Nibozali
JF-Expert Member
- Oct 15, 2016
- 572
- 1,055
Tahadhari!
Usinihoji kuwa mimi ni nani, lakini kiufupi naipenda Tanzania ingawa yenyewe hainipendi kama ninavyoipenda.
Kama kawaida yangu naendelea kunyetisha na kuwapa habari motomoto zihusianazo na makinikia pamoja na hawa wanaume wezi ( Acacia na Barrick)
Viongozi wa Tanzania waliteleza katika hili na wanaendelea kuteleza na sasa kilichobaki ni kuanguka na kushindwa kuendelea na safari ya kuokoa makinikia na madini ya Watanzania. Kosa la kwanza ni kumpuuza Acacia ambaye ndiye mwizi mkuu na namba Moja. Amepuuzwa na kuchukuliwa kama mtu mdogo sana asiye na madhara katika wizi huu ingawa ndiye mwizi wetu. Kiuhalisia mwizi wetu siyo Barrick ila nguvu zetu zote tumehamishia kwake huku tukiwa na matarajio makubwa!!!! Mwizi tumemuacha, sasa anatamba! Yuko huru! Hata kwenye mazungmzo hayumo na tunaamini hivo kuwa hayumo maana mazungumzo ni kati yetu na Barrick, WATANZANIA MNAJIDANGANYA!!!
Huu ndio mkakati wa Acacia na Barrick na ukifanikiwa watanzania wake kwa waume mnatakuwa mmepigwa bao!
Kama makubaliano kati Barrick na Serikali ya Tanzania hayatakuwa na manufaa kwa Acacia na Barrick, kwa maana ya malipo ambayo yanapaswa kulipwa kwa Tanzania ( ingawa pesa itakayolipwa ni ndogo tofauti na matarajio ya Watanzania) Acacia wataendelea na Kesi yao ambayo wanapanga kuifungua dhidi ya Tanzania. Katika kesi hii ambayo kwa kiasi kikubwa wana uhakika Wa kushinda watadai fidia kubwa mno ambayo ikilipwa itawawezesha kuendesha kampuni yao bila wasiwasi.
HOFU YAO KWA SASA
Hofu yao mpaka sasa ni pale watakapoamua kuishitaki Tanzania basi kuna uwezekano wa kufukuzwa kuendesha shughuli zao hapa nchini. Naam! Hili wamshaliona na wamekubaliana na Barrick namna watakavyoendesha biashara zao hata baada ya kufukuzwa, kwani kama haya yatatatokea Barrick watamiliki hisa zote hata zile zilizokuwa zikimilikwa na Acacia.
Lakini wanaona hawatakuwa na namna ya kurudisha pesa yao zaidi ya kuishitaki Tanzania ambayo mpaka sasa imeshasahau kuwa ndio iliyosaini mikataba na kuiruhusu kampuni ya acacia kuendesha shughuli zao hapa nchini
MPANGO WAO
Barrick wanaweza kulipa hicho kiasi kidogo harafu kwa mkakati mzito acacia watarudisha pesa zaidi ya hizo kwa njia ya mahakama huku wakijifanya kuwa wao hawana habari na mazungumzo yanayoendelea. Ukweli ni kwamba acacia wanahusika chini ya mkakati mzito na Barrick na Leo lao ni kuipiga Tanzania na mpango wao huenda ukafanikiwa.
Mpango wao ukifanikiwa wale mliokuwa mmeshakabidhiwa noa mjiandae kuzirudisha
Ni hayo tu
NIBOZALI WA LUMUMBA
Usinihoji kuwa mimi ni nani, lakini kiufupi naipenda Tanzania ingawa yenyewe hainipendi kama ninavyoipenda.
Kama kawaida yangu naendelea kunyetisha na kuwapa habari motomoto zihusianazo na makinikia pamoja na hawa wanaume wezi ( Acacia na Barrick)
Viongozi wa Tanzania waliteleza katika hili na wanaendelea kuteleza na sasa kilichobaki ni kuanguka na kushindwa kuendelea na safari ya kuokoa makinikia na madini ya Watanzania. Kosa la kwanza ni kumpuuza Acacia ambaye ndiye mwizi mkuu na namba Moja. Amepuuzwa na kuchukuliwa kama mtu mdogo sana asiye na madhara katika wizi huu ingawa ndiye mwizi wetu. Kiuhalisia mwizi wetu siyo Barrick ila nguvu zetu zote tumehamishia kwake huku tukiwa na matarajio makubwa!!!! Mwizi tumemuacha, sasa anatamba! Yuko huru! Hata kwenye mazungmzo hayumo na tunaamini hivo kuwa hayumo maana mazungumzo ni kati yetu na Barrick, WATANZANIA MNAJIDANGANYA!!!
Huu ndio mkakati wa Acacia na Barrick na ukifanikiwa watanzania wake kwa waume mnatakuwa mmepigwa bao!
Kama makubaliano kati Barrick na Serikali ya Tanzania hayatakuwa na manufaa kwa Acacia na Barrick, kwa maana ya malipo ambayo yanapaswa kulipwa kwa Tanzania ( ingawa pesa itakayolipwa ni ndogo tofauti na matarajio ya Watanzania) Acacia wataendelea na Kesi yao ambayo wanapanga kuifungua dhidi ya Tanzania. Katika kesi hii ambayo kwa kiasi kikubwa wana uhakika Wa kushinda watadai fidia kubwa mno ambayo ikilipwa itawawezesha kuendesha kampuni yao bila wasiwasi.
HOFU YAO KWA SASA
Hofu yao mpaka sasa ni pale watakapoamua kuishitaki Tanzania basi kuna uwezekano wa kufukuzwa kuendesha shughuli zao hapa nchini. Naam! Hili wamshaliona na wamekubaliana na Barrick namna watakavyoendesha biashara zao hata baada ya kufukuzwa, kwani kama haya yatatatokea Barrick watamiliki hisa zote hata zile zilizokuwa zikimilikwa na Acacia.
Lakini wanaona hawatakuwa na namna ya kurudisha pesa yao zaidi ya kuishitaki Tanzania ambayo mpaka sasa imeshasahau kuwa ndio iliyosaini mikataba na kuiruhusu kampuni ya acacia kuendesha shughuli zao hapa nchini
MPANGO WAO
Barrick wanaweza kulipa hicho kiasi kidogo harafu kwa mkakati mzito acacia watarudisha pesa zaidi ya hizo kwa njia ya mahakama huku wakijifanya kuwa wao hawana habari na mazungumzo yanayoendelea. Ukweli ni kwamba acacia wanahusika chini ya mkakati mzito na Barrick na Leo lao ni kuipiga Tanzania na mpango wao huenda ukafanikiwa.
Mpango wao ukifanikiwa wale mliokuwa mmeshakabidhiwa noa mjiandae kuzirudisha
Ni hayo tu
NIBOZALI WA LUMUMBA