili mechi na kuanza kumshughulikia yeye.
Siamini kama huu ndio mwisho wake, ila naamini hili ni FUNZO KUBWA analoweza kujifunza kama kichwa chake kitapenda kujifunza.
"Mafuta ya taa robo tu yanaweza kuharibu Maji pipa zima."
Sent using Jamii Forums mobile app