Kama kuna Rais anayetafuta legacy ya kudumu asimamie mipango miji

CCM na serikali yake ndio imeiharibu mipango miji ya nchi hii open space zote za dar ni za viongozi playing grounds zote za dar za wakubwa madiwani wanaharibu mipango miji ktk halmashauri zao petrol stations kila mahali makanisa kila kona baa kila uchochoro

Sasa hivi hawapangi tena miji wanarasimisha kuna barabara mpaka za mita 3 hakuna tena viwanja vya wazi wala michezo pia makaburi naipongeza CCM na wizara ya ardhi kukosa maarifa.
 
Ukiwaangani kwenye ndege wakati wa kutuq airport ya Dar es Salaam, huwa najihisi natua kwenye zizi la ng'ombe jinsi nyumba zilivyojengwa kiholela
 
Mji ukishakuwa kama huu kwenye picha hayo maji unapitisha wapi ?? Miundombinu yote ya maji ,umeme,cable ,gesi n.k yote inatakiwa kupita katika hifadhi ya barabara kama hakuna usitarajie kupata huduma bora
 
Kukisha kuwa na mpangilio mzuri
Hata kusambaza mabomba ya maji safi ni rahisi

Ova
 
Uko sahihi Ndugu, Kitengo cha Udhibiti Majenzi (Development control) nacho ni Changamoto, Mipango ipo, ila wasimamiaji wa Utekelezaji wa Hiyo Mipango ndio Changamoto.

Kuna Maeneo Watu mpaka wana Vibali vya Ujenzi na Wakati Hapakuruhusiwa Kujengwa.
 
Halafu iweke sheria kwamba ni marufuku kujenga kwenye eneo ambalo halijawekwa kwenye mpango mji.

Kisha serikali ikawa inawahi maeneo ambayo hayajajengeka na kuyapima na kuyawekea ramani
Kasi ya Uendelezaji wa Ardhi ( Ujenzi hususani wa Makazi) ni kubwa kuliko Kasi ya Serikali kupanga na Kupima.

Utaratibu ulipaswa kuwa Hivi;
1. Eneo Linapangwa
2. Panapimwa
3. Panawekewa Miundombinu ya Barabara
4. Panawekwa Huduma za Maji, Umeme n.k
5. Unamilikishwa
6. Unapewa Kibali cha Ujenzi
7. Unajenga.
Kote unako ona Mji unapendeza Kulitumika Huu utaratibu. Ambao ndio nimesema ili ufanikiwe kwanza unahitaji Fedha, na Usimamizi Makini, Jambo ambalo sio Kipaumbele cha Serikali.

Sasa sisi Maeneo Mengi tunaanzia Mwisho kwenda Mwanzo kwa Mtiririko huu;
1. Nunua Eneo (Shamba au Kipande cha Ardhi kisichopangwa)
2. Unajenga Nyumba
3. Unavuta Umeme na Maji
4. Unapanga ( Kwa kua ulisha jenga Kiholela kwaiyo kinacho fanyika ni URASIMISHAJI)
5. Unapima
6. Barabara zinachongwa (Sasa hizi ndio zile Za upana wa Mita 3, Kwakua mlishajenga Kiholela.)
7. Unamilikishwa
Hapo usitarajie kupata Mji unaoeleweka.

Ili Mambo yaweze kwenda Serikali ni Lazima Iwekeze kwenye Kupanga Miji yake. Utapiga watu marufuku wasijenge eneo ambalo Halina Mpango Mji, Sawa, Sasa unajiuliza Umepanga Hayo maeneo?
 
Na cha ajabu zaid unaeza kwenda baadhi ya vijiji ukakuta vimepangwa vizuri sana kukiko mijini na cha ajabu zaid ni kuwa watu wa kule hawana elimu kubwa lakin wanatunza ustarabu
 
kwenye mipango miji.

Dawa ni Waanzishe serikali za majimbo na ni legacy nzuri, kuwapa uhuru ili suala hili dogo la mipango miji walitekeleze wenyeji wa maeneo husika badala ya kumtegemea rais ambaye ana majukumu mengi.

Hatuwezi kutegemea rais kwa maamuzi hata ya kupanga mitaa, mifereji ya maji taka, mabomba ya maji safi salama, kutega maeneo ya misitu na mapumziko, shule kuwa na viwanja vya michezo n.k mambo ni mengi kumtwisha rais afanye hata mambo ya ngazi za mikoa au majimbo.
 
Kujenga inatakiwa upewe kibali na ramani ipitishwe ila hapo tutaibua tatizo la rushwa yani dah tupo shimoni sana sisi
 
Sisiemu imejaa wapumbavuu tupu unategemea nini ....wanajenga mji bila hata kuweka level eneo la ujenzi tizama hata chuo cha dodoma ni kuchimba tu na kuinua magorofa.mfano kigamboni ilitakiwa kabla ya kujenga eneo lote lipimwe na kuwekwa tambarare
 
Utasambazaje maji safi na salama kiufanisi bila mipango miji mizuri mji unapangiliwa ili kuwezesha na hayo uliyo sema yafanyike kwa ufanisi
 
Vijana tunaowaza kama wew ni wachache mno. Wananchi wanajitaidi sana kupambana na umaskini ila swala la mipango miji linatufanya tuonekane wote hatuna akili. Mipango miji iwe agenda ya kitaifa.
 
Vizuri sana ndugu! Kama kuna jambo nachukia nchi hii ni kushindwa kupanga miji yetu! Walipoishia wakoloni ndipo palipopangwa vizuri baada ya uhuru ni vululuvululu tu.
 
Umeongea Vizuri sana!! Nitoe ya kwangu ya Moyoni, mimi ni mkaazi WA DSM, huwa natembea maeneo mengi sana kutokana na shughuli zangu, kikubwa kinachonisikitisha ni Serekali kufumbia macho mji kuendelea kukua kiholela!! Kweli nchi imesomesha maofisa WA mipango miji, Kuna Tamisemi, Kuna wizara ya Ardhi, Kuna Tarura, Kuna Tanroads, huwa najiuliza Hawa watu mindsets zao kichwani zimekaaje!? Waziri WA Ardhi anapita Huku akijisemea viwanja vya 20 Kwa 20 visipimwe, huwa najiuliza anajua dhana nzima ya mipango miji!? Sasa unakuta watu wanazidi kujenga kiholela hakuna hata utaratibu wa kuonyesha mipaka ya barabara za mitaa hakuna chochote Karne ya 21!? Yaani huwa machozi yananitoka najiuliza wajukuu zetu watajifunza nini kwetu!?
 
Watu wametumia pesa za world Bank kuweka vibao vya mitaa kwenye chochoro badala ya kuomba Hela kupanga miji yetu!! Haya ni maajabu ya Musa na Firahuni!! Watu wanapiga bila kuwa na aibu!! Hii Professor Tibaijuka inamuhusu!! In Habitant WA Dunia haweze kupanga nyumbani kwake anajiita professor Shame!!
 
Umedadavua vizuri mkuu.

Kuhusu makatazo ya viwanja vya 20 kwa 20 hata mimi nilisikia ingawa ninachojua waziri husika anafuata miongozo, maelekezo na malengo kutoka kwa wataalamu wa wizara.

Kwa ishu ya 20 na 20 kulikuwa na mantiki hasa katika upimaji kwa lengo la uboreshaji wa makazi bora.Pia kulitokea udanganyifu uliofanywa na baadhi ya watu wasio waaminifu. Kwa mfano katika vipimo unaweza kupima kwa kutumia mita au futi ingawa kanuni na taratibu zinataka kipimo cha mita za mraba kitumike kupima eneo. Wananchi wengi wakiambiwa urefu kwa upana wa eneo hawajui maana yake halisi na kujikuta wakipimiwa kwa futi badala ya mita na kupelekea kupata maeneo madogo mno wakati wangeweza kupimia maeneo yanayotosheleza.

Fikiria ukiwa na eneo la mita za mraba 400 ambalo ndio hizo 20mita kwa 20mita kwa ajili ya makazi, eneo hilo ujenge nyumba ya kawaida tu, itakulazimu uweke mashimo ya maji taka, uwe na parking au sehemu ya bustani kidogo kwa ajili ya mboga mboga. Je, jiulize eneo hilo litatosha?

Kwa hiyo nafikiri kwa maeneo mapya ni bora kwa faida ya maendeleo ya baadae waachane na viwanja vidogo wakati maeneo ya ardhi bado ni makubwa.
 

Nani huyo anapima viwanja kwa futi nchini Tanzania? Watu kama hao inatakiwa wakae jela angalau mwezi mmoja ili waache ujinga huo.
 
kwa ccm hilo haliwezekana. Chukulia mfano rais wa kenya , Ruto. Moja ya vipaumbele vyake miaka hii mitano ni kujenga nyumba 200,000 jijini nairobi. Serikali inapoamua kujenga makazi ya watu mji lazima upangike. Mji ambao serikali ingeujenga ingekuwa serious ilikuwa Dodoma. Ijapokuwa nao viwanja umepimwa, lakini ni skwata tu. Wanadai umepimwa lakini viwanja vilivyopimwa ni vidogo havifai.


Na hiyo ni kwa nchi nzima, kwa mfano dar na Pwana, viwanja vinapimwa watu wanauziwa lakini viwanja vinavyopimwa ni vidogo skwata style vingine ni chini ya sqm 400. unakuta kiwanja kimepimwa cha 12x16. Na halamashauri wamekipitisha, wizara imetoa blue print na plan number....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…