Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,809
- 15,421
Tunapopatwa au kuingia kwenye hali ambapo tunajikuta tumeshindwa kufanikiwa au kupata matokeo tuliyoyataka, kuna njia kadhaa katika kuitazama hali hiyo ili isituumize.
Kwanza inabidi tujiulize kama hakuna namna nyingine ya kulitazama jambo au hali inayotukabili. Je, kama mpenzi ametukimbia ni lazima tutazame jambo hilo kama tatizo au tunaweza kulitazama kama mabadiliko ya kimaisha yasiyoepukika?
Pili inabidi tujiulize kama hali hiyo iliyotokea haina faida yoyote kwetu. Ni lazima tutafute aidha katika hali hizi zenye kutuumiza au kutuvunjwa nguvu. Hakuna jambo au tukio lenye upande mmoja tu maishani. Kama wapenzi wametukimbia hatuwezi kuona kuwa huenda wametuepushia matatizo makubwa zaidi, wametupatia nafasi ya kutafakari upya maisha yetu na wametuonyesha kwamba tunahitaji kujikagua upya?Tukitafuta upande mzuri kwenye tukio tunaloliona baya ni lazima tutaupata na huo ndiyo wa kuupa nuvu.
Tatu ni lazima tujifunze kujiuliza kama tukio hilo halijatupatia elimu fulani maishani. Kila tunapopatwa na tatizo au hali yenye kuvunjwa moyo ni lazima tutafute tulichojifunza. Kwa kutafuta tulichojifunza na kukipata, tunakuwa tumepunguza pia uzito wa tatizo tunajihisi kwamba angalau tumejifunza jambo au kitu fulani.
Nne ni vizuri tukajiuliza, ingekuwaje, kama ni rafiki yangu ndiye aliyeingia kwenye tatizo au hali kama hii, ningemshauri nini? Kwa kutafakari jinsi ambavyo ungemshauri, unaweza kujikuta ukiwa umepata ufumbuzi au ahuweni fulani.
Kwa hiyo ni uchaguzi wa mtu mwenyewe kwani ni suala la kuamua tu. Kama tutaamua kuyatazama matatizo yanayotupitia kwa jicho la kujipa moyo, kwa kuwaza vizuri na kuamini kwamba kila ndani a anguko fulani kuna faida tusiyoiona, tutafika mbali. Tukifanya kinyume chake, tutaanguka na hatutaweza kusimama tena.
Kwanza inabidi tujiulize kama hakuna namna nyingine ya kulitazama jambo au hali inayotukabili. Je, kama mpenzi ametukimbia ni lazima tutazame jambo hilo kama tatizo au tunaweza kulitazama kama mabadiliko ya kimaisha yasiyoepukika?
Pili inabidi tujiulize kama hali hiyo iliyotokea haina faida yoyote kwetu. Ni lazima tutafute aidha katika hali hizi zenye kutuumiza au kutuvunjwa nguvu. Hakuna jambo au tukio lenye upande mmoja tu maishani. Kama wapenzi wametukimbia hatuwezi kuona kuwa huenda wametuepushia matatizo makubwa zaidi, wametupatia nafasi ya kutafakari upya maisha yetu na wametuonyesha kwamba tunahitaji kujikagua upya?Tukitafuta upande mzuri kwenye tukio tunaloliona baya ni lazima tutaupata na huo ndiyo wa kuupa nuvu.
Tatu ni lazima tujifunze kujiuliza kama tukio hilo halijatupatia elimu fulani maishani. Kila tunapopatwa na tatizo au hali yenye kuvunjwa moyo ni lazima tutafute tulichojifunza. Kwa kutafuta tulichojifunza na kukipata, tunakuwa tumepunguza pia uzito wa tatizo tunajihisi kwamba angalau tumejifunza jambo au kitu fulani.
Nne ni vizuri tukajiuliza, ingekuwaje, kama ni rafiki yangu ndiye aliyeingia kwenye tatizo au hali kama hii, ningemshauri nini? Kwa kutafakari jinsi ambavyo ungemshauri, unaweza kujikuta ukiwa umepata ufumbuzi au ahuweni fulani.
Kwa hiyo ni uchaguzi wa mtu mwenyewe kwani ni suala la kuamua tu. Kama tutaamua kuyatazama matatizo yanayotupitia kwa jicho la kujipa moyo, kwa kuwaza vizuri na kuamini kwamba kila ndani a anguko fulani kuna faida tusiyoiona, tutafika mbali. Tukifanya kinyume chake, tutaanguka na hatutaweza kusimama tena.