Ifanyike sensa ndogo ya wanafunzi, kujua idadi ya wanafunzi kila wilaya au kata kwa mfano. Kisha yawekwe mabasi makubwa kama ya UDA kwa kila route.
Mabasi hayo yawekwe kulingana na idadi ya shule na wanafunzi katika eneo husika, for instance, kwa shule zilizopo k/koo, wanafunzi wengi huenda Mbagala, Gongo la Mboto na Tabata, hapo wanaweza kuweka mabasi mawili yapitayo Nyerere Road kuelekea G/Mboto na lingine Kilwa Road kuelekea Mbagala. Watawasaidia wanafunzi wengi.
Kisha waweke basi moja litakalokwenda hadi Ubungo kwa kupitia barabara itakayofaa. Maeneo yapo mengi, nadhani point imeeleweka, wanaweza kupanga route za namna hiyo.
Wanafunzi watalipa nauli ya kawaida wanayolipa sasa ili kusaidia suala la maintenance ya mabasi, kama kutakua na pungufu serikali itachangia percent itakayobaki.
Kama hili litafanyika, idadi kubwa ya wanafunzi itapungua katika vituo vya mabasi.