Kama hayati Magufuli alimtuma Ole Sabaya kudhibiti wahujumu uchumi, Je huu ulikuwa ujambazi au matumizi mabaya ya ofisi?

Kama hayati Magufuli alimtuma Ole Sabaya kudhibiti wahujumu uchumi, Je huu ulikuwa ujambazi au matumizi mabaya ya ofisi?

Boss wake alijua KILA kitu kuhusu huyu mtumishi wake mwaminifu,alimuita akamuuliza akakiri kwamba anafanya Yale kupata pesa za kumsambaratisha Mbowe aliposikia yote Yale lengo ni kumsambaratisha akampa baraka tele na kumwambia ewe mtumishi mwaminifu endelea.Leo wote wamesambaratishwa hawapo tena.
Hakuna aliyewahi cheza na Mbowe akabaki salama.
 
Nani mwenye uhakika kama alitumwa? Hata kama alitumwa haimuondolei jinai aliyotenda,SABAYA HATOBOI....Hamuoni kwamba hiyo KUTUMWA ndio itakuwa kichaka kwa watumishi wa serikali?
 
Hata kule arusha utagundua mashahidi wa kipuuzi maana mwenye duka ni mwarabu fisadi. Wao wanamwamini bila kujua sabaya alikua kikazi na kisheria dukani kwa huyo mwarabu. Aibu ni kwa dola kufungua kesi dhidi ya kada mahiri wa chama tawala wakati chama bado kipo madarakani.
Ngoja tuone.
 
mpaka sasa shahidi wa 4 ameshatoa ushahidi wake lkn bado sijaona Ujambazi/unyang'anyi alio ufanya Sabaya.
jambazi au mnyanganyi anawezaje kuwapeleka watu anao daiwa kuwapora Polisi?!
Mnyang'anyi anachukua machine ya kutolea risiti? ya nn?
n.k
ngoja tuendelee kusikiliza.
lln hapo hakuna cha unyang'anyi wala ujambazi.
Mmmmmmmmm labda uporwe wewe ndio utaona ujambazi
 
Back
Top Bottom