Kalamu ya Mkali: Kuundwa kwa Kamati ya Mwigulu ni Matumizi Mabaya ya Fedha za Umma

Kalamu ya Mkali: Kuundwa kwa Kamati ya Mwigulu ni Matumizi Mabaya ya Fedha za Umma

Mathanzua

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2017
Posts
17,251
Reaction score
22,929
HII NI HUJUMA NA MATUMIZI MABAYA YA FEDHA ZA WANANCHI.

IMG_20220913_173937.jpg

Hebu tutazame kiasi gani cha fedha zitafujwa kupitia hii Kamati kwa kitu ambacho jibu liko wazi,tozo ni "Poll Tax," kwa hiyo wananchi hawapaswi kutozwa,vitafutwe vyanzo vingine vya mapato,na vipo..

1) Hao wajumbe 200 kila mmoja atalipwa ‘allowance – per diem) ya shilingi 250,000/= kila siku. (200 ×250,000 = 50,000,000).

2) Shilingi milioni hamsini zitakuwa zinatumika kila siku ya uhai wa hiyo Kamati.

3) Hii Kamati itadumu kwa muhula wa miezi minne. Tuzidishe hiyo milioni hamsini mara siku 120, (50,000,000 × 120 = 6,000,000,000/=). Hapo hatujaweka gharama za hivyo vitendea kazi: magari na Laptops. Kuharibu kiasi hiki cha fedha kuchunguza suala ambalo lilitakiwa kufutwa bila uchunguzi ni uhujumu uchumi.

4) Ni dhahiri kuwa Mh.Mwigulu amepwaya kwenye wadhifa wake. Dalili zote zinaonyesha kuwa kazi imemshinda. Upeo huu wa wananchi kuchukia uamuzi wa Serikali yao katika suala hili la tozo haujapata kutokea tangu uhuru.Mheshimiwa Mwigulu aidha apumzishwe au ajipumzishe kwa kujiuzulu.

5) Ni kweli kuwa huo uamuzi ulipitia Bungeni, lakini Rais hawezi kuwatumbua wabunge wote waliopitisha bili iliyozaa hii tozo. Lakini Kiongozi wa juu muhusika kuwajibika au kuwajibishwa ni sawa.

6) Katika muda wa miaka mitano, hayupo Rais, tangu uhuru, ambaye alileta huduma na kujenga miradi mikubwa kwa nchi yetu kama alivyofanya Hayati Magufuli. Lakini alitekeleza hayo bila tozo yoyote.

7) Aidha, hayati Mwalimu Julius Nyerere alituachia mashirika ya umma hai 450, alitoa bure huduma za afya na elimu pamoja na ruzuku kwa wakulima. Pamoja na hayo, alisaidia kimatendo ukombozi wa bara la Afrika kuliko Rais mwingine yoyote; na upeo wa utumiaji wa natural wa raslimali zetu wakati ule ulikuwa mdogo kuliko leo.
Na yeye pia hakutumia tozo. Huu umuhimu wa tozo leo, unaletwa na nini?

8) Kadhalika, hii tozo ni sawa kabisa na “Poll tax’ ya zama za kikoloni; ambayo Mwalimu Nyerere aliifuta mwaka 1968 kwa sababu ilikuwa ni ya kisheria lakini si ya haki.

9) Tujikumbushe kuwa aliyekuwa Waziri Mkuu wa Uingereza wakati huo Margaret Thatcher, alilazimishwa na Chama chake Cha Conservative ajiuzulu,baada ya kuleta tozo au “Poll tax”; tozo ambayo ingalikifanya Chama cha Conservative kisishinde uchaguzi uliokuwa unakuja. Aliyechukuwa nafasi yake John Major, alifutilia mbali hiyo tozo kabla ya uchaguzi.

USHAURI.
Hii tozo ifutwe bila kuundwa Kamati ya aina yoyote. Tozo hii inajenga chuki kali kati ya wananchi na Viongozi wa nchi yetu. Haileti maana Taifa kutumia Shilingi bilioni sita, kuchunguza kama wananchi waendelee kunyanyaswa na hii tozo ambayo si ya haki.


Tanzania tusikubali kuvuruga amani yetu ili kuhifadhi uso au nyuso za watu wachache waliobuni tozo kandamizi, tozo isiyo ya haki.
 
Sidhani kama hii ni kweli! kuna vingi vya kushangaza kwenye hiyo nchi lkn hili nakataa, data zimepikwa hizo,,, kwa mwenye akili timam haingii akilini
 
Aisee! Kwa hiyo hiyo kamati haramu ikija na majibu ya kuwa Tozo iendelee hizo 6 billions zitakuwa zime leta tija gani kwa mwananchi? Mama si angesema tozo isitishwe kwanza wakati serikali ikiangalia namna nyingine ya kumkamua mwananchi?

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Sidhani kama hii ni kweli! kuna vingi vya kushangaza kwenye hiyo nchi lkn hili nakataa, data zimepikwa hizo,,, kwa mwenye akili timam haingii akilini
Labda ungeleta za kwako unazozijua tulingsnishe na hizi tulizo nazo.Nullify facts by facts.Vinginevyo hatuwezi kukubali your side of the story.Tulizo nazo sasa ndio sahihi,unless you prove otherwise.
 
HII NI HUJUMA NA MATUMIZI MABAYA YA FEDHA ZA WANANCHI.

IMG_20220913_173937.jpg

Hebu tutazame kiasi gani cha fedha zitafujwa kupitia hii Kamati kwa kitu ambacho jibu liko wazi,tozo ni "Poll Tax," kwa hiyo wananchi hawapaswi kutozwa,vitafutwe vyanzo vingine vya mapato,na vipo..

1) Hao wajumbe 200 kila mmoja atalipwa ‘allowance – per diem) ya shilingi 250,000/= kila siku. (200 ×250,000 = 50,000,000).

2) Shilingi milioni hamsini zitakuwa zinatumika kila siku ya uhai wa hiyo Kamati.

3) Hii Kamati itadumu kwa muhula wa miezi minne. Tuzidishe hiyo milioni hamsini mara siku 120, (50,000,000 × 120 = 6,000,000,000/=). Hapo hatujaweka gharama za hivyo vitendea kazi: magari na Laptops. Kuharibu kiasi hiki cha fedha kuchunguza suala ambalo lilitakiwa kufutwa bila uchunguzi ni uhujumu uchumi.

4) Ni dhahiri kuwa Mh.Mwigulu amepwaya kwenye wadhifa wake. Dalili zote zinaonyesha kuwa kazi imemshinda. Upeo huu wa wananchi kuchukia uamuzi wa Serikali yao katika suala hili la tozo haujapata kutokea tangu uhuru.Mheshimiwa Mwigulu aidha apumzishwe au ajipumzishe kwa kujiuzulu.

5) Ni kweli kuwa huo uamuzi ulipitia Bungeni, lakini Rais hawezi kuwatumbua wabunge wote waliopitisha bili iliyozaa hii tozo. Lakini Kiongozi wa juu muhusika kuwajibika au kuwajibishwa ni sawa.

6) Katika muda wa miaka mitano, hayupo Rais, tangu uhuru, ambaye alileta huduma na kujenga miradi mikubwa kwa nchi yetu kama alivyofanya Hayati Magufuli. Lakini alitekeleza hayo bila tozo yoyote.

7) Aidha, hayati Mwalimu Julius Nyerere alituachia mashirika ya umma hai 450, alitoa bure huduma za afya na elimu pamoja na ruzuku kwa wakulima. Pamoja na hayo, alisaidia kimatendo ukombozi wa bara la Afrika kuliko Rais mwingine yoyote; na upeo wa utumiaji wa natural wa raslimali zetu wakati ule ulikuwa mdogo kuliko leo.
Na yeye pia hakutumia tozo. Huu umuhimu wa tozo leo, unaletwa na nini?

8) Kadhalika, hii tozo ni sawa kabisa na “Poll tax’ ya zama za kikoloni; ambayo Mwalimu Nyerere aliifuta mwaka 1968 kwa sababu ilikuwa ni ya kisheria lakini si ya haki.

9) Tujikumbushe kuwa aliyekuwa Waziri Mkuu wa Uingereza wakati huo Margaret Thatcher, alilazimishwa na Chama chake Cha Conservative ajiuzulu,baada ya kuleta tozo au “Poll tax”; tozo ambayo ingalikifanya Chama cha Conservative kisishinde uchaguzi uliokuwa unakuja. Aliyechukuwa nafasi yake John Major, alifutilia mbali hiyo tozo kabla ya uchaguzi.

USHAURI.
Hii tozo ifutwe bila kuundwa Kamati ya aina yoyote. Tozo hii inajenga chuki kali kati ya wananchi na Viongozi wa nchi yetu. Haileti maana Taifa kutumia Shilingi bilioni sita, kuchunguza kama wananchi waendelee kunyanyaswa na hii tozo ambayo si ya haki.


Tanzania tusikubali kuvuruga amani yetu ili kuhifadhi uso au nyuso za watu wachache waliobuni tozo kandamizi, tozo isiyo ya haki.

mkali@live.co.uk.
13/09/2022.
Hoja ya gharama ya kuhudumi hiyo timu kama ndivyo ilivyo basi ni sahihi haipaswi kuwa hivyo..

Pili swala la eti Mwendazake alijenga miundombinu mikubwa bila tozo ni upuuzi tuu kwa sababu zaidi ya kuanzisha hakuna miundombinu hata mmja aliumaliza Kati ya yoote iliyoanzisha..

Mwisho wakati akianzisha alikuwa anapora pesa za matajiri wachache huku wengi wakishangilia na matokeo yake aka paralyse uchumi Kwa kuwa frastrate wafanyabiashara hivyo Hali ya uchumi ikawa mbaya..

Awamu hii imerejesha mzunguko wa uchumi na hivyo kila mtu anatakiwa kuchangia gharama za kukamilisha hayo mamiradi yakipuuzi kadiri ya kipato chake so naunga mkono hoja ya tozo ila sio kukatwa mara mbili mbili maana watu wenyewe hawalipi Kodi inavyotakiwa hivyo tozo inaziba kinachpotea..

Mwisho kabisa ni kwamba watu wa Mjini walizoea kuwanyonya watu wa Vijijini ila sasa wamekamatika kwa njia ya tozo za banks ndio maana kuna makelele kibao ambayo hatukuyasikia kwenye miamala ya simu ambako makato ni makubwa kuliko banks sababu ni kwamba watu wa Vijijini wanatumia miamala ya simu na WA mjini wanatumia banks..

Tozo hazifutwi ndio maana Serikali imevuta mda hadi mwezi wa 4 Ili kufanya tathmini ya tozo kwenye uchumi..
 
Shibe mwana malevya....
Ni kweli kabisa mkuu,shibe inalewesha.Kwa bahati mbaya it turns out kwamba mwenye shida hamjui mwenye njaa,kwa hiyo si ajabu sasa kwamba tunaona ufujaji wa fedha za maskini katika kiwango cha kutisha.Mtumishi wa serikali ya wananchi maskini,unapata wapi ujasiri wa kununua gari la Sh.500 million na kutembea kwenye misafara mikubwa ya magari!!!!
 
Hoja ya gharama ya kuhudumi hiyo timu kama ndivyo ilivyo basi ni sahihi haipaswi kuwa hivyo..

Pili swala la eti Mwendazake alijenga miundombinu mikubwa bila tozo ni upuuzi tuu kwa sababu zaidi ya kuanzisha hakuna miundombinu hata mmja aliumaliza Kati ya yoote iliyoanzisha..

Mwisho wakati akianzisha alikuwa anapora pesa za matajiri wachache huku wengi wakishangilia na matokeo yake aka paralyse uchumi Kwa kuwa frastrate wafanyabiashara hivyo Hali ya uchumi ikawa mbaya..

Awamu hii imerejesha mzunguko wa uchumi na hivyo kila mtu anatakiwa kuchangia gharama za kukamilisha hayo mamiradi yakipuuzi kadiri ya kipato chake so naunga mkono hoja ya tozo ila sio kukatwa mara mbili mbili maana watu wenyewe hawalipi Kodi inavyotakiwa hivyo tozo inaziba kinachpotea..

Mwisho kabisa ni kwamba watu wa Mjini walizoea kuwanyonya watu wa Vijijini ila sasa wamekamatika kwa njia ya tozo za banks ndio maana kuna makelele kibao ambayo hatukuyasikia kwenye miamala ya simu ambako makato ni makubwa kuliko banks sababu ni kwamba watu wa Vijijini wanatumia miamala ya simu na WA mjini wanatumia banks..

Tozo hazifutwi ndio maana Serikali imevuta mda hadi mwezi wa 4 Ili kufanya tathmini ya tozo kwenye uchumi..
Mkuu hoja zako zote mbona ni nyepesi sana na hazina mashiko.Naomba uzitafakari, vizuri ni mufilisi kabisa.
 
Mkuu hoja zako zote mbona ni nyepesi sana na hazina mashiko.Naomba uzitafakari, vizuri ni mufilisi kabisa.
How mufilisi?

Tozo za miamala zimeanza last year kwenye simu ila zilipoanza na kwenye banks kumegokea makelele,jibu ni kwamba wa mjini ndio wenye acconts banks so lipa tozo Kwa maendeleo ya Vijijini..
 
Yule mzee mzungu wa gazeti la Mwananchi ameichambua hii in a very comical but insightful way. Hakika kesho ya nchi hii ipo njiapanda kama sio shakani.
 
Mkali ndio nani mkuu ?
Mkali ni Journalist ambaye ana base yake London.Ni mtoto wa Mzee Mkali wa Dar es Salaam ambaye kimsingi ni mmoja wapo wa waasisi wa CCM.Sina hakika kama Mzee Mkali bado yupo,nadhani kama sikosei he died last year,or year last.
 
Mkali ni Journalist ambaye ana base yake London.Ni mtoto wa Mzee Mkali wa Dar es Salaam ambaye kimsingi ni mmoja wapo wa waasisi wa CCM.Sina hakika kama Mzee Mkali bado yupo,nadhani kama sikosei he died last year,or year last.
Kuna mwandishi wa habari wa kimataifa niliwahi kukutana na kuwa rafiki yangu kwa muda nae anaitwa Ephraim Mkali (kama sikosei )alikuwa ana madini ya uzani nimepotezana nae muda mrefu sijui yuko wapi now nilivyoliona jina hilo nilistuka kidogo.
 
Tafsiri yake pamoja na malalamiko yote na maagizo ya chama chao bado uwepo wa hizi tozo ni confirmed kwa miezi mitatu ijayo halafu kuna wapumbavu wanasifia mama msikivu.
sijui wanatuchukuliaje hawa jamaa!!!
 
How mufilisi?

Tozo za miamala zimeanza last year kwenye simu ila zilipoanza na kwenye banks kumegokea makelele,jibu ni kwamba wa mjini ndio wenye acconts banks so lipa tozo Kwa maendeleo ya Vijijini..
Fallacy,mwandishi wa hiyo makala amesema wazi:- 1.Kwamba tozo ni Poll Tax,na kimsingi ni kwamba tunawarudisha wananchi kwenye ukoloni,and that is not acceptable.
2.There are many sources of revenue which have not been exploited,sasa kwa nini tusi-exploit hizo,na badala yake tunatoza watu maskini ambao hata mlo mmoja kwa siku kwao shida kuupata?Bandari zetu tu zingetosha kutupatia mapato ya kutosha. Tunayo ona sasa ni ukosefu wa weledi,kutokuwa tayari kuwatumikia wananchi kwa moyo na kutokujiongeza.
3.Already Watanzania wako burdened na kodi nyingi, PAYE,VAT,Michango ya Mwenge,Majengo,Ardhi,miundo mbinu ya maji nk.nk.Hivi serikali na hata wewe,huoni kwamba huku ni kumfukarisha mwananchi na kum-expose to the poverty vicious circle?
4.Naomba pia ukumbuke kwamba ukituma hela kwa kutumia Bank unakatwa wewe unayetuma na anayepokea,this is not fair.Hela hizo hizo zikatwe tozo mara mbili!!!No,no,no,huo ni uonevu na wizi.
5.Ikumbukwe pia kwamba anayeweka,anayetuma hela au anayepokea hela kwa kutumia Bank sio mtu wa mjini tu siku hizi,Mawakala wa Banks wapo vijijini ,kwa hiyo wananchi vijijini wana access to banking services,so they are affected by these very poor decisions of our leaders.
 
Fallacy,mwandishi wa hiyo makala amesema wazi:- 1.Kwamba tozo ni Poll Tax,na kimsingi ni kwamba tunawarudisha wananchi kwenye ukoloni,and that is not acceptable.
2.There are many sources of revenue which have not been exploited,sasa kwa nini tusi-exploit hizo,na badala yake tunatoza watu maskini ambao hata mlo mmoja kwa siku kwao shida kuupata?Bandari zetu tu zingetosha kutupatia mapato ya kutosha. Tunayo ona sasa ni ukosefu wa weledi,kutokuwa tayari kuwatumikia wananchi kwa moyo na kutokujiongeza.
3.Already Watanzania wako burdened na kodi nyingi😛AYE,VAT,Michango ya Mwenge,Majengo,Ardhi nk.nk.Hivi serikali na hata wewe,huoni kwamba huku ni kumfukarisha mwananchi na kum-expose to the poverty vicious circle?
4.Naomba pia ukumbuke kwamba ukituma hela kwa kutumia Bank unakatwa wewe unayetuma na anayepokea,this is not fair.Hela hizo hizo zikatwe tozo mara mbili!!!No,no,no,huo ni uonevu na wizi.
5.Ikumbukwe pia kwamba anayeweka,anayetuma hela au anayepokea hela kwa kutumia Bank sio mtu wa mjini tu siku hizi,Mawakala wa Banks wapo vijijini ,kwa hiyo wananchi vijijini wana access to banking services,so they are affected by these very poor decisions of our leaders.
Hizo a lot of sources of revenues ni kama zipi? Mbona Kodi tuu ya pango hamtaki kulipa,ukienda dukani hutaki kudai risiti nk nk..

Hizo toll taxes zimekuwa zikitozwa kwa sie wanavijiji kwenye mazao yetu over years na kujenga Mjini..Sasa ni zamu ya Wa mjini kulipa tozo by whatever naming it ila pesa ipatikane na iounguze adha Vijijini..
 
Kuna mwandishi wa habari wa kimataifa niliwahi kukutana na kuwa rafiki yangu kwa muda nae anaitwa Ephraim Mkali (kama sikosei )alikuwa ana madini ya uzani nimepotezana nae muda mrefu sijui yuko wapi now nilivyoliona jina hilo nilistuka kidogo.
Huyu sio yeye mkuu.Huyu ni Harid,ni Muislam,na makazi take ni London.
 
Hizo a lot of sources of revenues ni kama zipi? Mbona Kodi tuu ya pango hamtaki kulipa,ukienda dukani hutaki kudai risiti nk nk..

Hizo toll taxes zimekuwa zikitozwa kwa sie wanavijiji kwenye mazao yetu over years na kujenga Mjini..Sasa ni zamu ya Wa mjini kulipa tozo by whatever naming it ila pesa ipatikane na iounguze adha Vijijini..
Nimesema hizo tozo hawalipi wa mjini tuu,hata watu wa vijiji wanalipa,kwa kuwa banking services zipo hata vijijini......!!!
Why don't you address this.Acha kuwa kipofu wewe.Tumesema kibaya zaidi ni kwamba tozo hizo hazina MATUMIZI mazuri zinafujwa,na wananchi tunaona.You people must be able to see the writing on the wall.Governments have fallen kwa kutokuzingatia matakwa ya wananchi.Juzi tu hapa the Sri Lankan government has fallen,Kenyatta and Company has suffered defeat in the of the opposition,so the government should not underestimate people's power,na kudhani kwamba it is indispensable.
 
Nimesema hizo tozo hawalipi wa mjini tuu,hata watu wa vijiji wanalipa,kwa kuwa banking services zipo hata vijijini......!!!
Why don't you address this.Acha kuwa kipofu wewe.Tumesema kibaya zaidi ni kwamba tozo hizo hazina MATUMIZI mazuri zinafujwa,na wananchi tunaona.You people must be able to see the writing on the wall.Governments have fallen kwa kutokuzingatia matakwa ya wananchi.Juzi tu hapa the Sri Lankan government has fallen,Kenyatta and Company has suffered defeat in the of the opposition,so the government should not underestimate people's power,na kudhani kwamba it is indispensable.
Yaa wa Vijijini tuna feel proud of tozo Kwa sababu tunaona zinavyorudi kutusaidia..

At a particular time,Ulimwengu aliwahi sema kwamba alikataa kuwa DC huko Dar coz hakuna kipya angefanya kingeonekana ila Vijijini unafanya vinaoneka na unasema tozo imeleta kile na hiki..

Kama tozo hazina matumizi mazuri zina matumizi yapi sasa tofauti na tunayoyaona na nayokwambia na ambayo serikali imeyasema na tunayaona? Wewe wa mjini huwezi ona coz unavyo vitu daily ila sie ambao hatukuwa na vitu tunavyo..

Kwamba una address vipi ndio kama hivi lipa tozo mambo yawe addressed..

Hayo ya Sri Lanka na Kenya ni irrelevant,kwani unadhani SSH anashindwa kuwaambia village dwellers kwamba nime impose for your development na matokeo Ndio haya mnaona..

Wa mjini wanapinga kwa sababu wamewabyonya over years,kwa nini wasimuelewe?
 
Back
Top Bottom