Kama mtu chini ya miaka 18 haruhusiwi kupiga kura, basi iwe marufuku watoto wadogo kufundishwa imani za kidini mpaka wafike miaka 21

Kama mtu chini ya miaka 18 haruhusiwi kupiga kura, basi iwe marufuku watoto wadogo kufundishwa imani za kidini mpaka wafike miaka 21

Mimi naamini Mungu aliyeniumba hana Kabila sasa kwanini nimuombe kwa Lugha ya Kigeni?!

Nitamuomba Mungu kwa Lugha yangu iwe Kiswahili au Kikabila changu.
Kwanza sijui kama kuna imani inasema kwamba ukiomba dua lazima utumie lugha fulani tu na si lugha zengine, mbona tunaona viongozi wa dini wakiomba dua kwa kiswahili wanapokuwa katika shughuli za kiserikali au kisiasa?

Mungu hana kabila kama ulivyosema, sema wewe mtazamo wako kuhusu lugha ndio una shida na ndio maana nikakupa mfano wa kwamba hata hapa Tz kuna mjadala kuhusu lugha ya kufundishia kwa maana wapo wenye kuona kiendelee kutumika kiingereza(lugha ya kigeni) na wapo ambao wanataka kitumike kiswahili.
 
Uko sahihi,tunalazimishwa kuwa uislam na ukirsto ndio dini zenye maana kuzidi za kwetu za asili
Mimi nadhani hizo dini mnazoita za asili ndio zinalazimishwa tena zaidi ya hizi mnazoita za kigeni, kwa sababu zimefungamanishwa na asili na mababu ilivyo ni kama vile ambavyo mtu anatambulika kuwa yeye ni kabila fulani kwa sababu tu ya mzazi wake. Hizo dini za asili hazitoi nafasi ya kuamua uamini au usiamini kwa sababu kwa kutoziamini unaonekana umeacha asili yako na kukana mababu zako hivyo unalazimishwa kwamba walichokuwa wanaamini mababu zetu ndio ilikuwa sahihi kisa mababu zetu.
 
Moja ya mambo yanayovuruga sana wanadamu ni mambo ya imani ambayo msingi wake ni kuamini bila kuhoji na kuhoji ni sawa na kukufuru(unamezeshwa).

Maajabu zaidi ni kuwa tuna vitabu viwili ambavyo ni Bibilia na Quran, lakini kwasababu watu wamekuja na tafsiri zao za haya maandiko, leo tuna madhehebu kibao kwa kila dini wakati Mungu tunaambiwa ni mmoja.

Matokeo ya hali nii mtu anazaliwa na kukulia katika dhehebu fulani mfano mkatoliki, baadae anahama anakuwa mlokole kwa hoja hawezi kukombolewa kupitia ukatoliki au mtu anzaliwa na kukulia katika ukristo, akikua anaona ukristo sio dini sahihi anahamia kwenye uislamu and vice versa.

Kituko kingine ni mtu kubadili dini kisa kuoa au kuolewa. Huu ndio uthibitisho hizi dini sometimes tunaburuzana tu na wala hatuziheshimu kabisa.

Sasa swali linakuja, kwanini mtoto anapozaliwa asiachwe mpaka awe mtu mzima awezi kufanya maamuzi sahihi afuate dini gani na dhehebu gani au asifuate dini kabisa?

Kama tunaona mtu mwenye umri wa chini ya miaka 18 hawezi kuwa na maamuzi sahihi kwenye sanduku la kura, ni kwanini kwenye mambo sensitive kama haya ya kiimani turuhusu watoto kuburuzwa na wazazi wao kiiamini kwa kutakiwa au kuachwa kufuata dini za wazazi wao?

Mtu anapobadili dini au dhehebu, huwa anatubu kuwa alikuwa amepotoka, na kama hatubu, hiyo dhambi ni nani anastahili kuibeba kama sio mzazi au mlezi?

Tukumbuke baadhi ya hizi dini na madhehebu yametokana tu na mitazamo/tafsiri za wanadamu kama sisi.

Tuwaache watoto mpaka watopofikia utu uzima(walau miaka 21) ndio wachague dini na dhehebu au kutokuwa na dini kabisa wakiona ni sahihi kufanya hivyo.

Tubadilike.
We kweli zwazwa, kwa hivyo wafundishwe nini bwege wee
 
Hizo ni Dua lakini kwenye Sala sijawahi kusikia Kiswahili.
Tumetoka kwenye dua na sasa tumeingia kwenye ibada(sala), labda nikuulize kwa jinsi aina ya sala ya waislamu ilivyo wanakusanyika kwa pamoja kuna wakati unakuta ni jamii tofauti tofauti zenye lugha mbalimbali unadhani kikitumika kiswahili kwenye hiyo ibada wote wataelewa hata kama hawakijui kiswahili?
 
Tumetoka kwenye dua na sasa tumeingia kwenye ibada(sala), labda nikuulize kwa jinsi aina ya sala ya waislamu ilivyo wanakusanyika kwa pamoja kuna wakati unakuta ni jamii tofauti tofauti zenye lugha mbalimbali unadhani kikitumika kiswahili kwenye hiyo ibada wote wataelewa hata kama hawakijui kiswahili
Mbona katika Ukristo imewezekana.
 
Mbona katika Ukristo imewezekana.
NIni kimewezekana kwamba wasiojua kiswahili wakienda kwenye makanisa yenye kutumia kiswahili wanaelewa kiswahili?

Kuna ibada makanisani hapa hapa bongo huwa zinafanywa kwa kiingereza. Nilikuwa na rafiki yangu mmoja kutoka Ghana alikuja Tz yeye alikuwa anaenda kanisani ambapo hutumika kiingereza.
 
NIni kimewezekana kwamba wasiojua kiswahili wakienda kwenye makanisa yenye kutumia kiswahili wanaelewa kiswahili?
Kwasababu teyari wanajua Bible Verses na numbers
Mfano Corinthians 13:4–8 👈 teyari inajulikana 13:4-8 kwenye Bibilia ya Kiswahili.
 
Sisi Watanzania tunaelewa zaidi Kiswahili kuliko Lugha za Kigeni.
Ni kweli kabisa mkuu na changamoto iliyochangia kuzaa kizazi kibovu cha kiswahili kinachagizwa na kutokumheshimu baba wa kiswahili bwana shaban robert kama anavyoheshimika shakespear baba wa kingereza
Leo tanzania badala ya mswahili kuheshimika ndio anaonekana mpumbavu
 
Ni kweli kabisa mkuu na changamoto iliyochangia kuzaa kizazi kibovu cha kiswahili kinachagizwa na kutokumheshimu baba wa kiswahili bwana shaban robert kama anavyoheshimika shakespear baba wa kingereza
Leo tanzania badala ya mswahili kuheshimika ndio anaonekana mpumbavu
Uko sahihi.
 
Una Fuvu gumu sana, Quruani ni ujumbe uwe Kiarabu Kiswahili Kijapani Kingereza nk.nk.
Na ujumbe unawafikia watu na hilo ndio lengo kiarabu hakijakwamisha lengo, wewe unaleta habari za uzalendo kwamba kitumike kiswahili tu kusiwe na Qur'an iliyo katika lugha yake ya asili ya kiarabu tuwe na Qur'an ya kiswahili kisa sie ni wazungumzaji wa kiswahili.
 
Na ujumbe unawafikia watu na hilo ndio lengo kiarabu hakijakwamisha lengo, wewe unaleta habari za uzalendo kwamba kitumike kiswahili tu kusiwe na Qur'an iliyo katika lugha yake ya asili ya kiarabu tuwe na Qur'an ya kiswahili kisa sie ni wazungumzaji wa kiswahili.
Allah ni Mwarabu?! Mimi Imhotep ni Mwafrika nina Lugha yangu ya Kisumbwa na kuna Biblia za Kisumbwa.
 
Allah ni Mwarabu?! Mimi Imhotep ni Mwafrika nina Lugha yangu ya Kisumbwa na kuna Biblia za Kisumbwa.
Duh! Mkuu naona aje mtu kukusaidia kuelewa maana narudia yale yale tu. Hiyo biblia ya kisumbwa ni tafsiri ya biblia kwa kisumbwa kama ambavyo biblia ilivyo tafsriwa kwa lugha zengine pia. Sasa nimekwambia hata Qur'an imetafsiriwa kwa lugha zengine pia ikiwemo na kiswahili.

Sasa tatizo mara utasema hujaona watu wakisoma Qur'an kwa kiswahili mara kusali kwa kiswahili, hauelewi na hauelewi unachozungumzia.
 
Back
Top Bottom