Kama hufanyi kitu hiki kimoja kila siku, una utapiamlo wa akili

Kama hufanyi kitu hiki kimoja kila siku, una utapiamlo wa akili

We jamaa unaongea tu bira kufikiria hari ya mtu kiuchumi, mazingira, kifamilia.

Yaani mimi niliyeko kijiji cha Chankabhagabho, nitakipatia wapi hicho kitabu cha kusoma kila siku, pia mazingira ya huku kijijini ni yakuamka na jembe la mkono una lala na jembe, hicho kitabu hata kikipatikana utakisoma saa ngapi unalala upo hoi.

Pia majukumu ya kutafuta kuni, maji ukateke mtoni tena kilomita za ajabu na utafute chakula, huo mda wa kushika kitabu utaupata wapi.
Nakukumbusha tu life is not fare. Kama ilivyo vidole vya mkono ndivyo tusivyo lingana kimaisha
 
Ndiyo mkuu,
Namaanisha kitabu kama kitabu.
Hizo njia nyingine unaweza kujifunza mengi na yenye manufaa.
Lakini kuna manufaa ya kiakili ya kusoma vitabu ambayo huwezi kuyapata kwa njia nyingine ya kujifunza.
Magazeti nayaweka kwenye kundi la junk food kwa akili, unachokipata huko hakina manufaa kiafya kwa akili.
Hapana mkuu hapa siungani nawe!!

Hivi nikisikiliza speech kutoka kwa watu kama Oprah , Obama, Kapiga,Nnauka nk kwenye semina mbalimbali sitakuwa na manufaa ya kiakili?


Umeelezwa vizuri sana kuwa siyo njia moja tu ya kunoa akili zipo nyingi usibishe!!
 
Lakini wakati huo huo unapata pesa za kununua vocha na kuweka bando kwenye simu kila siku.
Wakati huo huo unapata muda wa kubishana mambo mbalimbali yasiyo na tija kwako.
Wakati huo huo unapata muda wa kufuatilia maisha ya wengine.
And that is life broh!!

Hebu tusi complicate maisha, yote hayo ni sehemu ya maisha na yanaumuhimu wake, binafsi kusemwa , kumsema mtu huwa sioni kama ni tatizo, mfn mie nikisikia watu wananisema regadless ni positive au negative najifunza namna wanavyo ni perceive watu,kwangu inakuwa ni faida , pia kusemwa huweza kukufanya uache tabia fulani na ubadilike ,sioni shida, watu wanunue mabando tu kwa matumizi haijalishi ya namna gani.


Umbea unaondoa stress pia, ukutanapo na wenzio mnabadilishana mawazo then siku zinaenda.
 
akili za kichadema izi ushashiba mbaa sasa unaanza andika pumba

kusoma vitabu ni anasa, mshika jembe wa Kiranjeranje huwezimwambia afanye huo ujinga
 
We jamaa unaongea tu bira kufikiria hari ya mtu kiuchumi, mazingira, kifamilia.

Yaani mimi niliyeko kijiji cha Chankabhagabho, nitakipatia wapi hicho kitabu cha kusoma kila siku, pia mazingira ya huku kijijini ni yakuamka na jembe la mkono una lala na jembe, hicho kitabu hata kikipatikana utakisoma saa ngapi unalala upo hoi.

Pia majukumu ya kutafuta kuni, maji ukateke mtoni tena kilomita za ajabu na utafute chakula, huo mda wa kushika kitabu utaupata wapi.
Nakukumbusha tu life is not fare. Kama ilivyo vidole vya mkono ndivyo tusivyo lingana kimaisha
Acha visingizio vitabu hta online unavipata tena ni bure huitaji hta kulipia chochote zaid ya bando lako ....km umeweza kuwa na smart phone huwezi kushindwa ku download vitabu pitia hii website pdfdrive.com kuna vitabu ya 10000 vya bure.

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
We jamaa unaongea tu bira kufikiria hari ya mtu kiuchumi, mazingira, kifamilia.

Yaani mimi niliyeko kijiji cha Chankabhagabho, nitakipatia wapi hicho kitabu cha kusoma kila siku, pia mazingira ya huku kijijini ni yakuamka na jembe la mkono una lala na jembe, hicho kitabu hata kikipatikana utakisoma saa ngapi unalala upo hoi.

Pia majukumu ya kutafuta kuni, maji ukateke mtoni tena kilomita za ajabu na utafute chakula, huo mda wa kushika kitabu utaupata wapi.
Nakukumbusha tu life is not fare. Kama ilivyo vidole vya mkono ndivyo tusivyo lingana kimaisha
Mkuu, kama wewe ni Mkristo basi soma biblia kila siku.
Kama ni Muislam soma kuran kila siku.
Kuna ugumu gani kwenye hilo?
 
Hapana mkuu hapa siungani nawe!!

Hivi nikisikiliza speech kutoka kwa watu kama Oprah , Obama, Kapiga,Nnauka nk kwenye semina mbalimbali sitakuwa na manufaa ya kiakili?


Umeelezwa vizuri sana kuwa siyo njia moja tu ya kunoa akili zipo nyingi usibishe!!
Na hayo wanayoeleza kwenye hizo speech zao nzuri wameyatoa wapi?
Jibu ni vitabuni, wameyasoma kwenye vitabu na kuweza kuyawasilisha kwa namna tofauti.
Sasa kwa nini na wewe usiende kwenye chemchem ujichotee mwenyewe badala ya kusubiri upimiwe kwa kikombe?
 
And that is life broh!!

Hebu tusi complicate maisha, yote hayo ni sehemu ya maisha na yanaumuhimu wake, binafsi kusemwa , kumsema mtu huwa sioni kama ni tatizo, mfn mie nikisikia watu wananisema regadless ni positive au negative najifunza namna wanavyo ni perceive watu,kwangu inakuwa ni faida , pia kusemwa huweza kukufanya uache tabia fulani na ubadilike ,sioni shida, watu wanunue mabando tu kwa matumizi haijalishi ya namna gani.


Umbea unaondoa stress pia, ukutanapo na wenzio mnabadilishana mawazo then siku zinaenda.
Mkuu mbona tu unataka ubishi usio na manufaa kwa yeyote,
Sijamkataza yeyote kufanya hayo.
Ninachoshangaa ni mtu anasema hana muda wa kusoma vitabu wakati ana muda wa hayo mengine.
Point yangu ni kama husomi vitabu sababu pekee ni hitaki tu, maana yale yote unayotaka unapata muda wa kuyafanya.
 
Ndiyo mkuu,

Namaanisha kitabu kama kitabu.

Hizo njia nyingine unaweza kujifunza mengi na yenye manufaa.

Lakini kuna manufaa ya kiakili ya kusoma vitabu ambayo huwezi kuyapata kwa njia nyingine ya kujifunza.

Magazeti nayaweka kwenye kundi la junk food kwa akili, unachokipata huko hakina manufaa kiafya kwa akili.
Essence ya junk food ni nini katika tafsiri ya muktadha wa chapuo la kitibu? Hivi unafahamu wabobezi wa makala?
 
Lakini mkuu wewe umeamua kumtusi bure muandishi ,maarifa mengi yameandikwa kwenye vitabu na ndoo maana ukiprlekwa shule karika mfumo wa kawaida lazima ukute vitabu shuleni vya kujifunzia na kufundishia.

Lakini pia muandishi siku zote anasema ukiwa msomaji wa vitabu na ukaviweka kwenye matendo lazima ubadilike na ufanikiwe.Kwanini hao wazungu wanapenda kusoma vitabu? Kuna siri gani huko kwenye vitabu?

Hiyo inatuonyesha wenzetu washajua tukitaka kufanikiwa lazima tupate maarifa ya kitu fulani kupitia kwenye vitabu au kwenda shule kabisaa.Muandishi anatupa kitu kizuri tusipende kumbeza bali tupende kuwashawishi jamaa zetu na nduguzetu wapende kutafuta maarifa kutoka kwenye virabu.

Sent from my TECNO KA7O using JamiiForums mobile app

Kwa mara ya kwanza
Consigliere ameteleza mkuu!
Kukutana na new friends kila mara na kusoma vitabu bora usome vitabu!
 
Essence ya junk food ni nini katika tafsiri ya muktadha wa chapuo la kitibu? Hivi unafahamu wabobezi wa makala?
Mkuu,
Soma makala upendavyo, lakini tambua vitabu vina sehemu yake na manufaa yake makubwa.
Maana hata anayeandika makala, anafanya utafiti kwa kusoma vitabu.
Huwezi kulinganisha makala yoyote ile na kitabu.
Hivyo tuweke kipaumbele kwenye usomaji wa vitabu, pamoja na kutumia hizo njia nyingine za kujifunza pia.
 
We jamaa unaongea tu bira kufikiria hari ya mtu kiuchumi, mazingira, kifamilia.

Yaani mimi niliyeko kijiji cha Chankabhagabho, nitakipatia wapi hicho kitabu cha kusoma kila siku, pia mazingira ya huku kijijini ni yakuamka na jembe la mkono una lala na jembe, hicho kitabu hata kikipatikana utakisoma saa ngapi unalala upo hoi.

Pia majukumu ya kutafuta kuni, maji ukateke mtoni tena kilomita za ajabu na utafute chakula, huo mda wa kushika kitabu utaupata wapi.
Nakukumbusha tu life is not fare. Kama ilivyo vidole vya mkono ndivyo tusivyo lingana kimaisha
Kwa aina hii ya akili nakushauri soma hata maphlet mkuu! Pls
 
Andiko zuri sana, lakini nafikiri msisitizo ungekua kujifunza jambo jipya bila kujali unatumia njia gani, inaweza kuwa kupitia mazungumzo na mtu mmoja mmoja, kuhudhuria semina, warsha na kujiendeleza kwa kujiunga kwenye kozi fupi kuongeza maarifa.

Vitabu ni njia bira na rahisi lakini sio njia pekee na inaweza isiwe rahisi kwa kila mmoja wetu kwa sababu tofautitofauti.

Jambo la msingi, hakikisha unaongeza ujuzi na maarifa kila siku kadri muda unavyoruhusu.
Kweli kabisa sio kusoma vitabu pekee bali ni kujifunza. Mimi kwa aiku hizi najifunza sana kupitia YouTube kuliko vitabu

Hata kutembelea watu wanaofanya vitu vipya na unavyopenda inakuongezea maarifa.

Kuna njia nyingi sana za kulisha ubongo, vitabu ni mojawapo
 
Rafiki yangu mpendwa,

Hata uwe umetingwa kiasi gani, kila siku lazima utenge muda na kula chakula. Sijawahi kukutana na mtu anayesema kwa wiki nzima hajala chakula kwa sababu hajapata muda.

Huo ni upande mmoja wa kulisha mwili wako. Lakini upo upande mwingine wa kuusafisha. Kila siku lazima uusafishe mwili wako na kuuvalisha mavazi ili kuusitiri. Hujawahi kutoka nyumbani ukiwa uchi kwa sababu huna muda wa kuvaa.

Ni muhimu kwako kula kila siku na hivyo unatenga muda wa kula, hata iweje huwezi kutotenga muda huo. Ni muhimu kwako kuoga na kuvaa nguo kila siku na hivyo unatenga muda wa kufanya hivyo. Pamoja na kulalamika mambo ni mengi na muda ni mchache, hujawahi kukosa muda wa kufanya hayo muhimu kabisa kwako.

Lakini kipo kitu kimoja chenye umuhimu kwako kama hivyo viwili nilivyoshirikisha hapo juu, ila umekuwa hukipi uzito wa kutosha.
Kitu hicho ni kulisha na kusafisha akili yako.

Kama unavyoulisha mwili wako chakula, unapaswa pia kuilisha akili yako chakula. Na chakula cha akili ni usomaji wa vitabu. Kama unavyousafisha mwili wako na kuuvalisha mavazi, ndivyo pia unapaswa kuisafisha akili yako na kuivalisha. Chakula na mavazi ya akili ni usomaji wa vitabu.

Kwa maana hiyo basi, kama husomi vitabu maana yake unatembea na akili yenye utapiamlo. Kama husomi vitabu unatembea na akili chafu na iliyo uchi. Haishangazi kwa nini matatizo na changamoto mbalimbali zinakuandama.

Mwili ukikosa chakula unakuwa dhaifu na kushambuliwa na magonjwa mbalimbali. Akili ikikosa maarifa inakuwa dhaifu na kudhambuliwa na changamoto mbalimbali. Kama unataka kuwa imara, iweze kukabiliana na kila aina ya changamoto inayokuja kwako na kuishinda, basi lisha akili yako maarifa sahihi.

Abraham Lincoln amewahi kusema akipewa masaa 6 ya kukata mti, atatumia masaa manne kunoa shoka lake. Kwa sababu anajua shoka likiwa kali, kazi itakuwa rahisi. Shoka ni akili yako, inoe kupitia usomaji ili uweze kufanya vizuri kile unachofanya.

Na jenerali Jim Mattis akasema kama hujasoma mamia ya vitabu ni sawa na mtu asiyejua kusoma na kuandika, utakuwa dhaifu na changamoto zitakuangusha kwa sababu uzoefu wako mwenyewe haukutoshi kupambana kwenye haya maisha.

Mimi mwenyewe, kutoka ndani ya nafsi yangu, huwa ninaamini kabisa mtu ambaye hasomi vitabu ana mtindio wa ubongo. Haiwezekani mbele yako kuwe na njia ya uhakika kabisa ya kukusaidia kupata unachotaka halafu huitumii na ukawa na akili sahihi.

Ujumbe mkuu hapa rafiki yangu ni soma vitabu. Siri za mafanikio zimefichwa kwenye vitabu. Changamoto yoyote unayokabiliana nayo sasa majibu yake yako kwenye vitabu. Hamasa unayohitaji ili kujituma zaidi kila siku ipo kwenye vitabu.

Usikubali kuendelea na maisha ya sasa ambayo yanakuwa magumu kwako kwa sababu hujanoa shoka lako. Usikubali kuendelea kujipa sababu kwamba husomi vitabu kwa sababu huna muda wa kusoma, unao sana au huna fedha za kununua, vingi unavipata bure kabisa.

Kila siku soma angalau kurasa kumi za kitabu. Kurasa nne unapoamka, kurasa tatu unapokula mchana na kurasa tatu kabla hujalala.
Kama huwezi kusoma kurasa 10 tu za kitabu kila siku, mbegu ya mafanikio makubwa haipo ndani yako na utataabika sana na haya maisha.

Karibu upate vitabu mbalimbali vya kusoma kwa kufungua www.amkamtanzania.com/vitabu na www.t.me/somavitabutanzania

Na kama unahitaji kusimamiwa kwa karibu ili uweze kusoma vitabu na kuyatumia maarifa unayopata kuboresha maisha yako, tuwasiliane kwa wasap 0717 396 253.

Rafiki yako anayekupenda sana,

Kocha Dr Makirita Amani.
wewe ni mjinga kama wajinga wengine tu na waganga njaa wote ndio mlivyo;
hivi vitabu unavyosema watu wasome ni vitabu gani hasa?,
vya nini?,
lengo la kusoma kitabu ni nini?,
chukulia mtu anasoma vitabu vyako hivyo vitamsaidia nini?,
mbona umekua mjinga kiasi hiki?,
najua hii ni biashara ila usiaminishe watu huo ujinga wa kusoma mawazo ya watu tu eti ndio umeshibisha akili,mimi namthamini mtu atakayeenda shambani kwa mkulima kuangalia anafanya nini kupata mazao bora kuliko msoma vitabu vyako;
acha kudanganya watu;
 
I beg to differ,chakula cha ubongo sio kusoma vitabu tuu.Vitabu ni njia moja wapo yakupata maarifa ila sio pekee.Vitu kama documentaries,kuongea na watu wenye maarifa,baadhi ya miziki na filamu,hotuba nk.vyote hivi hulisha ubongo. Hata hivyo hongera kwa chapisho lako na hata machapisho yako mengine yana vitu vya kujifunza.Ubarikiwe.
 
Kweli motivational speakers are born not made,mkuu huwa huchoki,huboi wala hupoi
😂😂
Ukishajua moto unaowaka ndani yako, hakuna anayeweza kuuzima.
Ukiwa umefanya kitu kazi na kikakupa matokeo, huwezi kumwelewa anayekipinga kwamba hakifanyi kazi wakati wewe mwenyewe ni shahidi.
Ndiyo hivyo tu mkuu.
 
Magazeti na majarida mbalimbali yalipoanza kuchapwa kwenye karne ya 18, watu walisema ndiyo mwisho wa vitabu.

Redio zilipoanza karne ya 19 watu wanasema ndiyo mwisho wa vitabu.

TV zilipoanza karne ya 20 watu wanasema ndiyo mwisho wa vitabu.

Na mitandao ya kijamii ilipoanza karne ya 21 watu wanasema ni mwisho wa vitabu.

Lakini katika nyakati zote hizo, vitabu vinesurvive, teknolojia zimekuja na kupita, vitabu vimebaki.

Hiyo inaonesha kuna kitu kipo kwenye kitabu ambacho huwezi kukipata sehemu nyingine yoyote ile.

Chukua mfano wa kitabu THE ART OF WAR au TAO TE CHING, vitabu vyenye miaka zaidi ya elfu tatu halafu niambie ni channel gani

YouTube unaweza kupata Madini kama yake?

Na uzuri ni kwamba, wale wanaotoa maarifa kwenye mitandao ya kijamii, wanayachimba kutoka kwenye vitabu.

Sasa kwa kuwa wengi siyo wasomaji, wanaona ni vitu vipya sana.

Tusome vitabu, kuna hazina kubwa huko ambayo huwezi kuipata sehemu nyingine yoyote.
Binafsi nakuelewa sana mkuu.
 
Back
Top Bottom