Boniphace Kichonge
JF-Expert Member
- Jul 31, 2017
- 1,605
- 1,957
Wakuu aliyekuwa mgombea mwenza wa Urais nchini Kenya kupitia muungano wa NASA ameshauriwa aachane na Raila Odinga na badala yake ajiunge na chama Tawala cha Jubilee.
Kwa mujibu wa Wazee wa Ukambani pamoja na washauri wengine wamedai kuwa kwa sasa mashirikiano hayo hayana faida yoyote kwa jamii hiyo badala yake yameiletea jamii hiyo hasara kwa hivyo nibora ajiondoe kwenye ushirika huo.
Mhesh Kalonzo pia amepinga mpango wa kufanya maandamano nchi nzima ulioitishwa na RAO kwa kusema una lengo lakuleta ghasia na vurugu nchini humo na ni kitendo cha kuhujumu Uchumi. Aidha amekosoa uamuzi wa RAO kujitoa kwenye uchaguzi wa marudio kuwa ni wa kibinafsi na haukufanywa kwa kuzingatia maslahi mapana ya Wakenya. Ameongeza kuwa njia sahihi ya kupata Uongozi ni kupitia Uchaguzi na sivinginevyo.
Taarifa hizi ni kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi.
Karibuni
Kwa mujibu wa Wazee wa Ukambani pamoja na washauri wengine wamedai kuwa kwa sasa mashirikiano hayo hayana faida yoyote kwa jamii hiyo badala yake yameiletea jamii hiyo hasara kwa hivyo nibora ajiondoe kwenye ushirika huo.
Mhesh Kalonzo pia amepinga mpango wa kufanya maandamano nchi nzima ulioitishwa na RAO kwa kusema una lengo lakuleta ghasia na vurugu nchini humo na ni kitendo cha kuhujumu Uchumi. Aidha amekosoa uamuzi wa RAO kujitoa kwenye uchaguzi wa marudio kuwa ni wa kibinafsi na haukufanywa kwa kuzingatia maslahi mapana ya Wakenya. Ameongeza kuwa njia sahihi ya kupata Uongozi ni kupitia Uchaguzi na sivinginevyo.
Taarifa hizi ni kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi.
Karibuni