Kama anga isiposafishwa basi Roketi zinaweza kushuka duniani Japan

Kama anga isiposafishwa basi Roketi zinaweza kushuka duniani Japan

Teknolojia ni Yetu sote

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2020
Posts
620
Reaction score
1,240
Japan kutuma chombo kwenda kusafisha Anga kwenye roketi zilizokufa

Ubongo _20250314_042201_0000.png

Shirika la Anga toka Japan Astrocale inakabiliana na tishio la kuongoezeka kwa takataka Angani na kuamua kuzindua Misheni ya ADRAS - J hii ni Jaribio la kwanza la kukaribia Roketi ya kijapan ya H - IIA iliyotupwa | kufa na kukaribia kushuka duniani.

Roketi hiyo iliyokufa toka mwaka 2009 inasemekana inataka kushuka duniani ambapo Japan waliweza kubaini kupitia Kamera Zao za leza cha chombo chao na kutoa picha zilizoonyesha chombo kilichokufa ndani ya mita 15 (futi 49) kutoka kwa uchafu.

2_20250314_040551_0001.png

Kwa kuzingatia Mafanikio haya Astrocale iliweza kutoa Dola milioni 88 kutoka kwa wakala wa anga za juu wa Japan ili kuzindua ADRAS-J2 mnamo 2027, ambayo itatumia mkono wa roboti kunasa na kugeuza hatua ya roketi hiyo iliyokufa isije shuka duniani.

Kukiwa na Roketi zaidi ya 2,000 zilizotupwa na kufa, vikiwa na vipande 32,000 vikubwa vya uchafu vinavyozunguka Dunia, kuondolewa kwa takataka ni muhimu,

3_20250314_040551_0002.png

NASA inakadiria na gharama kubwa ya dola milioni 8 kwa kila kipande, lakini kutochukua hatua kunaweza kuhatarisha migongano ambayo itavuruga mawasiliano ya kimataifa na mifumo ya navigation system.

#SpaceJunk #Astroscale #ADRASJ #SpaceDebris #Satellite Protection #SpaceExploration #OrbitalCleanup #NASA #JapanSpace Agency #TechNews
 
Wenzetu wametuacha mbali sana.sisi Huku eti Samia anazindua vyoo vya shule ya msingi na kujisifu kuwa maendeleo eti Kwa miaka zaidi ya 64 ya uhuru!
 
Back
Top Bottom