Kama kawaida ya madaktari, huwa hawapendi kuguswa

Kama kawaida ya madaktari, huwa hawapendi kuguswa

Mimi sio daktari ila kushangilia mwenzako anapokosa ulaji ni dalili za uchawi na umaskini.
Mkuu, assume mpo kwenye project, kuna makundi 3 ambayo kila mmoja ana part yake ya kufanya, lakini uzito wa kazi ni almost the same japokuwa haufanani, umezidiana kidogo tuu.

Kwenye malipo mnapewa fungu 1 kisha ndiyo mnagawana, lakini kundi moja likajiwekea % kubwa kushinda wengine kwa sababu wao ndiyo wameshikilia mpini nyie mmeshikilia makali.

Katika situation kama hiyo hayo makundi mengine yaki-raise concerns zao watakuwa wanawafanyia uchawi hilo kundi lililojipendelea ama watakuwa wanaomba kuwe na fair distribution ya hilo fungu lililotolewa?
 
Lile sakata la kufutwa gharama za kuonwa/kuhudumiwa hospitali na wahudumu linazidi kuchanja mbuga. Kwanza tuwekane sawa hapa, haiitwi gharama ya kumuona daktari, inaitwa "Consultation Fee" ikimaanisha "Gharama ya Kuhudumiwa" kwa maana utapita mikono ya wataalamu kadhaa siyo daktari tuu.

Baraza lao wanadai hii pesa huwa inaenda kwenye mfuko wa hospitali. Lakini hii ni danganya toto kwani hali ni tofauti kwa upande wa mifuko ya bima.
View attachment 2322322

Sasa ngoja tusanuane, kwa wale wasiojua. Suala la hii gharama ni kweli inaingia mfuko wa hospitali, lakini ni kwa wagonjwa wanaolipa cash tuu. Consultation fees za mifuko ya bima ina mgawanyo tofauti ambao umekaa kiunyanyasji wa hali ya juu sana.
Consultations fees za bima zote, hospitali inachukua 40%, daktari naye anachukua 40%, wauguzi wanachukua 15% na 5% inayobaki wanachukua wengine kama maabara na wahudumu wa afya.

Sasa ukiangalia hizo % hapo juu unaweza ukaona kama ni kitu kidogo, lakini ngoja niweke figure halisi ndiyo utajua hawa madaktari ni kwa jinsi gani wameweka mfumo wa kitumwa kwa kada zingine wanazoshirikiana nao.
View attachment 2322344
Huo mfano hapo juu ni wa consultation fee ya NHIF ambayo ni 25,000/=. Hospitali inachukua 10,000/=, Daktari anachukua 10,000/=, Muuguzi anachua 3,500/= na wengine wanaobaki wanagawana 1,500/= iliyobaki.

Ndiyo maana nasema hii ni janja janja tuu ya siku zote. Kwanza wale wanaolipia cash, consultation fee mara nyingi ni 10,000/= tuu. Hivyo bima ndizo zina consultation fee kubwa na ndizo hizo madaktari wakajitungia ka utaratibu ka kujikwapulia kiasi sawa na hospitali, huku wakiwabakizia wengine kiduchu.

Nimewahi kuleta uzi humu nikielezea ni kwa namna gani hawa madaktari wamejijengea ka empire kwenye sekta ya afya kiasi kwamba hawataki wengine nao waifurahie hii sekta. Wamejimilikisha sekta ya afya utadhani wako peke yao.


Hivyo waziri unapoenda kukaa nao chini kaa nao chonjo sana, wanaweza wakapendekeza consultation fee za cash ndizo zifutwe lakini za bima zisifutwe kwa sababu wao wanafaidika nazo.
Umeongea upumbavu tu.. yaan kwa hako kamshahara unachomlipa daktar ka 1.5m ndo unaona asipigie kelele maslah kuzid pungua.. hiv ushawai enda hospital ukaona jins hao watu wanavyopiga kaz.. unadhan ni sawa na vikaz vyenu uchwara mnaenda ofisin mnakunywa chai . Lunch then kwaheri... Acha watu wapambanie maslah yao kama nyie wengne mmeridhia kuwa misukule sawa endeleen
 
Vita ya ma Dr na kada zingine za afya haijawahi kupata suluhisho
 
Natamani kuona mkeka wa posho za sekta zote za umma.
Na posho zote hizi, bado wengi wanababaisha. Dah!
 
Mkuu, assume mpo kwenye project, kuna makundi 3 ambayo kila mmoja ana part yake ya kufanya, lakini uzito wa kazi ni almost the same japokuwa haufanani, umezidiana kidogo tuu.

Kwenye malipo mnapewa fungu 1 kisha ndiyo mnagawana, lakini kundi moja likajiwekea % kubwa kushinda wengine kwa sababu wao ndiyo wameshikilia mpini nyie mmeshikilia makali.

Katika situation kama hiyo hayo makundi mengine yaki-raise concerns zao watakuwa wanawafanyia uchawi hilo kundi lililojipendelea ama watakuwa wanaomba kuwe na fair distribution ya hilo fungu lililotolewa?
Anyway nimejaribu kusoma replies zako nyingi naona kuna vitu sijui wewe unavijua zaidi kwa kuwa ni idara yako. Kwa namna unaandika kuna chances unaumizwa sana na hii issue, pole sana na nakuombea upate posho zaidi.

Ila nikushauri kitu kidogo tu, sehemu za kazi mara nyingi haziko fair. Huwa ziko fair kwa wateule wachache sana.

Kwa kusema hayo nakushauri utafute namna ya kupata kipato nje ya ajira yako. Tengeneza ka side hustle flani kufidia gaps za namna hii.

Fikra zangu zinanituma ulitaka kuwa daktari sema issue za cutoff zikakutoa nje ya mchezo na ukizingatia ada za vyuo vya pvt ni kubwa pole sana na ufanye kazi kwa moyo mweupe na make sure unapata pesa nje ya eneo lako la kazi.

Mfumo yetu ya ajira ni mibovu mno hata hao MDs mshahara tu wanaolipwa bado uko chini ya kiwango achilia mbali hizo posho tunazodebate hapa.

Na hii sio kwenye kada ya afya tu, ni almost kada zote kasoro kwenye siasa.

Ahsante.
 
Ni wapi au muongozo gani umeandikwa kwamba utendaji kazi wa muuguzi au mfamasia au maabara unamtegemea daktari?[emoji1]

Wewe uko pale kutimiza wajibu wako, na wengine wako pale kutekeleza wajibu wao. NO ONE HAS AUTHORITY TO COMMAND OTHERS.

Na unachofanya wewe everyone ana knowledge nacho, ni protocols tuu zimewekwa kwamba huyu afanye hiki na hiki, na yule afanye kile na kile, basi.

Na ndio maana wewe ukiandika wrong dose, kisha muuguzi akai-execute jinsi ilivyo, basi anakuwa yuko responsible yeye na sio wewe kwa sababu nyote mmesoma kile kitu na mmoja akikosea basi mwenzako anatakiwa akurekebishe.

So, usidanganye umma kwamba nyie ndio ma generali na wengine ma kuruta.
Ingekuwa ni hivyo kusingekuwa na hiyo tofauti mkuu.. inaonekana hata mipaka yako ya kazi hujaijua vizuri, ungeijua usingekuja kulalama hapa
 
Mleta mada umeleta mada nzuri lakini umeamua kupotosha mambo kimakusudi. Ngoja tuweke pia ufafanuzi mwingine kutoka kwa wahusika wenyewe (NHIF na Jumuiya za Madaktari).

1. Consultation fee ni gharama ya kuonana na Daktari kimatibabu. Bila Daktari kukuona na kukuhudumia yeye mwenyewe NHIF haiwezi kulipa. Hivyo Daktari ndio anatumika kuingizia hospitali pesa kupitia medical consultation fee. Sio ajabu Daktari akilipwa 40% ya malipo hayo kwa kuwa bila uwepo wake na utaalamu wake kutumika basi hospitali haitaambulia hata senti tano. Kada zingine zozote kama uuguzi nazo zinapokea sehemu ya malipo hayo ya Medical consultation fee kutoka NHIF japokuwa hazihusiki moja kwa moja kutoa hiyo huduma.

2. Medical consultation ndio udaktari wenyewe, ndio kazi kuu ya Daktari na ndio jukumu kuu la madaktari wote duniani. Na hicho ndio NHIF inakilipa. Kiuhalisia kada nyingine yoyote haipaswi kulipwa hata senti tano kutokea kwenye medical consultation fee.

3. Daktari amezungukwa na kusaidiwa na watu wengine hususani kada ya uuguzi ili kufanikisha suala zima la medical consultation kiufanisi, na hivyo NHIF inatoa mgawanyo mwingine kwa kada zingine, lakini mgawanyo huo kamwe hauwezi kuwa sawa na mgawanyo mkuu wa Daktari.

4. NHIF inalipa pia gharama za huduma zingine ikiwemo vipimo vya maabara, vipimo vya radiolojia, Dawa, kulazwa, kusafishwa vidonda, upasuaji nk. Kada husika kama uuguzi, maabara, ufamasia nk. zinaweza kufaidika moja kwa moja na mapato hayo kulingana na mgawanyo waliojiwekea ndani ya hospitali husika.
 
Back
Top Bottom