Kama Kipimo kina matatizo wa kuwajibishwa ni Msimamizi wa Maabara au TBS?

Kama Kipimo kina matatizo wa kuwajibishwa ni Msimamizi wa Maabara au TBS?

Mkuu ninavyofikiria mimi hivi vifaa ni kutoka nchi za wenzetu. Ko hata hao TBS watalaumiwa bure, inawezekana ukaagiza kifaa na ukaambiwa specification yake ni kupima covid 19 kwa binadamu tu. Sasa sijui kwa akili ya kawaida kama utaanza kupima na ambavyo hujaambiwa.
 
Kwanini kila kitu nchi hii lazima wanasiasa ndo wanaumiza wataalamu..wanawapangia cha kusema wanawapingia cha kufanya....where are we heading as a nationa?
Wataalam wachache halaf hawadhaminiwi. Unafikiri watakuwa na moyo wa kufanya kazi kwa bidii kwa style hii?
Sisemi kuwa wadekezwe hapana. Panapo onekana uzembe wawajibishwe.. lakin si kwa sababu za kisiasa... ziwe za kisayansi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtumiaji ndie anawajibika sababu ndiye aliyeagiza na kutoa specification kuwa ziwe hivi na hivi na hivi mfano Wewe in afisa Wa wizara ukaagiza gari used Japan kwa ajili ya ofisi TBS watalipitisha kuwa liko sawa kivumbi utakutana nacho ofisini kwako sababu sheria ya manunuzi hairuhusu kununua gari used!!! Hapo sio kesi ya TBS in yako Wewe mtumiaji
Aliagiza kivipi?
 
Labda mkuu alitaka hizo mashine zitoe majibu kuwa kilichopimwa ni papai, kondoo, mbuzi, nk.
Ilitakiwa kuangalia kama specifications zilizingatiwa wakati wa manunuzi ya mashine. Vinginevyo waliosimamishwa kazi wameonewa maana walisoma matokeo yalyoonekana kwenye mashine.
 
Mtumiaji ndie anawajibika sababu ndiye aliyeagiza na kutoa specification kuwa ziwe hivi na hivi na hivi mfano Wewe in afisa Wa wizara ukaagiza gari used Japan kwa ajili ya ofisi TBS watalipitisha kuwa liko sawa kivumbi utakutana nacho ofisini kwako sababu sheria ya manunuzi hairuhusu kununua gari used!!! Hapo sio kesi ya TBS in yako Wewe mtumiaji
Unatetea usenge hadi unaboa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
HTP umelia sana mkuu, na bila shaka umeumizwa sana kama wengi wengine wanavyoumizwa wanapoona mambo ya nchi yao yanakwenda shaghala baghala kila sehemu, na wanaoyasababisha mambo yawe hivyo wakijulikana na hakuna njia yoyote ya kuwawajibisha.

Wakati wote na sehemu zote ni lazima pawepo na 'Bhangusilo' mkuu, na hiyo huumiza sana inapokuwa bhangusilo hao ni matokeo ya upuuzi wa mtu mmoja tu kwa kufanya mambo yake nje ya taratibu zilizopo kwa kujisikia tu kwamba yeye anataka iwe hivyo hata kama hakuna ushahidi wowote wa matokeo yaliyokwishaonyeshwa na njia anazotaka yeye mambo yafanyike. Huyu mtu mmoja sasa ndie anayeshikilia uhai wa raia zake wote.

Hali hii ndio halisi ya taifa letu sasa, na hatutaenda popote wakati mambo yakiendelea hivi hivi.

Nikiangalia aya yako ya kwanza, unalia sana. Watu wenye elimu zao na wanaotaka kufanya mambo katika taratibu zinavyotakiwa katika maeneo yao, wanalia, hawajui wafanye nini.
Ushauri kwao wote, ni lazima, tena mhimu kabisa kufanya kazi ndani ya taratibu ya ujuzi wao walio nao na kazi zao zinavyoelekeza bila kumjali mtu mwingine yeyote toka nje, hata awe na cheo cha kumkaribia mungu au shetani.

Ukitimiza matakwa ya ujuzi wa kazi yako, hakuna sababu ya kuogopa chochote.
Tatizo la wasomi wetu sasa hapa Tanzania ni hili hili linalokuliza - njaa. Siasa imekuwa kila kitu na ndio sababu wataalam wetu mnapata taabu sana, kwa sababu mnajipendekeza kwa hao hao wanasiasa mpate fadhira na mjaze matumbo yenu, na ujuzi wenu mlioupata mnauweka pembeni

Kama si hivyo, kwa nini ulie sana namna hii mkuu wangu huku ukijua ujuzi unao, na kazi utafanya sehemu yoyote nchini au duniani?

Kwa hiyo, katika hili la kutumbuliwa kwenu, binafsi sina huruma nanyi, kwa sababu nyinyi mmekuwa sehemu ya tatizo kwa kujikomba komba kwenu ili mpate uteuzi na kusahau matakwa ya kazi zenu.

Sehemu ya pili ya mada yako.

Hapa pia wataalam hao hawawezi kujitoa moja kwa moja kwenye lawama, ingawaje sehemu yao ya lawama ni ndogo; na inawezekana pasiwepo na lawama kabisa. Nitaeleza.

Maabara yoyote ile inazo taratibu zake za kupokea sampuli, kufanya vipimo na kutoa majibu ya vipimo.
Sampuli zimeletwa toka nje ili zifanyiwe vipimo.
Kosa linaweza likatokea katika mfumo wa kukabidhiana/kupokea sambuli hizo na utambulishi wake. Sasa hapa sijui taratibu za maabara husika ni upi.
Je, kuna uwezekano wa kuvurugwa taratibu za kupokea sampuli hizo, kiasi cha kuvuruga na kupenyeza zisizohusika? Hili niliache likining'inia, kwa sababu sijui utaratibu kwenye maabara hiyo upoje. Lakini hapa ndipo panapoweza kuwa na udhaifu unaoweza kuwapa watumbuliwa lawama.

Vipimo, sioni tatizo kubwa katika eneo hili, kwa sababu aina ya vipimo vinavyofanyika hapa ni kufuata 'protocol' tu na hakuna mambo mengi ya mtu kuingiza makosa katika upimaji.

Ubora wa vipimo - hili haliwezi likawa kosa la waliotumbuliwa, kwa sababu wao hawahusiki katika kujua ubora wa vipimo hivyo.
Wahusika hapa wala sio TBS, bali wale wa madawa na vifaa vya afya.

Kwa hiyo kwa kumalizia ni kwamba, hawa waliotumbuliwa ni bhangusilo tu, uzembe upo sehemu nyingine kabisa.
Lakini siwezi kuondoka bila kulisema hili: kulikuwa na sabau gani ya kutafuta sampuli za mapapai, mbuzi, mafenesi,n.k.; vitu visivyoshabihiana kabisa na aina ya vipimo vinavyofanyika? Angalao hata wangechukua sampuli ya maji.
Usahihi zaidi, huo aliyekuwa na mashaka na ubora wa vipimo, alitakiwa achukue sampuli toka kwenye watu ambao wanajulikana hawana tatizo lolote la Coronavirus, na kuziwasilisha zipimwe. Majibu ya hizi kama ndio yangetokea na ugonjwa, ingekuwa alama sahihi ya kujua kuwa vipimo haviko sawa.

Lakini inaeleweka kwa nini ilifanyika hivi, kwa sababu tunaye mtu anayeamini kwamba yeye anajua kila kitu. Na alikuwa tayari na lengo lake akilini kwa nini ifanyike hivyo.

Mbona sampuli hizo hizo hakuziwasilisha kwenye maabara nyingine, hata nje ya nchi, ili fahamike wazi kuwa ni hizi hizi za kwake tu ndio zenye matatizo?

Waziri wa Afya na watu husika walipaswa kuwa walishajiuzuru, sio kwa tatizo hili la vipimo, bali kwa mambo mengi mengine yaliyotokea katika wizara hiyo.
 
Hii nchi ni bora uwe businessman or Businesswoman kuliko kujichanganya kwenye siasa angalia wataalamu wanavyofanywa sasa na wanasiasa its a shame, watu wabiashara tunasumbuliwa na authorities ila sio kwa kutiana aibu hivi, kulambana miguu tu
 
Hii nchi ni bora uwe businessman or Businesswoman kuliko kujichanganya kwenye siasa angalia wataalamu wanavyofanywa sasa na wanasiasa its a shame, watu wabiashara tunasumbuliwa na authorities ila sio kwa kutiana aibu hivi, kulambana miguu tu
We achatu
 
Wrong sample lazima upate unexpected results!!

Kipimo cha COVID-19 hakijatengenezwa kupima content ya sugar kwenye matunda kama papai ama fenesi hapana..

Uzuri wa sayansi huwa haidanganyi....hata hizo kits zina Technical specifications.!!

Tutajua mengi ni suala la kamda kadogo tu!!
 
Shida ipo
Kumbukeni hiki kifaa si Tz pekee kimeleta balaa
Tunamheshimu raisi ila wataalam wakitumiwa kwa nafasi zao itapendeza sana
Huyu tunayeona anaongelea vitu vya maabara leo alituambia tusitishane,tuombee taifa kwa siku 3
Tutatuma ndege Madagascar ilete dawa
Mambo mengi ya kitaalamu yeye ndo msemaji
Kulikua na haja gani ya task force ya Covid-19?

Tutaona sana mauzauza


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna mengi nyuma ya pazia....!! Hata kusepa chato kuna watu walipanga apate maambukizi ya korona by any cost, anyway mambo ni meng mda hautoshi , huenda kuna dili nyingi zimefanywa kupitia MSD , maana mkuu wa MSD ana free entry zake amabazo anaweza kufanya bila mamlaka zingine kumgusa
Hata kukiwa na mengi nyuma ya pazia je unataka kutuambia Israeli naye anachukua watu kwa kufuata vipimo vya maabara, kwamba kipimo kikisema +ve anakutoa roho hata kama maabara imekosea. Maana kama maabara ilikuwa haitoi majibu sahihi watu wasingekuwa wanakufa kwa mpigo kama tulivyoshuhudia safari hii. Serikali yenyewe inajua kwamba watu wanaondoka kwa wingi ndio maana ikaja na wazo la kuwazika watu usiku ili isiwatie watu hofu kama inavyosisitiza. Error za maabara zipo lkn sio kwa kiasi ambacho tunaaminishwa lasivyo ununio isingepata umaarufu huo kwa muda mfupi kipindi hiki cha gonjwa la corona.
 
Mh Ummy, nakuhakikishia Mungu yupo hilo lielewe kabisa.. Najua kama binadamu unafanya mambo ili kumfurahisha anayekupa ugali na tabasamu, ila tambua Mungu alisema, AMELAANIWA MTU YULE AMTEGEMEAYE MWANADAMU na KUMFANYA KUWA KINGA YAKE.

Hivi tujiulize tu, hao watu wanaokufa na kuzikwa usiku wanakufa na ugonjwa gani??? Kama kweli Mkuu wa kaya na Ummy wangekua wanajali na ni watakatifu kiasi hiki cha kudhalilisha na kunyanyapaa ELIMU za watu walizosotea kwa miaka, KWANINI WASINGEKEMEA HADHARANI na kukutaza watu kuzikwa gizani? Kwanini WASINGETOKA HADHARARI WAKASEMA HAWA WATU WAMEKUFA KWA CORONA ila tutawazika kwa heshima?? Kwanini wao wanaficha kabisa Mambo yaliyoko wazi? na sasa wanamdhalilisha Msomi kisa vimetoka visa 480 ambavyo pia mambo yamefunikwa funikwa sana???? Kwanini hawa watu ni WAKATILI KIASI HIKI?? MUNGU TUNAKUOMBA HEBU TUSAIDIE HILI TAIFA NI LAKO.

Nirudi kweye Mada;

Kama Vilipimo vimeonyesha Fenesi lina Virusi, papai na Mbuzi, ambapo samples zilipelekwa kwa SIRI inamaana kuna shida kwenye Vipimo vyenyewe!! Huyu mtu angejua ni Fenesi labda hata angejiongeza kusema haiwezekani fenesi lisome + lakini maskini ya MUNGU hajui chochote anasoma kilichopo kwenye Mashine!!!!!! SASA KOSA LAKE NININI???? KWANINI ANAYESHUGHULIKA na MASWALA YA UBORA ambaye ni TBS asibebe hizi lawama kuruhusu bidhaa feki tena katika secta sensitive kama afya Ziingie NCHINI???.....Kwanini kila SIKU mambo yakienda vibaya lazima atafutwe MBUZI wa kafara??? Tena mara nyingi anatolewa ISAKA ambaya hana hatia yoyote???..MUNGU NAOMBA UFALME WAKO UJE TANZANIA MWAKA HUU KILA MTU AJUE UPO.......Naomba mwenye moja ya majibu ya mwaswali yangu anisaidie majibu.
Huyu Mama ni mtu hatari sana...
Mungu yupo kwani yote yatapita

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom