Kama kupata Maelezo ya Adamoo, sheria ilikiukwa, Yatatupwa

Kama kupata Maelezo ya Adamoo, sheria ilikiukwa, Yatatupwa

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Shauri dogo ndani ya shauri lilopo sasa hivi linatokana na utata kuwa je mshitakiwa wa pili Adamoo alitoa maelezo yake kwa mujibu wa sheria?

Kuna tashwishi kuhusiana na maelezo ya mshitakiwa huyu kuwa aliteswa au hakuteswa kwenye kupelekea kuwapo kwa maelezo yake.

Je kulikuwa na shinikizo lolote? Je kulikuwa na matumizi ya nguvu? Je kulikuwa na ushawisi wowote?

Je mshitakiwa alitoa maelezo hayo kwa mujibu wa sheria kama inavyoainishwa?

Kumekuwa na wachambuzi uchwara wanao jaribu kulazimisha shauri la uhaini la miaka ya 1980 kufanana na hili. Wakijaribu kuhalalisha matumizi ya mateso kama njia muafaka mno ya kupata maelezo kamili ya njama nzima kutoka kwa washitakiwa.

Ifahamike kuwa mheshimiwa Jaji yuko katikati ya kutafuta ukweli wa namna ambavyo maelezo ya mshitakiwa wa pili yalipatikana.

Akijiridhisha tu kuwa ilikuwa ni kinyume cha sheria, yaani kama mateso, mashinikizo, ushawisi, ghiliba, nk vilitumika na hata labda bila ya maonyo stahiki kutolewa ili kupata maelezo hayo, basi kwa mujibu wa sheria, Jaji atafanya kazi yake.

Ikumbukwe upande wa mashtaka wanahaha kweri kweri kukanusha kuwa watuhumiwa hawakuteswa. Katika hilo wameleta mashahidi watatu wazito kweri kweri.

Sasa kama kuna wachambuzi uchwara wanaoona mateso ni sawa, hii mbona sasa hiyo itakuwa ndiyo kubwa kuliko?
 
Kingai na Mahita ni watu waongo sana,wanadai wakati wanawakamata kina Adamoo kule Moshi na kufuata sheria zote palikuwa na mashahidi wanawake wawili.
Kwa nini wasiwalete wathibitishe madai yao?

Uzuri polisi wanajulikana kuwa ni wahalifu wazoefu. Kinyume cha sheria hupiga watuhumiwa.

Nani hakumsikia wa kipigo cha mbwa koko?

Wahalifu wazoefu hawa hawakumtesa Adamoo peke yake. Walimtesa pia Ling'wenya, Urio na wakamtupa Lijenje.

Pasipo na uhalali wowote wakawashurutisha watuhumiwa kutumia majina bandia na kuwanyima chakula.

Kama vile haitoshi wakamweka Adamoo kwenye kabati.
 
Shauri dogo ndani ya shauri lilopo sasa hivi linatokana na utata kuwa je mshitakiwa wa pili Adamoo alitoa maelezo yake kwa mujibu wa sheria?

Kuna tashwishi kuhusiana na maelezo ya mshitakiwa huyu kuwa aliteswa au hakuteswa kwenye kupelekea kuwapo kwa maelezo yake.

Je kulikuwa na shinikizo lolote? Je kulikuwa na matumizi ya nguvu? Je kulikuwa na ushawisi wowote?

Je mshitakiwa alitoa maelezo hayo kwa mujibu wa sheria kama inavyoainishwa?

Kumekuwa na wachambuzi uchwara wanao jaribu kulazimisha shauri la uhaini la miaka ya 1980 kufanana na hili. Wakijaribu kuhalalisha matumizi ya mateso kama njia muafaka mno ya kupata maelezo kamili ya njama nzima kutoka kwa washitakiwa.

Ifahamike kuwa mheshimiwa Jaji yuko katikati ya kutafuta ukweli wa namna ambavyo maelezo ya mshitakiwa wa pili yalipatikana.

Akijiridhisha tu kuwa ilikuwa ni kinyume cha sheria, yaani kama mateso, mashinikizo, ushawisi, ghiliba, nk vilitumika na hata labda bila ya maonyo stahiki kutolewa ili kupata maelezo hayo, basi kwa mujibu wa sheria, Jaji atafanya kazi yake.

Ikumbukwe upande wa mashtaka wanahaha kweri kweri kukanusha kuwa watuhumiwa hawakuteswa. Katika hilo wameleta mashahidi watatu wazito kweri kweri.

Sasa kama kuna wachambuzi uchwara wanaoona mateso ni sawa, hii mbona sasa hiyo itakuwa ndiyo kubwa kuliko?
Hivyo ndivyo sheria inavyotaka. Maelezo ni fake.
 
Kingai na Mahita ni watu waongo sana,wanadai wakati wanawakamata kina Adamoo kule Moshi na kufuata sheria zote palikuwa na mashahidi wanawake wawili.
Kwa nini wasiwalete wathibitishe madai yao?
Uongo mwingi sana.
 
Uzuri polisi wanajulikana kuwa ni wahalifu wazoefu. Kinyume cha sheria kupiga watuhumiwa.

Nani hakumsikia wa kidogo cha mbwa koko?

Wahalifu wazoefu hawa hawakumtesa Adamoo peke yake. Walimtesa pia Ling'wenya, Urio na wakamtupa Lijenje.

Pasipo na uhalali wowote wakawashurutisha watuhumiwa kutumia majina bandia na kuwanyima chakula.

Kama vile haitoshi wakamweka Adamoo kwenye kabati.
Ivi huyu Moses ijenje mbona kama vile hana ndugu.au wamelizika alichofanyiwa ndugu yao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ivi huyu Moses ijenje mbona kama vile hana ndugu.au wamelizika alichofanyiwa ndugu yao

Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu hii nchi viongozi wake ni dhwalimu sana.

Kwani nduguze Ben, Azory au hata Lissu utawasikia wapi?

Ndugu zao hao ni sisi ambao leo wahanga ni wao, kesho sisi.

IMG_20210930_170832_807.jpg


Arejeshwe Moses Lijenje akiwa hai.
 
Shauri dogo ndani ya shauri lilopo sasa hivi linatokana na utata kuwa je mshitakiwa wa pili Adamoo alitoa maelezo yake kwa mujibu wa sheria?

Kuna tashwishi kuhusiana na maelezo ya mshitakiwa huyu kuwa aliteswa au hakuteswa kwenye kupelekea kuwapo kwa maelezo yake.

Je kulikuwa na shinikizo lolote? Je kulikuwa na matumizi ya nguvu? Je kulikuwa na ushawisi wowote?

Je mshitakiwa alitoa maelezo hayo kwa mujibu wa sheria kama inavyoainishwa?

Kumekuwa na wachambuzi uchwara wanao jaribu kulazimisha shauri la uhaini la miaka ya 1980 kufanana na hili. Wakijaribu kuhalalisha matumizi ya mateso kama njia muafaka mno ya kupata maelezo kamili ya njama nzima kutoka kwa washitakiwa.

Ifahamike kuwa mheshimiwa Jaji yuko katikati ya kutafuta ukweli wa namna ambavyo maelezo ya mshitakiwa wa pili yalipatikana.

Akijiridhisha tu kuwa ilikuwa ni kinyume cha sheria, yaani kama mateso, mashinikizo, ushawisi, ghiliba, nk vilitumika na hata labda bila ya maonyo stahiki kutolewa ili kupata maelezo hayo, basi kwa mujibu wa sheria, Jaji atafanya kazi yake.

Ikumbukwe upande wa mashtaka wanahaha kweri kweri kukanusha kuwa watuhumiwa hawakuteswa. Katika hilo wameleta mashahidi watatu wazito kweri kweri.

Sasa kama kuna wachambuzi uchwara wanaoona mateso ni sawa, hii mbona sasa hiyo itakuwa ndiyo kubwa kuliko?
Haowanaoegemea upande wa mateso,Bila shaka nj wale wanaochambua kwa ajili ya tumbo lao.
 
Ktk suala la hawa makomando hata JWTZ lina mapungufu makubwa mno.
1) Walikuwa waajiriwa tena ma-Komando pamoja na kuwaachisha kazi walitakiwa kujua wako wapi na wanafanya nn kama wanajua ni watu hatari.
2) Kwa mafunzo waliowapa sio vyema makosa yao kushughulikiwa na akina Kingai na Maita ona sasa Moses Lijenje hatujui yuko wapi...🤔
 
Ushahidi wa upande wa mashitaka walidai washitakiwa walipotolewa Moshi kwenda Dar es salaam walifikishwa Central Dsm na Detention Registers vikapelekwa mahakamani. Lakini watuhumiwa wa ugaidi kwenye ushahidi wao walisema walifikishwa Tazara na baadae wakahamishiwa Mbweni. Je hapo ukweli wa mashahidi upande wa mashitaka upo wapi?

Suala la pili, upande huo huo wa mashitaka walitamka walimshika mmoja wa watuhumiwa wa ugaidi kuwa alikutwa na madawa ya kulevya kete 85 na bunduki moja aina ya bastola ambapo kulikuwa na utata wa idadi za risasi alizokutwa nazo kati ya maelezo ya shahidi na maelezo kwenye hati ya mashitaka. Swali; kwa nini madawa na bastola havipo kwenye vielelezo vilivyopelekwa mahakamani? Kuna kitu gani kilichofanya vielelezo hasa bastola isielezwe umiliki wake kama ulikuwa ni halali au siyo halali?

Haya maswali yatasaidia kujua kwamba watuhumiwa walibambikizwa kesi au hawakubambikizwa.

Sent from my SM-J700H using JamiiForums mobile app
 
Ushahidi wa upande wa mashitaka walidai washitakiwa walipotolewa Moshi kwenda Dar es salaam walifikishwa Central Dsm na Detention Registers vikapelekwa mahakamani. Lakini watuhumiwa wa ugaidi kwenye ushahidi wao walisema walifikishwa Tazara na baadae wakahamishiwa Mbweni. Je hapo ukweli wa mashahidi upande wa mashitaka upo wapi?

Suala la pili, upande huo huo wa mashitaka walitamka walimshika mmoja wa watuhumiwa wa ugaidi kuwa alikutwa na madawa ya kulevya kete 85 na bunduki moja aina ya bastola ambapo kulikuwa na utata wa idadi za risasi alizokutwa nazo kati ya maelezo ya shahidi na maelezo kwenye hati ya mashitaka. Swali; kwa nini madawa na bastola havipo kwenye vielelezo vilivyopelekwa mahakamani? Kuna kitu gani kilichofanya vielelezo hasa bastola isielezwe umiliki wake kama ulikuwa ni halali au siyo halali?

Haya maswali yatasaidia kujua kwamba watuhumiwa walibambikizwa kesi au hawakubambikizwa.

Sent from my SM-J700H using JamiiForums mobile app

Washitakiwa wanasema walikuwa Tazara si Central. Polisi wanasema Central si Tazara. Maneno ya washitaki dhidi ya washitakiwa.

Nani wa kuaminika?

Detention register hazikusoma majina yao as per shahidi wa 3 utetezi ambaye si mshitaki wala mshitakiwa.

Shahidi wa tatu na mkewe Ling'wenya wasingekwenda hadi mortuary kama detention register central ingesoma majina ya wenza wao.

Kama walikuwa Central kulikuwa na umuhimu gani kuwapeleka Mbweni kwa mfano? Kumbuka Mbweni ni padogo kuliko Central. Kumbuka pia Inspekta Mahita alishindwa kueleza uhalali au hata umuhimu wa kuwapeleka watuhumiwa Mbweni.

Uwezekano mkubwa ni kuwa waongo hapa ni polisi. Wewe huoni hivyo ndugu yangu?

Anayeongelea na kijichanganya kuhusu bastola na madawa ya kulevya ni polisi. Mshitakiwa wa pili anasema aliwekewa na polisi bastola na yaliyosemekana kuwa ni madawa. Iko kwenye rejea, kupisha yaliyompata mshitakiwa wa pili mshitakiwa wa tatu aliwahi kutoa vyake ili asiwekewe pia.

Polisi hawana kwenye rekodi chochote walichochukua kutoka kwa washitakiwa, zaidi ya bastola na madawa ya kulevya kutoka kwa washitakiwa. Kwani washitakiwa wangalilipa na nini huduma waliyokuwa wakiipata pande kabla ya kukamatwa?

Polisi hawana maelezo Adamoo na here 85 za madawa alikuwa anauza au anatumia? Haupo mwuunganiko wowote baina ya silaha wala madawa ya kulevya kwenye kesi hii.

Polisi wetu wanajulikana kuwa ni wabambikaji kesi sugu. Wanajulikana kubambukia wengi silaha na hata madawa ya kulevya. Wana bonasi ya kuuwa watuhumiwa kwa kauli ya kuwanyang'anya silaha haraka haraka.

Kwamba mtuhumiwa aliuawa akijaribu kuwatoroka au kuwarushia risasi, halipo geni hapo.

Polisi wanajulikana kwa udhwalimu wao:

IMG_20210930_170832_807.jpg


Ukiangalia yote haya mizani inaangukia upande wao. Uwezekano mkubwa waongo kwenye kadhia hii si washitakiwa.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Mh. Jaji Kiongozi kayapokea maelezo ya Adamoo kwa Kingai kuwa:

1. Yalitolewa ndani ya muda
2. Yalitolewa kwa ridhaa ya Mtuhumiwa.

Bila shaka atatusaidia kujua walipo Moses Lijenje na pia Luteni Urio.

Haki ikitendeka haijifichi.

"Sijui kutaga mayai, lakini yao bovu nalijua" -- Askofu Dr. Benson Bagosha.
 
Mh. Jaji Kiongozi kayapokea maelezo ya Adamoo kwa Kingai kuwa:

1. Yalitolewa ndani ya muda
2. Yalitolewa kwa ridhaa ya Mtuhumiwa.

Bila shaka atatusaidia kujua walipo Moses Lijenje na pia Luteni Urio.

Haki ikitendeka haijifichi.

"Sijui kutaga mayai, lakini yao bovu nalijua" -- Askofu Dr. Benson Bagosha.

JAJI KAYUMBA KWA MAKUSUDI KUANGALIA MASLAHI YAKE....YA KUZAWADIWA U-JAJI kiongozi, ila itabaki kwenye record kwa wanasheria wenzake hapa na ulimwenguni...pia mwisho Kwa Mungu wake anayemwabudu
 
JAJI KAYUMBA KWA MAKUSUDI KUANGALIA MASLAHI YAKE....YA KUZAWADIWA U-JAJI kiongozi, ila itabaki kwenye record kwa wanasheria wenzake hapa na ulimwenguni...pia mwisho Kwa Mungu wake anayemwabudu

Bila mihimili hii kuwa huru tungali na safari ndefu.

Shikamoo Kenya. Shikamoo Raila champion wa katiba mpya Kenya.
 
Shauri dogo ndani ya shauri lilopo sasa hivi linatokana na utata kuwa je mshitakiwa wa pili Adamoo alitoa maelezo yake kwa mujibu wa sheria?

Kuna tashwishi kuhusiana na maelezo ya mshitakiwa huyu kuwa aliteswa au hakuteswa kwenye kupelekea kuwapo kwa maelezo yake.

Je kulikuwa na shinikizo lolote? Je kulikuwa na matumizi ya nguvu? Je kulikuwa na ushawisi wowote?

Je mshitakiwa alitoa maelezo hayo kwa mujibu wa sheria kama inavyoainishwa?

Kumekuwa na wachambuzi uchwara wanao jaribu kulazimisha shauri la uhaini la miaka ya 1980 kufanana na hili. Wakijaribu kuhalalisha matumizi ya mateso kama njia muafaka mno ya kupata maelezo kamili ya njama nzima kutoka kwa washitakiwa.

Ifahamike kuwa mheshimiwa Jaji yuko katikati ya kutafuta ukweli wa namna ambavyo maelezo ya mshitakiwa wa pili yalipatikana.

Akijiridhisha tu kuwa ilikuwa ni kinyume cha sheria, yaani kama mateso, mashinikizo, ushawisi, ghiliba, nk vilitumika na hata labda bila ya maonyo stahiki kutolewa ili kupata maelezo hayo, basi kwa mujibu wa sheria, Jaji atafanya kazi yake.

Ikumbukwe upande wa mashtaka wanahaha kweri kweri kukanusha kuwa watuhumiwa hawakuteswa. Katika hilo wameleta mashahidi watatu wazito kweri kweri.

Sasa kama kuna wachambuzi uchwara wanaoona mateso ni sawa, hii mbona sasa hiyo itakuwa ndiyo kubwa kuliko?
Majibu umeyapata leo
 
Majibu umeyapata leo

Hata jiwe aliwahi kusema nini wateuliwa wake wanatakiwa kufanya:




Sembuse na cheo juu?

Nini hakifahamiki bila katiba mpya?

Mengine haya si ni ushahidi tu kwanini katiba mpya ni lazima?
 
Hata jiwe aliwahi kusema nini wateuliwa wake wanatakiwa kufanya:




Sembuse na cheo juu?

Nini hakifahamiki bila katiba mpya?

Mengine haya si ni ushahidi tu kwanini katiba mpya ni lazima?

Bali tulieni mahakama ifanye kazi.
 
Back
Top Bottom