Kama Mungu hayupo, umaarufu wake unatoka wapi?

Kama Mungu hayupo, umaarufu wake unatoka wapi?

ukitaka kupima akili ya mtu zungumzia swala la mungu ndio unaweza kugundua kwamba humu jf kuna matahira wengi sana.
lakini ninauhakika kufikia mwaka 2050 watanzania wengi watakuwa wamejua mungu hayupo.
Na hii ndio inaprove zaidi uwepo wake kwa wake waaminio haya yote yalishatabiriwa nyakati hizi.
 
Anakwambia uwezo wa mungu hauchunguziki, hapo kashakuambia mungu ni yule yule jana leo na milele.

Kama uwezo wa mungu hauchunguziki, huyu kajuaje mungu ni yule yule jana leo na milele?
Mungu ni yuleyule maana yake tabia zake hazibadiliki we di reflect his word which is never change his principles are forever the same.
 
Mbona vipo vitu vingi sana vimetungwa ni maarufu na wakati ni vya kufikirika tu mfano spiderman na babu krismasi(santa claus)

Kitu kuwa maarufu haukifanyi hicho kitu kuwa halisi hata kidogo.
 
ukitaka kupima akili ya mtu zungumzia swala la mungu ndio unaweza kugundua kwamba humu jf kuna matahira wengi sana.
lakini ninauhakika kufikia mwaka 2050 watanzania wengi watakuwa wamejua mungu hayupo.
Shetani, mapepo na majini yapo au hayapo?
 
Mungu hayupo.

Idea ya Mungu kuwapo inapata umaarufu kwa sababu watu wengi wavivu hawataki kufikiri na hawataki kuchukua responsibility, wanataka mungu awepo ili achukue dhamana ya kutatua mambo yote.

Pia watu wengi hawafikirii logically, wanafikiria emotionaly.

Pia watu wengi wanaogopa kusema wanachofikiri na ku question uwepo wa mungu kwa sababu wanaogopa kuonekana wako tofauti.

Pia kusema huamini kuwepo mungu kunaweza kukukosanisha na familia, jamaa, rafiki, kazini etc.

Kitu kukubalika haina maana ni cha kweli. Kuna wakati watu waliamini dunia ni bapa na si tufe. Hilo halikufanya dunia iwe bapa.

Kuna wakati watu waliamini jua linazunguka dunia. Hilo halikufanya jua lizunguke dunia.

Hata kama watu wote wataamini mungu yupo, kama hayupo hayupo tu.

Kama unasema mungu yupo, thibitisha mungu yupo.

Bravo mkuu Kiranga upo?
 
Nipo sana tu. Labda tunapishana tu hapa.

Sijapata majibu ya maswali yangu bado.

Hawawezi kujibu kabisa.Lile swali lako la "Kwa nini mungu mwenye uwezo wote akaumba dunia yenye maovu wakati alikuwa na uwezo wa kuumba dunia ambayo maovu hayawezekaniki?" Linawaumiza vichwa.
. ....Free ideas......
 
Mungu hayupo.

Idea ya Mungu kuwapo inapata umaarufu kwa sababu watu wengi wavivu hawataki kufikiri na hawataki kuchukua responsibility, wanataka mungu awepo ili achukue dhamana ya kutatua mambo yote.

Pia watu wengi hawafikirii logically, wanafikiria emotionaly.

Pia watu wengi wanaogopa kusema wanachofikiri na ku question uwepo wa mungu kwa sababu wanaogopa kuonekana wako tofauti.

Pia kusema huamini kuwepo mungu kunaweza kukukosanisha na familia, jamaa, rafiki, kazini etc.

Kitu kukubalika haina maana ni cha kweli. Kuna wakati watu waliamini dunia ni bapa na si tufe. Hilo halikufanya dunia iwe bapa.

Kuna wakati watu waliamini jua linazunguka dunia. Hilo halikufanya jua lizunguke dunia.

Hata kama watu wote wataamini mungu yupo, kama hayupo hayupo tu.

Kama unasema mungu yupo, thibitisha mungu yupo.
Ya wew ndio mvivu kufikilia kama ukaa darasani kidogo tu kwa elimu yetu ya bongo inaweza kukisaidi
kuthibisha uwepo wake ,kwani hadhihiliki kwa milango ya fahamu,labda nikuulize swali moja we unaamini uchawi upo?
 
Ya wew ndio mvivu kufikilia kama ukaa darasani kidogo tu kwa elimu yetu ya bongo inaweza kukisaidi
kuthibisha uwepo wake ,kwani hadhihiliki kwa milango ya fahamu,labda nikuulize swali moja we unaamini uchawi upo?
Wewe unayenisema mimi mvivu ni mvivu kiasi hata spelling za Kiswahili zinakushinda.

Hujui kwamba "kufikilia" si neno la Kiswahili in context, neno sahihi ni "kufikiria"?

Hujui kwamba "hadhihiliki" si neno la Kwahili, neno sahihi ni "hadhihiriki" ?

Wewe unayenisema mimi kwamba mungu hadhihiriki kwa milango ya fahamu unatumia nini kumuelewa?

Wapi umeona nimeishia kwenye milango ya fahamu?

Mimi siamini uchawi, kwa nini niamini uchawi?

Kwa nini mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote kaumba ulimwengu ambao uovu unawezekana wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao uovu hauwezekani?
 
Hayo ni makosa ya kawaida ila nitakufahamisha Leo uondokane na hiyo hali yako uliyo NATO naamini umetengenezwa kuwa hivyo,hacha sisi tunao fikili tukusaidie
 
Back
Top Bottom