Kama kweli Mo Dewji kamuuza Chama katukwaza wana Simba

Riz king

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2018
Posts
276
Reaction score
549
Hamna kitu nimeumia kama kuona taarifa Instagram za wachambuzi wa soka bongo kuwa Chama tayari kashapigwa bei na picha ikimwonesha yupo na Tuisila Kisinda kwenye uzi wa waarabu.

Mo sijui umetutendea haki, nimetoa chozi langu kumshtaki Mo kwa mwenyezi Mungu kama hili jambo likiwa kweli. Moo ulituahidi kuwa bado unajenga timu ya ushindani ndani na nje ya Africa kumbe upo kimasilahi.

Sikuamini tena Moo Dewji, mbona hujatuuliza wana Simba ili tukupe mawazo, wewe umejichukulia uamuzi. Asante kwa haya maumivu uliyotupa wana simba aisee
 
Utopolo mtalia sana. Na Bado.
Na hapo hamjaanza kudondosha point.
Utopolo kila mkilala mnamuota Mo. Na chawa lenu halipo siku hizi mtakua mnashangaa na surprise tu.
 
Kwani unamlipa wewe?

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
Nacheka kama mazuri, ila SIMBA SC kuuza key players wawili kwa wakati mmoja bila kujua uwezo wa tuliowasajili, katika kuziba pengo ni ujinga mkubwa.

Ikitokea Hawa tuliowasajili kwasasa wameshindwa kudeliver kile tulichokuwa tunakipata kwa kina Chama na Miquisone,basi tujue kwamba tutakuwa wahanga uwanjani kwa muda usiojulikana mpaka pale tutakaocheza kamari nyingine katika manunuzi.

Hebu tuifikirie ile Simba Sc uliyowahi kucheza mechi kadhaa huku chama na Miquisone wakiwa benchi, hakika ilikuwa ni kituko.Leo tunauza Chama na Miquisone alafu replacement ni kumuongeza Ajib mkataba seriously? Aiseeeh😂

Lakini pia tujue tu kwamba hii biashara imefanyika kwa siri sana na jaluna shabiki wa kawaida atakaekuja kujua hao wachezaji wameuzwa kwa bei gani, unajua ni kwanini? Sikuzote hatutakiwi kuona kwamba Simba inaingiza hela,tunatakiwa kujua tu kwamba hakuna faida inayoingia pale zaidi ya kupokea hisani tu.Hivyo hizo deals zitabaki kwa tetesi mpaka kiama,labda tuzisikie kutoka kwa hizo teams zilizowasajili.

Anyways tumeuza Triple C alafu tukamuomgezea mkataba AJIB , daah ngoja tuone.
 
Kwani unamlipa wewe?

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
Hizi kauli ni za kijinga sana, kwahiyo kwakuwa shabiki hamlipi mchezaji basi hana haki ya kumzungumzia? Daah

Hicho kiburi cha kudharau mashabiki endeeleni nacho wakati huu ambao Simba Sc inafanya vizuri kama hivi, ila upepo ukigeuka mtakuja kuitafuta support ya mashabiki kwa tochi (labda sio mashabiki wa Simba ninaowajua mimi) na wakati huo mtakacyokipata ni lawama tu.

Shabiki aheshimiwe.
 
Hiyo klub ni ya Muddy wewe unaumia nini kuna ulichochangia
 
Kama tumemuuza kwa TZS. 1.5bil. kwenye hayo mauzo Serikali yetu itajipatia TZS. 228.8 mil.!
Hutakiwi kujua dau lilitolewa Ili siku zote uendelee kuamini kuwa Pale Simba Sc hakuna faida yoyote inayopatikana zaidi ya hisani tu inazopokea.
 
Hutakiwi kujua dau lilitolewa Ili siku zote uendelee kuamini kuwa Pale Simba Sc hakuna faida yoyote inayopatikana zaidi ya hisani tu inazopokea.
Yaah pale simba hatupati faida kabisa kwenye uendeshaji
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…