Milele Amina!
Kama unaikumbuka Parokia yako uliyobatizwa basi nenda hapo ukiwa na taarifa zako sahihi kwa maana ya jina lako la Ubatizo, Jina la Baba na la Mama. Pia kama hukumbuki mwaka exactly unaweza wapa range, watacheki kwenye register na wakikupata watakupa Cheti kipya cha Ubatizo kikiwa na details zote!
Sasa ukiisha kipata hicho cheti cha Ubatizo rudi kwenye Parokia yako ya sasa na uongee na uongozi kujua ni kipindi gani mafundisho ya Wakatukumeni yataendeshwa, jiunge nayo na utapatiwa Komunyo ya kwanza na Kipaimara!
Angalizo:
Utafute na Jumuiya mahalia unapoishi ili uwe unasali pamoja na wana jumuiya wenzako, hii itakusaidia sana kwenye process za Masakramenti hayo na hata Ndoa muda ukifika!
Kila la heri na Mungu akuongoze!