Kama Daktari wa Binadamu anaumizwa na kifo cha mgonjwa. Je, ni maumivu gani aliyonayo mtekaji na muuaji?

Kama Daktari wa Binadamu anaumizwa na kifo cha mgonjwa. Je, ni maumivu gani aliyonayo mtekaji na muuaji?

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2019
Posts
762
Reaction score
6,984
Mdogo wangu ni retired Dr. Juzi alikuwa anaangalia kumbukumbu ya kifo kwenye tv. Moja ya tangazo aliloliona ni tangazo la mgonjwa aliyefariki miaka 12 baada ya kumfanyia upasuaji, alishtuka na kuumia sana.

Mdogo wangu aliumia si kwa sababu nyingine bali anaeleza kuwa wao madaktari ni walinzi wa uhai na kiapo chao ni kuokoa maisha. Anaposhuhudia uhai ukitoka mikononi mwao pamoja na juhudi kubwa walizofanya uumia sana. Daktari utibu kwa akili za kawaida lakini pia kila hatua umshirikisha Mungu awape ulinzi na mwongozo wa Nini wafanye, anasema huyu ndugu yangu.

Story na machungu aliyonayo yakanifanya nijiulize ni namna gani baadhi ya matangazo kwenye social media na vyombo vingine kwa habari yanawaumiza watu tusiowajua? Lakini nikasema ukitenda kwa haki maumivu ya kile ulichokiona yataambatana na faraja kutoka kwa Mungu.

Lakini nilipoanza kutafakari nikakumbuka juzi nilisoma kumbukizi ya Mawazo aliyeuawa Geita, Leo nikaona wanamzungumzia Ben Saanane aliyetekwa na kupotea tusijue alipo, nikakumbuka kuwa kuona kilichotokea Zanzibar kwenye uchaguzi nk nikajiuliza Hawa waliotenda haya waonapo matangazo wanaumizwa Kama madaktari? Wakiumizwa ujifariji kwa kipi ilihali awakufanya kwa haki?

Ewe mwanadamu, social media na viweka kumbukumbu vimewekwa kukumbusha uliyowatendea wanadamu wenzio, hatutachoka kuwakumbuka waliotangulia, vivyo hivyo atutachoka kukukumbusha huko uliko kwamba huu uhai ulitoka kwa maelekezo yako, kwa mikono yako au kufedha zako.

Hii dhambi haina toba zaidi ya kukiri hadharani. Kuua toba yake ni kukiri adharani, Mwenyenzi Mungu hana siri
 
Maelezo yako yana majibu hapohapo.

Leo hii mfano mzazi wako angekua mwanajeshi aliyekua mstari wa mbele vita ya Kagera unadhani akionyeshwa maiti alizozisababisha roho itamuuma?

Majukumu yako yanafanya uone huruma ama la.

Umesema jukumu la mdogo ako ni kulinda uhai.

Mtekaji/ muuaji jukumu lake ni?
 
Mtu aliyeelimika hawezi uwa au tumika kuuwa mtu. Ni mtu punguani pekee ndo ukubali kutumika kuuwa mtu. Unamuua binadamu mwenzako wakati nawe ni marehemu mtarajiwa usiyejua hata kesho yako.

Unatumwa ukaue mtu ukishauwa kisha nawe ni lazima uuliwe ili kuficha Siri ya muuaji mkuu. Akili au matope
 
Pole sana,

Kuna mtu alimuuliza siku moja jasusi Chahali swali hili (kle insta)lakini kuna kitu aligusia kama vile dhamira inawsuta baadae.

Yote kwa yote hata mwizi anapokuja kukuibia kwanza anahalalisha kitendo kile (kwanza huyu hatoi zaka,hata wao waliiba n.k)
Lakini pia tusisahau kuwa kama tunavyomfuga mbwa tukamfundisha vile vile binadamu anaweza kufundishwa na hata kufanya ambao yeye mwenyewe mwanzoni alikuwa anakanusha.

Chukulia unaingia katika kozi ambayo kila unachofundishwa ni kuhusu Taifa lako na usalama wake,unafundishwa ya kuwa kuua watu wawili au watatu kwa ajili ya kuokoa mamilioni ni jambo la heri kabisa.Haya ndiyo manfundisho ambao hata magaidi wanafundishwa mpaka kufikia kuchinja binadamu mwenzie kama kuku.

Nakushauri tafuta gazeti la Mwananchi la miaka iliyopita kuna mahojiano na mnyongaji mmoja anaishi Dodoma,inaweza ikukasaidia ukawa na mwanga kidogo.

Hii ndiyo dunia la muhimu hakuna atakayedumu humu!!
 
Mtu aliyeelimika hawezi uwa au tumika kuuwa mtu. Ni mtu punguani pekee ndo ukubali kutumika kuuwa mtu. Unamuua binadamu mwenzako wakati nawe ni marehemu mtarajiwa usiyejua hata kesho yako.

Unatumwa ukaue mtu ukishauwa kisha nawe ni lazima uuliwe ili kuficha Siri ya muuaji mkuu. Akili au matope
Mbaya zaidi unatumwa kuutoa Uhai wa MTU ambaye unafahamu fika hana HATIA kabisa...
 
Mtu anaefanya kazi inayohusisha kushika bunduki hawezi kuumizwa na kifo labda kifo hicho kiguse familia yake moja kwa moja
fanya utafit utagundua hilo ni hatar sana kuwa karibu na watu hao
 
True che
Mbaya zaidi unatumwa kuutoa Uhai wa MTU ambaye unafahamu fika hana HATIA kabisa...

True check mfano mapolisi unamuua mtu asiye hata na silaha ili kumridhisha mwanasiasa ambae akipata nafasi kwa kupora haki za wengine amkumbuki hata kujali au kuboresha maisha ya police.Hii ipo afrika yote ya weusi.
 
Hao wasiojulikana nao wana roho ngumu kweli eti unatumwa kamuue fulani nao haooo wanaenda.

Sijui wakitafakari huwa hawaumii au kwao ni kama kuchinja kuku vile!
 
True che

True check mfano mapolisi unamuua mtu asiye hata na silaha ili kumridhisha mwanasiasa ambae akipata nafasi kwa kupora haki za wengine amkumbuki hata kujali au kuboresha maisha ya police.Hii ipo afrika yote ya weusi.
Adui wa MTU mweusi ni Mweusi mwenyewe...

Magufuli anasahau kuwa kumwaga Damu isiyo hatia ni LAANA juu ya Nchi na ndo maana Utajiri wote wa Tanzania unaenda Ulaya na Amerika kwasababu ya laana ya watawala.
 
Back
Top Bottom