Zanzibar 2020 Kama Maalim Seif akishindwa kuchukua nchi mwaka huu, ajilaumu mwenyewe kwa uamuzi wake wa kutokwenda kwa Wapinzani wenye nguvu (CHADEMA)

Zanzibar 2020 Kama Maalim Seif akishindwa kuchukua nchi mwaka huu, ajilaumu mwenyewe kwa uamuzi wake wa kutokwenda kwa Wapinzani wenye nguvu (CHADEMA)

Naanto Mushi

JF-Expert Member
Joined
Oct 16, 2015
Posts
6,236
Reaction score
15,677
Nimesikiliza kwa makini sana hotuba za Tundu Lissu akiwa Zanzibar, yaani unaona kabisa madini aliyokuwa anamwaga Tundu Lissu, laiti kama ile platform angekuwa yupo bega kwa bega ana mnadi Maalim Seif kama mgombea wa CHADEMA Zanzibar, mambo yangekuwa tofauti sana.

Sio kwamba napuuza nguvu ya ACT - Wazalendo kama chama cha upinzani chenye nguvu, ila ni kwamba kwenye nyakati ngumu kama hizi za kisiasa ambazo zina watawala wakorofi, ili uweze kupata matokeo, ni lazima uwe upande wa chama cha upinzani chenye historia ya uhodari wa hoja, harakati, na mapambano.

Nikifananisha ACT - Wazalendo na CHADEMA, ni vyama ambavyo vinautofauti mkubwa sana kwenye uhodari wa hoja, harakati, na mapambano. ACT bado nakichukulia kama chama ambacho kipo 'soft sana' na kinachofata misingi ya kujali sana taratibu na sheria. Ni chama ambacho kina uwoga uwoga fulani wa kuwaudhi watawala. Angalia ile kauli ya Bernard Membe ya kwamba eti alitafuta wadhamini kimya kimya ili kutokuingia kwenye mtego wa kuanza kampeni', ni moja wapo ya viashiria kwamba ACT bado kipo soft sana. Kwa mzani huo, sioni ni namna gani msimamo wa chama utaunga mkono mapambano ya Maalim Seif ya kudai haki yake endapo kama ataporwa ushindi kama ilivotokea miaka ya nyuma. Huwa inakuwa ngumu sana, kupambana ikiwa upo kwenye chama chenye falsafa nyepesi kuhusu mapambano na harakati.

Upande wa CHADEMA, wana historia thabiti ya harakati za kupambana, ambazo hata mimi binafsi naamini ndo mwarobaini wa kupambana na CCM, suala la Zanzibar, ukizingatia na historia yake, hakuna namna upinzani watashinda kule bila harakati za mapambano. Kwa historia ya CHADEMA na viongozi wake ambao wanamisimamo imara na wasioyumba, naamini kabisa Maalim Seif angekuwa kwenye chama salama sana kwenye huu uchaguzi ambao kwa huku Tanganyika, CHADEMA wameshajipambanua wazi wazi kwamba hawatakubali kunyongwa ifikapo October 28.

Haya ni mawazo tu, kulingana na upepo unavoenda sio kwamba nakichukia ACT Wazalengo, ila pia ni changamoto kwa ACT Wazalengo, wanatakiwa waamue kuwa maji ya moto kweli, nawaona wapo soft sana na kwa kweli wananiuzi, na wakiendelea kuwa soft hivi, hakuna namna Maalim atachukua nchi endapo ACT itaendelea kuwa na misimamo isiyokuwa ya kiharakati na mapambano kama wenzao CHADEMA.
 
Kwani wanaomnyima kila wakati huwa ni kina nani?
Kuna hotuba ya Lissu kaelezea vizuri sana kwamba ni Tanganyika, ila naamini endapo angekuwa anapambania haki yake kikamilifu, huenda hata hao waporaji wangeufyata
 
Mkoa wetu wa Zanzibar utaendelea kutawaliwa na Ccm wa Tanganyika hadi kieleweke.

Nyie wapinzani mnapoteza muda wenu tu
 
Maalim huwa anashida kila chaguzi. Dola sasa.......
Hata Dola huwa inaangalia pa kuonea, jiulize ni kwanini mikoa kama Morogoro, Dodoma, na Lindi kuna watu wengi wamepita bila kupingwa na sio mikoa kama Mara, Mbeya na Arusha.

Issue ni kwamba hata hiyo Dola wanaogopa sana nguvu ya umma. Asikuambie mtu chief, tuna marafiki kibao maaskari wanatuambia the same same thing, watu wanavokuwa waoga ndo wao wanapata urahisi wa kutekeleza majukumu yao
 
Maalimu anazielewa siasa za Chadema na 2015 aliona jinsi Chadema walivyokua wapuuzi, Maalim Sefu na viongozi wenzake walifanya tathmini ya kutosha na kujirizisha kuwa nibora wajiunge ACT kuliko Chadema.
Maalimu anazijua siasa za nchi hii vizuri kuliko mwanachadema yoyote unaye mfahamu. Maalm ana uzoefu wa halizote za kisasa kuanzia za kutumia nguvu na kupambana na polisi mbaka siasa za kukaamezani kutafuta suluhu.
Mleta mada huna chochote Cha kumfundisha maalimu katika siasa za Tanzania, anajua matokeo ya kutumia Maguvu na matokeo ya kutumia busara na hivyo vyote walisha wahi kuvijaribu akiwa CUF.
 
Maalimu seifu kazoea kuuza ushindi nilipumba tu huyo haiwezekani hatoboe then I washindwe kumtangaza.
 
Nimesikiliza kwa makini sana hotuba za Tundu Lissu akiwa Zanzibar, yaani unaona kabisa madini aliyokuwa anamwaga Tundu Lissu, laiti kama ile platform angekuwa yupo bega kwa bega ana mnadi Maalim Seif kama mgombea wa CHADEMA Zanzibar, mambo yangekuwa tofauti sana.

Sio kwamba napuuza nguvu ya ACT - Wazalendo kama chama cha upinzani chenye nguvu, ila ni kwamba kwenye nyakati ngumu kama hizi za kisiasa ambazo zina watawala wakorofi, ili uweze kupata matokeo, ni lazima uwe upande wa chama cha upinzani chenye historia ya uhodari wa hoja, harakati, na mapambano.

Nikifananisha ACT - Wazalendo na CHADEMA, ni vyama ambavyo vinautofauti mkubwa sana kwenye uhodari wa hoja, harakati, na mapambano. ACT bado nakichukulia kama chama ambacho kipo 'soft sana' na kinachofata misingi ya kujali sana taratibu na sheria. Ni chama ambacho kina uwoga uwoga fulani wa kuwaudhi watawala. Angalia ile kauli ya Bernard Membe ya kwamba eti alitafuta wadhamini kimya kimya ili kutokuingia kwenye mtego wa kuanza kampeni', ni moja wapo ya viashiria kwamba ACT bado kipo soft sana. Kwa mzani huo, sioni ni namna gani msimamo wa chama utaunga mkono mapambano ya Maalim Seif ya kudai haki yake endapo kama ataporwa ushindi kama ilivotokea miaka ya nyuma. Huwa inakuwa ngumu sana, kupambana ikiwa upo kwenye chama chenye falsafa nyepesi kuhusu mapambano na harakati.

Upande wa CHADEMA, wana historia thabiti ya harakati za kupambana, ambazo hata mimi binafsi naamini ndo mwarobaini wa kupambana na CCM, suala la Zanzibar, ukizingatia na historia yake, hakuna namna upinzani watashinda kule bila harakati za mapambano. Kwa historia ya CHADEMA na viongozi wake ambao wanamisimamo imara na wasioyumba, naamini kabisa Maalim Seif angekuwa kwenye chama salama sana kwenye huu uchaguzi ambao kwa huku Tanganyika, CHADEMA wameshajipambanua wazi wazi kwamba hawatakubali kunyongwa ifikapo October 28.

Haya ni mawazo tu, kulingana na upepo unavoenda sio kwamba nakichukia ACT Wazalengo, ila pia ni changamoto kwa ACT Wazalengo, wanatakiwa waamue kuwa maji ya moto kweli, nawaona wapo soft sana na kwa kweli wananiuzi, na wakiendelea kuwa soft hivi, hakuna namna Maalim atachukua nchi endapo ACT itaendelea kuwa na misimamo isiyokuwa ya kiharakati na mapambano kama wenzao CHADEMA.
Inakuwa vizuri ukijua historia. Nakubaliana nawe kwamba ACT Wazalendo wako soft, lakini kule visiwani huwa hawategemei sana uimara wa chama kutoka Bara; na ndiyo maana mwaka 2001 CUF, wakati huo, ikaitisha maandamano na yakatokea yaliyotokea. Hakukuwa na kuungwa mkono kwa uwazi kutoka Bara. Mwaka huu ikitokea vyovyote, haitokuwa ni kwa sanbabu ya kuungwa mkono na Bara ila ni kwa sababu ya maamuzi ya Wazanzibari wenyewe. Natamani sana kuona mwaka huu CHADEMA itafanya nini kwani 2015 iliporwa ushindi na ikatulia kama maji mtungini. Historia hutukuka ikiwa ya vitendo kuliko ya kusema bila kutekeleza. Tusubiri tuone.
 
kwa taarifa yako maalim Seif hajawahi shindwa Zanzibar, tatizo ni wazanzibari wenyewe awajui kulinda kura zao
 
Maalim seif ata angekuwa private candidate angeshinda kama kawaida
 
Kwa mwaka huu maalimu anashinda dr hussen mwinyi wazanzibar hawamtambui nadhan wazanzibar mnawaelewa
 
Back
Top Bottom